MAMMAMIA
JF-Expert Member
- Feb 26, 2008
- 3,811
- 1,607
Hii ni hadithi tu lakini ndni yake kuna ukweli na mafunzo.
Bwana mmoja, kwa kushirikiana na mke wake, walikuwa wanamdhalilisha babake yule bwana. Mfano, wakati wa kula walikuwa, wanampa chakula katika vyombo chakavu, wanamtenga hawakai nae mezani kwa sababu wakati anakula anadondosha, anatoka mate ovyo n.k.
Siku moja wakati wa chakula walikuwa wanamtafuta mtoto wao msichana akawa haonekani. Walimtafuta hatimaye wakamkuta yuko uwani anachezea udongo mfinyanzi.
Wakati wa kula tayari, unafanya nini hapo?", babake alimwuliza.
"Ninatengeneza sahani na vikombe kwa ajili yenu mtakapokuwa wazee kama babu".
Ndugu zangu:
Tusisahau tabu walizopata mama zetu tukiwa tumboni miezi bila kujua kama tutazaliwa hai au tumekufa, wazima au walemavu.
Tusisahau pale tulipokuwa wachanga tulienda haja mwilini mwao.
Tusisahau maili walizokuwa wanatembea usiku chumbani, sisi mikononi, migongoni au mabegani mwao.
Tusisahau tulipokuwa tunalia bila ya wao kujua tuna nini wakati bado hutujui kusema.
Tusisahau walivyokuwa wanajinyima hali na mali ili kutupa malezi, hifadhi, ulinzi, chakula, nguo, matibabu, elimu....
Na zaidi, tusisahau kuwa chochote tunachomiliki, hadhi yoyte tulonayo, wasingekuwa wao tusingefika hapa tulipo leo.
Tukumbuke, tunavyowafanyia wazazi wetu leo, watoto wetu wanaweza kutufanyia hivyohivyo. Tusije wakatutengenezea sahani za udongo tutapokuwa wazee kama babu.
Bwana mmoja, kwa kushirikiana na mke wake, walikuwa wanamdhalilisha babake yule bwana. Mfano, wakati wa kula walikuwa, wanampa chakula katika vyombo chakavu, wanamtenga hawakai nae mezani kwa sababu wakati anakula anadondosha, anatoka mate ovyo n.k.
Siku moja wakati wa chakula walikuwa wanamtafuta mtoto wao msichana akawa haonekani. Walimtafuta hatimaye wakamkuta yuko uwani anachezea udongo mfinyanzi.
Wakati wa kula tayari, unafanya nini hapo?", babake alimwuliza.
"Ninatengeneza sahani na vikombe kwa ajili yenu mtakapokuwa wazee kama babu".
Ndugu zangu:
Tusisahau tabu walizopata mama zetu tukiwa tumboni miezi bila kujua kama tutazaliwa hai au tumekufa, wazima au walemavu.
Tusisahau pale tulipokuwa wachanga tulienda haja mwilini mwao.
Tusisahau maili walizokuwa wanatembea usiku chumbani, sisi mikononi, migongoni au mabegani mwao.
Tusisahau tulipokuwa tunalia bila ya wao kujua tuna nini wakati bado hutujui kusema.
Tusisahau walivyokuwa wanajinyima hali na mali ili kutupa malezi, hifadhi, ulinzi, chakula, nguo, matibabu, elimu....
Na zaidi, tusisahau kuwa chochote tunachomiliki, hadhi yoyte tulonayo, wasingekuwa wao tusingefika hapa tulipo leo.
Tukumbuke, tunavyowafanyia wazazi wetu leo, watoto wetu wanaweza kutufanyia hivyohivyo. Tusije wakatutengenezea sahani za udongo tutapokuwa wazee kama babu.