Waziri Biteko anakosa mshauri wa kisiasa. Hana muda na Wizara ya Nishati, muda mwingi anatumia kujitangaza mikoani na ameanza kupoteza mvuto jukwaani

Mimi keshaanza kuniboa kama anavyo niboa waziri mdogo wa nishati na jesinter.
Naibu kawa philosopher, mshauri, mwanasiasa mahiri et al.
Nadhani kuna mtu kamwambia 2030 kina kipara na kina Madelu hawatakua kwenye reli.
 
Ulikuwa unaishi Ulaya? Maigizo yenu ya kula mahindi barabarani mara kigawa pesa na upuuzi kama huo unadhani hizo propaganda zililenga nini?
 
Unata Unataka kusema kwamba wanaiasa ni empty headed? Yaani hata ukiwa na proffesion yako kitendo Cha kuwa mwanasiasa tayaru we unakuwa tabulalasa au. Unataka kusema mfano akina prof mkenda, ndalichako nk kwa vile ni wanasiasa basi uprof wao umefutwa na hivi wamekjwa vilaza lazima kuwe na thinkers waendeshe?
 
Kazi ya Waziri ni ku manage politics.. utendaji haswa unaukuta kwa waandamizi kuanzia kwa katibu mkuu wa wizara..

Yeye kukaa ofisini ama kutokukaa sidhani kama inaongeza chochote zaidi zaidi tu ni anatakiwa kuwa na mawasiliano ya karibu na katibu mkuu wa wizara ili kufanya follow up ya utendaji
 
Dah watu mnauchungu na nchi aisee...



Anyway siasa ndio ilivyo
 
Cheo cha NAIBU WAZIRI mkuu kimekaa kichawachawa tu. Hana majukumu maalumu ya kusimamia ktk hiki cheo chake zaidi ya kubeba maagizo ya hos wake
 
Mwanzo nilidhani Waziri wa Nishati anapewa na kofia ya Unaibu Waziri Mkuu ili aweze kukabiliana na urasimu wa kiwizara ambao unaweza ukamkwamisha mf.akitaka kumhamisha Mtumishi basi akiwasiliana na Waziri wa Utumishi iwe ni kumpa maelekezo sio kushauriana au akihitaji fungu au lolote toka Wizara zingine alipate kwa wakati kwa kutumia kofia ya Unaibu PM

kumbe u Naibu PM kapewa yeye kama Yeye na hata siku akihamia Wizara ya Michezo ataenda nao.
 
Tulio wengi tuliamini hivo. Tukaamini kwa mabadiliko haya pengine Samia kauona uozo pale nishati, na kaamua sasa kuufanyia kazi. Kumbe ni changa la macho. Imefikia wakati naanza kuamini anamtumia Dotto kugain political popularity kanda ya ziwa. Sio kwa manufaa ya taifa.
 
Au basi tuseme ile wizara alipewa mtu kisha akapewa na majukumu mengine ili iwe ni kama wizara isiyo na msimamizi iwe rahisi kwao kupiga.
 
Wewe na Lucas, baada ya hapa sijui mtakwenda wapi?

Mmejitoa ufahamu na kubaki kama misukule tu. Utashi wa ubinaadam wenu mmeupeleka wapi?
 
Moja ushauri mzuri kwa Biteko. Hakika inashangaza sana kuzurula kama yeye ni waziri mkuu. Anasahau tunachangamoto ya nishati.

Nilitarajia nguvu kubwa iwepo huko, hiyo nafasi ya unaibu amepewa ili imuongezee nguvu kiasi kufanya maamuzi katika hiyo sekta na sio kufanya harakati nyingine.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…