Kipindi hiki ajira ngumu akatokea jamaa tulisoma naye O level akasema mjomba ake ana ishu ya kutulink na Tanesco elimu inayohitajika ni form four tu.
Ila inahitajika tumpe 73k na watu wanahitajika haraka mno ndani ya wiki 2 nafasi ziwe zimejazwa, kuanzia hiyo siku tuliyopata mchongo, mshahara 600k.
Mi hua fasta sana kudetect scam na scammer. Sheria kuu ni hii "Ukiona mchongo ni mtamu kuliko utamu wenyewe achana nao" sasa 73k kwa 600k ni mchongo mtam mno, kufikia hapo nikadetect hii ni scam.
Wadau tukaomba kuonana na jamaa, akaja. Nikaangalia mavazi, namna anavyoongea na ndevu zake alivyoamua kuzitunza na jinsi anavyojibu maswali (alikua anakazana sana na neno "Niaminini mimi" "Mnaweza kuja hata ofisini", tukaachana naye. Tukabaki wadau sita tunaotaka hizo nafasi tukaanza kujadiliana.
Tukamuuliza yule rafiki yetu mjomba wako una uhakika anafanya kazi Tanesco? Akajibu hua anaonana naye kwa babu tu hua hana stori naye na alicheki na shangazi yao akasema anavyojua jamaa anafanya kazi Coca. Lakini pia jamaa anaishi kwa kujitenga mno.
Tukamwambia mpange jamaa kua hii 73k siyo kubwa sisi tunataka tumpe shukrani kubwa, atuache tuingie kazini tutagawana naye mshahara. Jamaa akagoma.
Tukasema basi tukupe hiyo 73k tukiingia ofisini akagoma pia kwa madai mkono mtupu haulambwi.
Kufikia hapa nikakamilisha kua huyu ni scammer, unakataaje 1.8m over 438k? Nikawaambia wadau huyu mwana hafai.
Wakajibu ila 73k ni ndogo, nikasema zikishakua nyingi hazitakua 73k, mmoja akajibu jiangalie wewe ulichotoa siyo na cha wenzako. Nikamuuliza akienda dukani akiambiwa hii feni ni 80k atasema hawezi kununua kwakua ana 73k ya Castr na hawezi ichanganya na yako?
Mi nikasema hii deal mi najivua. Wana wakasema we are giving it a try nikawajibu poa.
Kesho yake wakampelekea jamaa pesa na cv zao, hiyo ilikua mwezi wa 3 mpaka leo wanazungushana na yule bwana.
NB. Kama tulikua wote pale kikaoni siku ile tafadhali usitaje jina langu hapa, wala usije pm.