Waziri Bashe, wauzaji wengi wa pembejeo za kilimo hawana utaalamu wa kilimo na mifugo

Waziri Bashe, wauzaji wengi wa pembejeo za kilimo hawana utaalamu wa kilimo na mifugo

baba anjela

JF-Expert Member
Joined
Mar 17, 2013
Posts
431
Reaction score
310
Mh Bashe , wewe ni miongoni mwa mawaziri mnaochapakazi na zinaonekana, hongera sana.

Ombi langu kwako nalielekeza kwenye maduka ya pembejeo za kilimo na mifugo...kwakweli kumejaa makanjanja wengi sana. Wauzaji wao wengi hawana utaalamu wa kilimo au mifugo.

Na wale walio na wataalamu basi ni level ya diploma au certificate... na kichwani mwao sifuri tupu. Wewe jaribu kufanya utafiti wako binafsi utagundua jinsi wakulima na wafugaji wanavyopata hasara kubwa hasa katika upande wa madawa mpaka upate dawa sahihi ya ugonjwa utajikuta umenunua dawa tofauti zaidi ya tatu au nne ni kama vile wanabahatisha katika kutibu ugonjwa...na hapo unakuta dawa moja si chini ya 13, 000 sasa piga hesabu , mpaka unavuna au unapeleka kuku sokoni umeingia hasara kiasi gani, wao ni chanzo cha mifugo kufa au mazao kuharibika.

Nilijaribu kufanya utafiti mdogo tu...ni lilima matikiti maji , ukaingia ugonjwa (mdudu mafuta) nikachuma matawi kama matano nikapeleka hiyo sample maduka kama kumi tofauti cha kushangaza maduka yote yalinipa majibu tofauti tofauti na dawa tofauti hakuna majibu yaliyofanana kabisa.

Mh Bashe, jaribu kutazama kwa jicho la tatu. Haya maduka yanachangia sana vijana wengi kuona kilimo na ufugaji ni hasara na hakuna faida.

Haya maduka wanatengeneza faida sana , nijukumu la serikali kuwawekea utaratibu juu ya wataalamu wao na ikibidi kuwafanyia snap check mara kwa mara ili kulinda uduma bora.
 
Maduka ya dawa na pembejeo mengi yanamilikiwa na maafisa mifugo na kilimo sema wanaajiri watu makanjanja sababu ya kutafuta cheap labor na pia sababu kwenye hiyo sekta hakukuwa na usimamizi wa karibu Yani mifugo na kilimo imeonekana Kama kichaka fulani.

Kiukweli ni kwamba wanaouza dawa za mifugo kwanza wanatupiga sana, mtu anajua kabisa huyu ng'ombe anahitaji sindano ya dawa fulani Ila daktari anakuja anakuandikia lundo la madawa ilimradi akufanye ununue zaidi sababu duka ni la kwake.

Kwenye kilimo nako usiseme, dawa, mbolea mbegu unakuta hazifai Ila anakupa tu.

Ng'ombe anatakiwa apigwe sindano ya mg kadhaa yeye anachanganya na maji kidogo Yani uhuni tu.

Hii sekta bila kuweka udhibiti haitaendelea na tutaendela kumuumiza mkulima na mfugaji.
 
Inshu sio wauzaj,ni aina ya makampuni ama viwanda.hayo nayashuhudia hapa home,unakuta mtu anahitaj dawa fulan anakwenda kutibu tatzo haijamsaidia.akirud,unampa dawa aina nyngine ya kampun unakuta inamsadia.pia dawa hz kama katika kilimo penda kufuata kila hatua inavyostahil ukikosea tu,utajuta.mi naona kwanza tuanze na viwanda halafu mengine tuangalie
 
Hii siyo kweli kwa asilimia kubwa. Kati ya mwaka 2016 to 2021, kulikuwa na mradi mkubwa uliojulikana kama TIJA TANZANIA. Mradi huo uliofadhiliwa na AGRA, ulifanikisha mafunzo kwa wauza pembejeo mamia kwa mamia. Mafunzo hayo yalisimamiwa na kuratibiwa na TPRI.

Kwa hiyo wataalamu wapo wa kutosha. Mafunzo ya mwisho yalifanyika Kigoma 2021 Oct. Wengi wa wahitimu wana maduka ya pembejeo na wanafanya vizuri.

