Pre GE2025 Waziri Bashungwa aiagiza NIDA kutoa vitambulisho vya taifa haraka, kwa wananchi wa mikoa ya pembezoni

Pre GE2025 Waziri Bashungwa aiagiza NIDA kutoa vitambulisho vya taifa haraka, kwa wananchi wa mikoa ya pembezoni

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

The Watchman

JF-Expert Member
Joined
Nov 7, 2023
Posts
896
Reaction score
1,427
Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA) imeagizwa kushirikiana kwa karibu na Idara ya Uhamiaji na Idara ya Wakimbizi ili kubaini waomba vitambulisho vya taifa wanaoikidhi vigezo vya kupatiwa vitambulisho hivyo hususani kwa kwa wananchi wa mikoa ya pembezoni na kuwapatia kwa haraka.

Maagizo hayo yametolewa na Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Innocent Bashungwa kwenye mkutano wa kutathmini utendaji kazi ya mamlaka hiyo sambamba na kupanga mikakati ya uboreshaji wa huduma zinazotolewa na mamlaka hiyo.

Pia soma: Pre GE2025 Special Thread: Mijadala na Matukio ya Uchaguzi Mikoa yote Tanzania Bara na Zanzibar kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025

“Shirikianeni na Idara ya Wakimbizi na Uhamiaj katika kushughulikia kwa haraka na ufaninisi bila kuvunja sheria maombi ya wananchi wa mikoa kama Kigoma na Kagera na wasiokidhi vigezo wataarifiwe kwa wakati na wenye vigezo wapewe kwa haraka” amesisitiza Bashungwa.

Mbali na msisitizo huo pia Bashungwa amemtaka Mtendaji Mkuu wa NIDA kuongeza ubunifu ili wamiliki wa vitambulisho vilivyochapishwa wakabidhiwe mapema.

Kwa mujibu wa NIDA kufikia tarehe 10 Februari 2025 vitambulisho 1,507,796 vimesomeshwa kwenye mfumo na wamiliki wa vitambulisho 918,216 wameshatumiwa ujumbe mfupi ili kuchukua vitambulisho vyao.

Chanzo: Azam TV
 
Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA) imeagizwa kushirikiana kwa karibu na Idara ya Uhamiaji na Idara ya Wakimbizi ili kubaini waomba vitambulisho vya taifa wanaoikidhi vigezo vya kupatiwa vitambulisho hivyo hususani kwa kwa wananchi wa mikoa ya pembezoni na kuwapatia kwa haraka.

Maagizo hayo yametolewa na Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Innocent Bashungwa kwenye mkutano wa kutathmini utendaji kazi ya mamlaka hiyo sambamba na kupanga mikakati ya uboreshaji wa huduma zinazotolewa na mamlaka hiyo.

Pia soma: Pre GE2025 Special Thread: Mijadala na Matukio ya Uchaguzi Mikoa yote Tanzania Bara na Zanzibar kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025

“Shirikianeni na Idara ya Wakimbizi na Uhamiaj katika kushughulikia kwa haraka na ufaninisi bila kuvunja sheria maombi ya wananchi wa mikoa kama Kigoma na Kagera na wasiokidhi vigezo wataarifiwe kwa wakati na wenye vigezo wapewe kwa haraka” amesisitiza Bashungwa.

Mbali na msisitizo huo pia Bashungwa amemtaka Mtendaji Mkuu wa NIDA kuongeza ubunifu ili wamiliki wa vitambulisho vilivyochapishwa wakabidhiwe mapema.

Kwa mujibu wa NIDA kufikia tarehe 10 Februari 2025 vitambulisho 1,507,796 vimesomeshwa kwenye mfumo na wamiliki wa vitambulisho 918,216 wameshatumiwa ujumbe mfupi ili kuchukua vitambulisho vyao.

Chanzo: Azam TV
Mpango wa kuandikisha na wale ambao sio Watanzania ndio umeanza, ili waongeze wapiga kura feki? Pascal Mayalla Kiranga Mshana Jr Erythrocyte
 
Tunaangalia hili tatizo na kutaka kulitatua kwa njia ambazo sio sahihi...

Haya mambo ya vitambulisho yasingewekewa kipaumbele bali namba..., hivyo taasisi yoyote ambayo ina mamlaka ya kumtambua mtu yoyote iweze kuwa na system ya kuhakiki mtu huyo iwapo atawapa namba yake..., Kwahio mtu awe na namba yake kila anapotembea; vitambulisho hata tukiwapa vitapotea (unless nao ni mradi wa kula elfu 30 au zaidi kila kitambulisho kinavyopotea) Au kama vipi kwanini NIDA wasitume softcopy kwa all registered users iwapo wakiwatumia emails au namba zao za whatsapp ?

Sababu ile option ya online copy waliifuta...
 
Mpango wa kuandikisha na wale ambao sio Watanzania ndio umeanza, ili waongeze wapiga kura feki? Pascal Mayalla Kiranga Mshana Jr Erythrocyte
Mkuu mimi nilishapiga kura kwa miguu yangu kuelekea Vingunguti tangu enzi za Benjamin Mkapa.

Na nilishaamua kuondoka kimoja, si kubangaiza halafu kurudi. Tangu enzi hizo.

Niombe kitambulisho cha taifa kwani nimesahau nini Bongo?
 
Back
Top Bottom