Waziri Dkt. Mwigulu atoa ufafanuzi wa baadhi ya tozo alizowasilisha wakati wa Mapendekezo ya Bajeti Kuu na kuleta mkanganyiko kwa wananchi

Nyumba nilopanga tuko wapangaji wawili na kila mmoja ana mita yake sasa tutalipaje hiyo kodi ya majengo.
Hafu mita yenyewe ina jina la mpangaji wa zamani
 
Umeeleza niliyokuwa nawazia 🙂🙂
 
Bado hajaeleweka anazidi kuongeza ukakasi
 
Alibainisha kuwa haimaanishi kwamba shilingi 10 sio mzigo lakini Serikali iliangalia matatizo yaliyopo na kugundua kuwa yanagharimu zaidi, kuliko thamani ya shilingi 10 itakayotozwa kama kodi.
Je wewe mwenyewe Waziri na jamaa zako humo ndani kwanini hamlipi kodi!!!!?
 
Je tunaposema wananchi, Rais, Makamu wa Rais, WM, Mawaziri, wabunge, Makatibu Wakuu, Majaji, siyo wananchi? Je kwanini hawalipi kodi? Je ni foreigners?
 
Hapa amenichanganya labda angeweka jedwali ingesaidia kuelewa vema
 
Alisema kutumia barabara mbovu ni gharama kubwa kuliko ongezeko la kodi hiyo kwenye mafuta, akitolea mfano wa vifo vya wakinamama wajawazito wanopokwenda kujifungua kutokana na ubovu wa barabara hizo.
Shallow thinking
 
Kwa upande wao wahariri walioshiriki semina hiyo wamempongeza Waziri Dkt. Nchemba pamoja na uongozi wa Wizara kwa kutoa ufafanuzi huo na kuomba kuendelea na utaratibu huo ili kuondoa mikanganyiko kwa wananchi.
Baadaa ya kupewa bahasha za kaki
 
Mama anasubiri hadi naye yamkute ndio amtumbue huyu Waziri mwehu jambazi na damu ya shetwan... Kuna watu wanaudhi sana...
 
Nyumba nilopanga tuko wapangaji wawili na kila mmoja ana mita yake sasa tutalipaje hiyo kodi ya majengo.
Hafu mita yenyewe ina jina la mpangaji wa zamani
Ukinunua Umeme tu wanabeba chao
 
Kodi ni kodi, haijawahi kutokea binadamu akapenda sana kulipa kodi. Tujitahidi kulipa kwa maendeleo ya Taifa letu na "Viongozi wetu".
Wapi binadamu wanaopenda kulipa kodi bila shuruti kwa sababu in wajibu wao.Tatizo ni aina,idadi,viwango na njia za ukusanyaji.Vile vile walipa kodi wanapenda sana kuona faida za kodi zao.
Kuna mataifa mengine risiti ya kodi in tiketi ya bahati nasibu inayochezeshwa kila mwezi na zawadi nono hutolewa,karibu uone kama kuna manunuzi bila risiti.Ubunifu=0.
 
Hii ni kodi ya kichwa kwani wabunge wawakili wetu wanasemaje?
 
Mbona hakuna mapendekezo ya Wabunge kutozwa kodi kwenye mapato yao. Yaani wao wanapigia debe uzalendo kwenye pesa za wenzao tu ......... za kwao hawazigusi .....!!
 
Watwambie na wao wanachangia nini kutoka kwenye mishahara yao minono.
 
Kwayo TRA imevunjwa au?
 
Wameanza na Simu, Watafata Benki
Wameacha kukwapua pesa Kutoka kwa akaunti zetu, sasa wanazichukua kwa kisheria zaidi. Kodi ya majengo kupitia Luku ni wizi wa wazi kabisa. Kama nyumba ina mita za Luku Zaidi ya moja ina maana kila mita Itakatwa Kodi ya jengo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…