Wazazi wenye Wachezaji hawa wafuatao wa Yanga SC waonyeni wasikubali kubebeshwa ' Hirizi ' mtawakosa

Wazazi wenye Wachezaji hawa wafuatao wa Yanga SC waonyeni wasikubali kubebeshwa ' Hirizi ' mtawakosa

GENTAMYCINE

JF-Expert Member
Joined
Jul 13, 2013
Posts
60,660
Reaction score
121,325
Kwa taarifa za ndani kabisa ambazo nimehangaika mno kuzinyaka / kuzipata kutoka katika Klabu ya Yanga zinasema kwamba kuna Wachezaji Watatu ambao ni Wakristo inasemekana wanalazimishwa ili wabebe ' Hirizi ' kuweza kuisaidia Yanga SC katika mechi yake na Simba SC tarehe 29 April 2018 kutokana na ' Nyota ' zao Kung'aa.

Wachezaji hao ni:

  1. Kelvin Yondan
  2. Raphael Daud
  3. Gadiel Michael
Nikiwa kama mmoja wa Watu ambao tumeamua kuingia ' chimbo ' ili kuweza kuisaidia Simba SC ishinde siku hiyo natoa ' ONYO ' mapema kwa Wazazi wa hawa Wachezaji tajwa hapo juu kwamba wawawahi na wawazuie kutumika na Yanga SC kubeba ' Hirizi ' kwani kwa tulichokifanya Simba SC hasa Kamati yetu ya Ufundi ( Ushirikina )kuna uwezekano hawa Wachezaji kama kweli wakibeba tusiwe nao tena Ulimwenguni.

Nimetoa ONYO mapema na tusije tukalaumiana tafadhali. Ukiona mpaka GENTAMYCINE najitoa mhanga na kuwa mbele Kukesha kwa Mchina / Uwanja wa Taifa na kufanya mambo ya ' Kufuru ' kwa ajili ya kuipigania Simba SC yangu jua ya kwamba safari hii nimeamua kweli na kilichofanyika kuna Watu hiyo tarehe 29 April 2018 hawataamini kitakachowatokea na si ajabu wanaweza hata wakaiomba TFF wasiwapangie tena kucheza na Simba SC na badala yake kila mechi yao ya Simba SC wakaiomba tu TFF iwape points zao Simba SC.

Kama umekaa hapo na unajishauri au bado hujapata Tiketi yako halafu ni mwana Simba SC fanya upesi / haraka sana wahi kajipatie Tiketi yako ili ushuhudie Kipigo cha ' Karne ' ambacho watakutana nacho Wazee wa Mafuriko na Uogeleaji kitakachowafanya hata wapigane na wafukuzane Klabuni Kwao.

Mpaka muda huu bado naziona Goli / Bao Saba ( 7 ) huku nikiona Wachezaji wawili wa Simba SC wanaoanzia na Majina yenye Herufi E, J na S wakifunga hayo magoli yote ambapo hao E na J watafunga ' hat trick ' na huyo S atafunga 1. Na kwa upande wa pili kwa Kikosi cha Mafuriko na Uogeleaji jijini Dar es Salaam naona Kadi Nyekundu moja kwa Mchezaji mwenye jina linaloanzia na herufi K au R na kuna uwezekano Watu zaidi ya 500 wakazimia Kesho wote wakitokea upande wa watakaofungwa hivyo nitoe tu RAI yangu mapema kwa Red Cross Tanzania kwamba waanze kupasha moto miili yao kwani hiyo Siku watakuwa na Kazi ya ziada kuwaokoa Watu pale kwa Mchina / Uwanja wa Taifa.

Nawasilisha.
 
So mnataka kuwauwa???

Kilichofanyika na ' Majini ' tuliyoyatumia hilo ulilolisema laweza kutokea Mkuu kama wasipokuwa makini na kuchukua huu ushauri wangu na kama uko karibu na Wazazi wa hao Wachezaji waambie wawaambie wasikubali kubebeshwa ' Hirizi ' kwani Mimi mwenyewe niliyeko katika Kamati naogopa sasa Wao itakuwaje? Una Kifua Mkuu? Kama unacho nakuomba leo usiku Saa 5 njoo Uwanja wa Taifa upande ule kama unaenda Indoor Stadium uone nini kitafanyika ndipo utajua kuwa safari hii ' Mnyama ' hatutanii na hatuna utani na Mtu iwe jua iwe mvua tarehe 29 April 2018 lazima Wazee wa Mafuriko na Uogeleaji ' wazikoge ' nyingi sana hadi watuamkie Shikamoo.
 
Huu mpira wa bongo hautafika popote kwa hizo imani zenu za kishirikina kila kukicha!

Tuachie mpira Wetu wa Bongo tafadhali na Wewe endelea kuufuatilia huo huo wa Ulaya ukidhani kwamba wao hawarogi.
 
Huu mpira wa bongo hautafika popote kwa hizo imani zenu za kishirikina kila kukicha!
Wacha tudumishe tamaduni zetu..!Unaweza kukuta wewe mwenyewe una ‘chuma’ kiuononi,ukiwa kwenye keyboard unajifanya kukataa
 
Wacha tudumishe tamaduni zetu..!Unaweza kukuta wewe mwenyewe una ‘chuma’ kiuononi,ukiwa kwenye keyboard unajifanya kukataa

Kwa uzoefu wangu mkubwa tu ni kwamba mara nyingi wale Watu ambao huwa wanasema wanachukia ushirikina / ulozi / fusho ndiyo huwa Wanachama wa Kutukuka wa hayo mambo Mkuu. Amini haya maneno yangu na ndiyo hata ukienda katika Nyumba za Ibada huwakosi ' Front Seats '.
 
Mbongo hakutakaa kuwe na soka!

Una uhakika kwamba huko Ulaya hawarogi? Ni mara ngapi tumeshudia Mipaka Shume ikikatiza bila aibu katika mechi za Arsenal, Bayern na hata Barcelona? Wale Nguchiro nao huwa wanatokea wapi? Acheni Unafiki hapa.
 
Back
Top Bottom