Roving Journalist
JF Roving Journalist
- Apr 18, 2017
- 3,984
- 13,760
Bashungwa ametoa agizo hilo Aprili 22, 2024 jijini Dodoma wakati akizindua Baraza la Wafanyakazi la Mfuko wa Barabara (RFB) na Mfumo wa Ufuatiliaji na Tathmini ya Wizara na Taasisi zake ambapo ameagiza hadi kufikia Juni 30, 2024 Mabaraza ya Taasisi za NCC na CRB ziwe zinafanya kazi kwa mujibu wa Sheria.
“NCC pamoja na CRB kupitia kwa Katibu Mkuu jipangeni nataka hadi kufika Juni 30 nipate taarifa ya Taasisi hizi ziwe na Mabaraza ya Wafanyakazi na yanayofanya kazi”, amesisitiza Bashungwa.
Bashungwa amesisitiza kwa wajumbe wa mabaraza kutumia fursa ya uwepo wao katika mabaraza hayo kuhoji na kutoa mapendekezo yatakayokuwa na mchango na kuzaa matunda katika kuiletea nchi yetu maendeleo.
Vilevile, Bashungwa amewakumbusha wajibu wa Baraza la Wafanyakazi ikiwemo Usimamizi wa Rasilimali watu sambamba na kuwajengea weledi, ujuzi na uwezo kwa watumishi pamoja na kusimamia haki na ustawi katika sehemu za kazi.
Kuhusu mfumo wa ufuatiliaji na tathimini, Waziri Bashungwa amewasihi Wakuu wa Taasisi kuboresha majukumu yao ya kiutendaji kupitia mfumo huo ikiwemo kuongeza ufanisi na weledi.
Kwa upande wake, Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Balozi Mhandisi Aisha Amour ameeleeza kuwa Wizara pamoja na Taasisi zake itaanza kutumia rasmi mfumo huu kuanzia tarehe 2 Mei, 2024 ambapo matarijio ya Wizara kupitia mfumo huo utaongeza ufanisi wa Wizara na Taasisi zake na kupunguza matumizi ya fedha za Serikali na kuwezesha kuwa na takwimu sahihi kati ya Wizara na Taasisi zake.
Naye, Kaimu Mtendaji Mkuu wa Bodi ya Mfuko wa Barabara ambaye ni Mwenyekiti wa Baraza la Bodi hiyo Mhandisi Rashid Kalimbaga ameeleza kuwa Baraza la wafanyakazi wa Bodi hiyo linajumuisha wajumbe mbalimbali wakiwemo Wakuu wa Vitengo, Wawakilishi wa Vitengo, Wajumbe wa Halmashauri ya TUGHE tawi la Bodi, Mwenyekiti wa TUGHE kutoka Wizarani, Mjumbe wa TUGHE Taifa na Mjumbe wa TUGHE Mkoa wa Dodoma.