Kwa sasa wengi wameunda magrupu ya whatsapp na facebook kwa ajili ya kushare ujuzi. Lakini nashauri kama kuna swala technical, mwenye shida yeyote aanzie kwa afisa ugani. Kumbuka, huwezi kwenda famasi bila kuandikiwa dawa na daktari.
 
Mkuu mimi naona kama unawaonea tu hawa wenye maduka ya pembejeo za kilimo pamoja na mifugo. Kwanza tuwashukuru kwa kujituma kwao kutuletea madawa hayo hadi huku vijijini. Bila wao kilimo na ufugaji ungekuwa kwenye hali mbaya sana. Aidha hao wauzaji ni kweli wengi wao hawamudu sawa utambuzi wa magonjwa ya mazao ya kilimo na wanyama, hawalazimiki kujua vyote. Mimi nadhani wa kuwalaumu huko vijijini ni mabwana na mabibi kilimo maana wao ndio wasomi na wataalamu wa hayo magonjwa na matumizi yake kwenye mazao na mifugo na wapo hapo kijijini ama Kata kwa kazi hiyo.

Kwa muda mrefu wakulima wengi hapa nchini wanalima bila msaada ama mwongozo wa maafisa kilimo, wengi wao hawana uzoefu katika kutatua namna ya kupambana na wadudu waharibifu pamoja na magonjwa yake kwenye mazao huko mashambani. Aidha wengi wao hawana hata faili ama kalenda za kuwaongoza katika shughuli zao kwa wakuliwa wao, kwa mantiki hiyo wakati mwingine wakulima waona ni bora kuulizana wao kwa wao. Ni jambo la kawaida sana huko vijijini kukuta shamba la mwanakijiji mkulima limesitawi vizuri kuliko la Afisa kilimo.
 
We jamaaa mweupe kaka kopo tupu yaaana badala umwambie apambane pembejeo zishuke bei unapiga kelele eti wauzaji?
Mkuu Ridomill gold, polepole basi haya mambo ya kuelimishana kwenye kilimo hayataki hasira. Jina lako tu kwenye kilimo linaheshimika sana. Linatatua magonjwa mengi sana, wakulima wengine bila kuwa na ridomill gold kwanza - halimi.

Kwa kweli bei za pembejeo za kilimo ziko juu kwa zaidi ya asilimia 100 (100%>) Nazani ni wakati mwafaka kwa Waziri wa Kilimo akatueleza vigezo vyake alivyotumia hadi kufikia bei kupanda kwa zaidi ya asilimia 100, huku akitilia maanani kuwa wakati wa Rais Msitaafu Kikwete bei ya mbolea ilikuwa nafuu sana lakini yeye aliwapatia wakulima ruzuku na hivyo kununua mbolea kwa bei ya chini sana na hivyo kumuwezesha kila mkulima kulima kwa mbolea AU wakati wa Baba wa Taifa alipo kuwa anagawa bure mbolea kwa wakulima ama wakati mwingine anatoa ruzuku.
Kwa heshima na taadhima tuomba Waziri wa Kilimo, awaondolee Wakulima mzigo huu.
 
We jamaaa mweupe kaka kopo tupu yaaana badala umwambie apambane pembejeo zishuke bei unapiga kelele eti wauzaji?
Sasa matusi ya nini ...hii ni mitazamo ..ukiona nimesema hivyo tambua ndipo maumivu yangu yalipo,usitake maumivu yako ndiyo yawe ya kwangu, huu ni mtazamo wangu mimi ... kama hoja yangu kwako haina mashiko... ignore then andika ujumbe wako...watu wote hatuwezi tukawa na mitazamo inayofanana..... au matatizo yanayofanana..
 
Hoja ni kushusha bei ya pembejeo wakuluma walime mazao yao na wapate mavuno yenye uhakika izo swaga zungne watajadiliana na wamiliki wa maduka badae

Asitake kuyumbisha wakulima kwann abadilishe gia wakulima wanalia na bei ya pembejeo na sio elimu ya waudumu wa maduka ya mifungo na kilimo
 
Kabla ya kwenda ktk duka la pembejeo; unatakiwa uonane na daktari (afisa ugani/mifugo)

Yeye atakueleza tatizo hilo unatakiwa kutibu kwa dawa yenye kiambata gani (usiulize jina la biashara uliza kiambata) na kwa dose gani

Baada ya hapo utaenda ktk duka la pembejeo/mifugo kununua dawa husika

Kuhusu kila duka kuambiwa dawa tofauti.. inawezekana kwa sababu makampuni yanayozalisha dawa za kilimo ni mengi

Kwa hiyo zinaweza kuwa dawa za makampuni 20 ila kazi yake moja.

