Roving Journalist
JF Roving Journalist
- Apr 18, 2017
- 3,984
- 13,760
SERIKALI YAIAGIZA TCRA KUFATILIA WANAOUZA VOCHA TOFAUTI NA BEI ELEKEZI
Naibu Waziri wa Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Mhandisi Maryprisca Mahundi amesema Serikali imetoa maelekezo kwa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) kufuatilia Wafanyabiashara wanaouza vocha za kukwangua kinyume na bei elekezi.
Amesema hayo wakati akijibu swali la Mbunge Tunza Malapo aliyehoji suala hilo, pia JamiiForums.com Wadau kadhaa wakiwemo kutoka Kagera na Songwe (Mji wa Mlowo, Mbozi) walidai kuna changamoto hiyo ambayo imekuwa kero kwa Wanunuaji wakidai Vocha ya Tsh. 500 inauzwa Tsh. 600 au ya Tsh. 1,000 inauzwa Tsh. 1,200.
Waziri wa Ujenzi, Innocent L. Bashungwa (Mb) akiwasili katika Viwanja vya Bunge jijini Dodoma, ambapo atawasilisha Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ujenzi kwa Mwaka wa Fedha 2024/25, Leo tarehe 29 Mei 2024.