#COVID19 Waziri Gwajima amteua Steve Nyerere kuwa Balozi wa Uviko-19

Suley2019

JF-Expert Member
Joined
Oct 7, 2019
Posts
2,203
Reaction score
5,610
Msanii maarufu nchini na Mwenyekiti wa Jukwaa la Mama Ongea na Mwanao, Steven Mengele 'Steve Nyerere' ameteuliwa kuwa Balozi wa harakati za kupambana na ugonjwa unaosababishwa na virusi vya corona (Uviko-19).

Steve ameteuliwa leo Alhamisi Agosti 12 na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dk. Dorothy Gwajima, jijini Dar es Salaam.

Pamoja na Steve, wengine walioteuliwa ni Mwanaharakati wa Kutetea Haki za Wanawake nchini, Joyce Kiria na Mbunge wa Viti Maalumu, Neema.

Tangu janga la Uviko 19 liibuke tena nchini mwaka huu, Steve ameonyesha kupambana na janga hilo huku akihamasisha Watanzania kupata chanjo ili kujikinga dhidi ya ugonjwa huo hatari duniani.
 
Tunaelekea kuzuri tunakubali kuwa Covid ipo na inatumalizia Watu wetu.
 
Akili zao zinafanana, I mean mteuzi na mteuliwa wote ni Political Comedians
 
Huyu mpiga debe wa wachina wa bandari ya bagamoyo akae atulie kabisa huyu andunje.
Wapiga kura wa Ndugai wamechanjwa wote? Kwa hiyo hatatembelea jimboni?
 
Hongera kwake Steve. Wacha naye ale keki ya taifa ambayo kila mwananchi anastahili. Wamtafutiepo ukatibu tarafa akazeekee huko. 😁😁😁
 
Hivi Serikali imerudisha makao makuu yake Dar es salaam tena?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…