Kikubwa serikali ijikite ktk kudhibiti uuzwaji holela wa dawa na wakulima pia wajiepushe na ununuzi holela au kutumia dawa kwa mazoea bila ushauri wa kitaalam
 
Mh Bashe , wewe ni miongoni mwa mawaziri mnaochapakazi na zinaonekana, hongera sana.

Ombi langu kwako nalielekeza kwenye maduka ya pembejeo za kilimo na mifugo...kwakweli kumejaa makanjanja wengi sana. Wauzaji wao wengi hawana utaalamu wa kilimo au mifugo.

Na wale walio na wataalamu basi ni level ya diploma au certificate... na kichwani mwao sifuri tupu. Wewe jaribu kufanya utafiti wako binafsi utagundua jinsi wakulima na wafugaji wanavyopata hasara kubwa hasa katika upande wa madawa mpaka upate dawa sahihi ya ugonjwa utajikuta umenunua dawa tofauti zaidi ya tatu au nne ni kama vile wanabahatisha katika kutibu ugonjwa...na hapo unakuta dawa moja si chini ya 13, 000 sasa piga hesabu , mpaka unavuna au unapeleka kuku sokoni umeingia hasara kiasi gani, wao ni chanzo cha mifugo kufa au mazao kuharibika.

Nilijaribu kufanya utafiti mdogo tu...ni lilima matikiti maji , ukaingia ugonjwa (mdudu mafuta) nikachuma matawi kama matano nikapeleka hiyo sample maduka kama kumi tofauti cha kushangaza maduka yote yalinipa majibu tofauti tofauti na dawa tofauti hakuna majibu yaliyofanana kabisa.

Mh Bashe, jaribu kutazama kwa jicho la tatu. Haya maduka yanachangia sana vijana wengi kuona kilimo na ufugaji ni hasara na hakuna faida.

Haya maduka wanatengeneza faida sana , nijukumu la serikali kuwawekea utaratibu juu ya wataalamu wao na ikibidi kuwafanyia snap check mara kwa mara ili kulinda uduma bora.
Yale maduka yanatakiwa yawe na watu wenye degree
 
Mh Bashe , wewe ni miongoni mwa mawaziri mnaochapakazi na zinaonekana, hongera sana.

Ombi langu kwako nalielekeza kwenye maduka ya pembejeo za kilimo na mifugo...kwakweli kumejaa makanjanja wengi sana. Wauzaji wao wengi hawana utaalamu wa kilimo au mifugo.

Na wale walio na wataalamu basi ni level ya diploma au certificate... na kichwani mwao sifuri tupu. Wewe jaribu kufanya utafiti wako binafsi utagundua jinsi wakulima na wafugaji wanavyopata hasara kubwa hasa katika upande wa madawa mpaka upate dawa sahihi ya ugonjwa utajikuta umenunua dawa tofauti zaidi ya tatu au nne ni kama vile wanabahatisha katika kutibu ugonjwa...na hapo unakuta dawa moja si chini ya 13, 000 sasa piga hesabu , mpaka unavuna au unapeleka kuku sokoni umeingia hasara kiasi gani, wao ni chanzo cha mifugo kufa au mazao kuharibika.

Nilijaribu kufanya utafiti mdogo tu...ni lilima matikiti maji , ukaingia ugonjwa (mdudu mafuta) nikachuma matawi kama matano nikapeleka hiyo sample maduka kama kumi tofauti cha kushangaza maduka yote yalinipa majibu tofauti tofauti na dawa tofauti hakuna majibu yaliyofanana kabisa.

Mh Bashe, jaribu kutazama kwa jicho la tatu. Haya maduka yanachangia sana vijana wengi kuona kilimo na ufugaji ni hasara na hakuna faida.

