Waziri aliyetemwa na JK achukua fomu kupambana na Sitta Uenyekiti Bunge la Katiba

Waziri aliyetemwa na JK achukua fomu kupambana na Sitta Uenyekiti Bunge la Katiba

BONGOLALA Wanawake hawapendani hata kidogo na hasa kukiwa na uwanja huru wa ushindani
 
Last edited by a moderator:
huu ni mtihani kwa wajumbe wanawake kumchagua mama Thereza Huviza, sababu idadi ya wajumbe wanaume na wajumbe wanawake inakaribia kulingana.
 
Suala siyo kuwa mwanamke ila ana uwezo? Aliwahi wapi kuongoza mabaraza makubwa vile tena yenye watu wa kila sampuli kuanzia maprofesa hadi waganga wa kienyeji.
 
Nampongeza atleast ameweka sawa ule usemi tupeni nafasi tunaweza.Amepewa nafasi amechukua form,kama uwezo anao wanawake wanahaki ya kumpigia, lakini huwezi kumchagua tu mtu sababu ya jinsia yake hata kama uwezo hana.:whoo:
nakubaliana na wewe kuwa huwezi kumchagua tu mtu kwa sababu ya jinsia yake hata kama uwezo hana!bunge hili si la kulilia uenyekiti mwanamke watu ni full majanga!
 
mhalisi usitegemee wanawake hata kumpigia kura mwanamke mwenzao. Ni wanafiki na wasiopendana daima
 
Last edited by a moderator:
huu ni mtihani kwa wajumbe wanawake kumchagua mama Thereza Huviza, sababu idadi ya wajumbe wanaume na wajumbe wanawake inakaribia kulingana.
Akipata kura sawa na nusu ya wajumbe wote wanawake nitafute uchukue zawadi yako.
 
Akipata kura sawa na nusu ya wajumbe wote wanawake nitafute uchukue zawadi yako.

kwa jinsi wanawake amabao ni viongozi wanavyosikika wakipigania usawa wa kinjisia, pengine mtu unaweza kufikiri wanawake hao wana utofauti na wanawake walio wengi.
 
Dr Huviza ni mzigo mzigo mzigo. Na kama si kelele za jinsia huyo mama asingepata uwaziri, na hata hivyo uvumilivu ulifikia mwisho, akatemwa.

Kwenye hili bunge maalam, maana wameweka jinsia na nchi kama vigezo vya kuwania vyeo basi mwenyekiti akiwa mwanaume toka bara, makamu wake awe mwanamke toka Zanzibar na awe wa chama tofauti na mwenyekiti. Hayo ndiyo matekeo ya kuingiza usanii wa kibaguzi.
 
nakubaliana na wewe kuwa huwezi kumchagua tu mtu kwa sababu ya jinsia yake hata kama uwezo hana!bunge hili si la kulilia uenyekiti mwanamke watu ni full majanga!

Kaka tatizo hatujaielewa Beijing,mpaka tukija kuielewa tumekosa opportunity nyingi sana.
 
hivi ni kura ya siri au ya wazi kwenye huo uchaguzi
 
Kaka tatizo hatujaielewa Beijing,mpaka tukija kuielewa tumekosa opportunity nyingi sana.

haya mambo ya mwanamke kutawala/kuongoza. kibinadamu si kitu ila ki Mbingu, ni mambo makubwa sana yanahitaji kupingwa kwa guvu.
 
Hivi na wewe ni mjumbe...lol kweli tunamhtaji mungu aingilie kati kama michango yako ndo itakuwa kama ya jamii forum no expectations
Mkuu acha tu, nilisikitika sana huyo jamaa alivyosema na yeye ni mjumbe wa hilo Bunge.
 
haya mambo ya mwanamke kutawala/kuongoza. kibinadamu si kitu ila ki Mbingu, ni mambo makubwa sana yanahitaji kupingwa kwa guvu.

Kuongoza ni haki ya kila binadamu,soma kitabu cha Esther ndiyo utajua nguvu ya mwanamke na uongozi.Hata familia zetu nyingi muongozaji ni Mama na si Baba.Angalia familia ambazo Mama ametangulia kufariki nyingi zimesambaratika lakini angalia zile ambazo Baba ametangulia ni chache sana zimesambaratika.

Kinachotakiwa ni uwezo wake katika kuongoza na si jinsia yake katika kuongoza.Sijasema Mwanamke achukue nafasi ya Mwanaume,la hasha,kinachotakiwa mwanamke apewe fursa sawa na mwanaume katika kugombea uongozi na achaguliwe si kwa sababu ya jinsia yake bali kwa sababu ya uwezo wake.
 
Nadhani ni busara akichaguliwa mtu mwenye uwezo kuliko kuangalia ni mwanamke au mwanaume.
 
Back
Top Bottom