Suley2019
JF-Expert Member
- Oct 7, 2019
- 2,203
- 5,610
Steve ameteuliwa leo Alhamisi Agosti 12 na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dk. Dorothy Gwajima, jijini Dar es Salaam.
Pamoja na Steve, wengine walioteuliwa ni Mwanaharakati wa Kutetea Haki za Wanawake nchini, Joyce Kiria na Mbunge wa Viti Maalumu, Neema.
Tangu janga la Uviko 19 liibuke tena nchini mwaka huu, Steve ameonyesha kupambana na janga hilo huku akihamasisha Watanzania kupata chanjo ili kujikinga dhidi ya ugonjwa huo hatari duniani.