mathsjery
JF-Expert Member
- Sep 26, 2015
- 2,249
- 1,813
Kuna tabia ya wazazi ama walezi wenye marafiki mbalimbali pia hata majirani kuwaambia watoto wao kuwa, waitane kaka na dada ama mjomba ama aunt. Hapa sijaeleweka ngoja nitoe mfano.
Wewe una mtoto mdogo na jirani yako naye ana mtoto mdogo, yule mtoto wako ukamsikia anamsalimia yule jirani yako shikamoo, basi ukamkemea huku ukisema sema shikamoo mama mdogo ama shikamoo mjomba, ama shikamo bibi.
Huyu mtoto akikuwa akajua kuwa wale si ndugu zake bado ataendelea kuwapa salamu za undugu.
Sasa shida iko hapa:
Je, mwanao akimpenda binti wa rafiki yako wa karibu, ama jirani yako ambaye umekuwa ulimwambia amwite mama mdogo, shangazi au dada je, itakuwa rahisi kwake kumuoa/kuolewa naye maana bado kuna hiyo mentality ndani yake ya kuitana kaka na dada sijui mjomba na hakuna undugu wowote.
Vipi hamna namna ya kumsalimu mtu mzima asiye ndugu yako? Hivi ndo tunakosa wake zetu kwa undugu fake.
NB maoni yenu
Wewe una mtoto mdogo na jirani yako naye ana mtoto mdogo, yule mtoto wako ukamsikia anamsalimia yule jirani yako shikamoo, basi ukamkemea huku ukisema sema shikamoo mama mdogo ama shikamoo mjomba, ama shikamo bibi.
Huyu mtoto akikuwa akajua kuwa wale si ndugu zake bado ataendelea kuwapa salamu za undugu.
Sasa shida iko hapa:
Je, mwanao akimpenda binti wa rafiki yako wa karibu, ama jirani yako ambaye umekuwa ulimwambia amwite mama mdogo, shangazi au dada je, itakuwa rahisi kwake kumuoa/kuolewa naye maana bado kuna hiyo mentality ndani yake ya kuitana kaka na dada sijui mjomba na hakuna undugu wowote.
Vipi hamna namna ya kumsalimu mtu mzima asiye ndugu yako? Hivi ndo tunakosa wake zetu kwa undugu fake.
NB maoni yenu