Haya maduka wanatengeneza faida sana , nijukumu la serikali kuwawekea utaratibu juu ya wataalamu wao na ikibidi kuwafanyia snap check mara kwa mara ili kulinda uduma bora.
Kilimo ndo sekta pekee ambayo kila mtu hujifanya mshauri na mtalamu. Kila mtu anaongea lake.Huyu analaumu wauza madawa mwingine
atalaumu maafisa kilimo kwamba hawawatembelei wakulima. Hivi mnajua changamoto za maafisa kilimo/mifugo? Hii ndo sekta ambayo wafanyakazi wake hawana mtetezi. Kwa kifupi wametelekezwa. Mtu anatupwa kijijini bila kupewa nyumba na hakuna anaejali.
Waziri wa kilimo ili aonekane anafanya kazi kwanza atatafta kiki kwa kumdhalilisha Afisa kilimo mbele za watu. Utasikia;Jamani huyu mtu huwa anatembelea mashambaaa? Wananchi....Hakunaaaa!!!

Wakati kiuhalisia mtalamu huyu hana chombo chochote cha usafiri wala vifaa vyovyote vya kufanyia kazi. Jiulize katika kijiji kidogo tu chenye watu elf 4000 je kwa mwaka ataweza kuwatembelea wote na kutoa ushauri tena kwa miguu?
Mbaya inapotokea wakulima wakavuna na kuuza vizuri mazao yao sifa zinaenda kwa wanasiasa ila wakipata mavuno kidogo au hasara hapo jumba bovu ataangushiwa afisa kilimo. Cha ajabu hata kukitokea ukame afisa kilimo hulaumiwa.

Kabla ya kumlaumu mtu ni vema kwanza kujua changamoto zake,kisha ushiriki kuzitatua na kumsaidia then baadae ndo umlaumu.

Sent from my SM-G955U using JamiiForums mobile app
 
Kabla ya kwenda ktk duka la pembejeo; unatakiwa uonane na daktari (afisa ugani/mifugo)

Yeye atakueleza tatizo hilo unatakiwa kutibu kwa dawa yenye kiambata gani (usiulize jina la biashara uliza kiambata) na kwa dose gani

Baada ya hapo utaenda ktk duka la pembejeo/mifugo kununua dawa husika

Kuhusu kila duka kuambiwa dawa tofauti.. inawezekana kwa sababu makampuni yanayozalisha dawa za kilimo ni mengi

Kwa hiyo zinaweza kuwa dawa za makampuni 20 ila kazi yake moja.

Kikubwa serikali ijikite ktk kudhibiti uuzwaji holela wa dawa na wakulima pia wajiepushe na ununuzi holela au kutumia dawa kwa mazoea bila ushauri wa kitaalam
Soma vizuri nimeandika dawa tofauti na ugonjwa tofauti....
 
Hii siyo kweli kwa asilimia kubwa. Kati ya mwaka 2016 to 2021, kulikuwa na mradi mkubwa uliojulikana kama TIJA TANZANIA. Mradi huo uliofadhiliwa na AGRA, ulifanikisha mafunzo kwa wauza pembejeo mamia kwa mamia. Mafunzo hayo yalisimamiwa na kuratibiwa na TPRI.

Kwa hiyo wataalamu wapo wa kutosha. Mafunzo ya mwisho yalifanyika Kigoma 2021 Oct. Wengi wa wahitimu wana maduka ya pembejeo na wanafanya vizuri.

Kwa sasa wengi wameunda magrupu ya whatsapp na facebook kwa ajili ya kushare ujuzi. Lakini nashauri kama kuna swala technical, mwenye shida yeyote aanzie kwa afisa ugani. Kumbuka, huwezi kwenda famasi bila kuandikiwa dawa na daktari.
Nadhani mwanzisha thread hajui utaratibu. Huwezi kwenda duka la dawa na majani ya mimea yaliyoshambuliwa kununua dawa. Sahihi ni kumuita afisa kilimo aangalie shamba lako ndiyo akundikie dawa ya kununua. Utaratibu ni ule ule kama wa binadamu. Huwezi kwenda pharmacy na mtoto mgonjwa ili upate dawa. Najua kwenye nchi kama yetu, yenye upungufu wa wataalam, haya mambo hufanyika lakini siyo utaratibu rasmi.
 
Back
Top Bottom