Waziri Aweso ateua Mkurugenzi Mpya wa Maji Morogoro, aelekeza iundwe timu maalum ya Wataalam

Waziri Aweso ateua Mkurugenzi Mpya wa Maji Morogoro, aelekeza iundwe timu maalum ya Wataalam

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Joined
Apr 18, 2017
Posts
3,984
Reaction score
13,760
WhatsApp Image 2025-02-22 at 18.43.16_eab93100.jpg
Waziri wa Maji, Jumaa Hamidu Aweso leo terehe 22 February 2025 amefanya mabadiliko ya kiutendaji katika Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Morogoro (MORUWASA).

Waziri Aweso kwa Mamlaka aliopewa na Sheria ya Huduma za Maji na Usafi wa Mazingira Na. 5/2019 amemteua CPA Sais Andongile Kyejo kuwa Mkurugenzi Mtendaji MORUWASA.

Ndugu Kyejo alikuwa ni Mkurugenzi wa Fedha Mamlaka ya Maji na Usafi wa Mazingira Dar Es Salaam (DAWASA) na atachukua nafasi ya Eng Tamimu Katakweba aliekuwa Mkurugenzi Mtendaji wa MORUWASA.

Aidha, Waziri Aweso amemuelekeza katibu Mkuu wa Wizara ya Maji Mhandisi Mwajuma Waziri kuunda timu maalumu ya Wataalamu watakaofanyia kazi changamoto za hali ya huduma ya upatikanaji wa Maji Manispaa ya Morogoro na maeneo yote yanayohudumiwa na MORUWASA katika kipindi ambacho utekelezaji wa Mradi mkubwa wa Maji unaendelea.
WhatsApp Image 2025-02-22 at 18.43.17_5df31266.jpg

CPA Sais Andongile Kyejo
Pia soma:
~
Waziri Aweso unasema DAWASA kuna hujuma? Njoo Morogoro, huduma ya Maji ni kero kubwa
~ Morogoro: Meneja wa MORUWASA asimamishwa kazi
 
Eti Morogoro kuna shida ya Maji. Drama haziishu hii nchi.

Ukosefu wa Maji Morogoro kuna watu wananufaika. Wakiwemo MORUWASA wenyewe.

Fuatilia uone kwente treatment plant yao ya Iringa Rd pale wanavyouza maji kwenye yale magari ya kusambaza maji (Madoza).

Kwahiyo wanatengeneza tatizo ili wauze solution.
 
Back
Top Bottom