Waziri Hussein Bashe futa kauli yako kuhusu Roho Mtakatifu

Waziri Hussein Bashe futa kauli yako kuhusu Roho Mtakatifu

Dr Slaa hawezi kutoa tamko kama hilo kwa sababu anaujua Ukristo na nafasi ya Roho Mtakatifu katika wokovu. Kiimani Roho Mtakatifu ni nafsi ya Mungu. Huwezi kumlinganisha Roho Mtakatifu hata na Mtume Mohamad ambaye, kwa imani ya waislam, alikuwa mwanadamu.

Wanasiasa waache kabisa kugusa masuala ya imani, na kisha kuyafanyia kejeli.
Mbona huwa tunasema maendeleo hayaji kwa muujiza wa Mungu na watu hawatoki povu
 
Ufafanuzi: Bashe kasema wanasiasa wanawaeleza vijana wajiajiri, akasema hayo ni mameno ya kisiasa kwani huyo kijana hawezi kuniajiri tu kwa jina la roho mtakatifu yaani akae kila kitu kijilete ili ajiajiri, akakumbusha wanasiasa wanatakiwa kuwaandalia miundombinu bora ya vijana kujiajiri kwa mfano wajengewe malambo yenye maji ili wafanye umwagiliaji na kadhalika, hapo ubaya uko wapi au umekurupuka bila kufahamu theme and content ya Bashe,
Anaelewa ata maana ya roho mtakatifu?Roho mtakatifu anahusika vipi na mambo ya Kilimo.Mbona mweanzake Ndugai aliomba radhi baada ya kusema Yesu alikuwa na Mke!
Bashe atakuwa anatumia kitu cha Arusha,maana ni mfuasi mzuri wa imani ya Rastafari na Hayati Bobu Marley!
 
Miaka ya hivi karibuni kumetoka tabia ya viongozi wa serikali mara kwa mara kutoa kauli za hovyo zisizo na staha zinazoleta ukakasi katika jamii ila kwa sababu hatuna uwajibikaji, tatizo hilo tumeendelea kulilea.

Nilikuwa naangalia clip moja ya hivi karibuni ya Waziri wa Kilimo Hussein Bashe akiongelea masuala ya ajira, akasema hivi "Hauwezi kujiajiri kwa jina la Roho Mtakatifu, you have to prepare".

Bwana Bashe ni mtu ambaye nimekuwa namuona anaongea kwa kufikiri na umakini tofauti na viongozi wengine kwa hiyo nilishtuka nilipoisikia hii kauli yake. Nilisita hata kuleta huu uzi ila nimeona niandike hivi kwa faida yake na viongozi wengine. Kwa mtazamo wangu akirekebisha kauli hii itakuwa mfano mzuri kwa viongozi wengine ambao huwa hata hawarudi kuomba radhi pale wanapotoa kauli za kuudhi.

Nimkumbushe Bwana Bashe kuwa ni muhimu sana akawa sensitive na imani za watu wengine. Katika Ukristo, dhambi ambayo HAISAMEHEKI ni kutoa maneno ya kejeli au kashfa dhidi ya Roho Mtakatifu (Mathayo 12:31-32).

Kipande cha video hiki hapa chini.


View attachment 2492415
Hussein Bashe, your days are numbered
 
Sijui hata hotuba umeielewa? Bashe ana kosa gani hapo?
Angesema "Hauwezi kujiajiri kwa jina la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania", angefukuzwa kazi siku hiyo hiyo, ila kwa hili amepata watetezi.

Tunakumbushana tu.
 
Miaka ya hivi karibuni kumetoka tabia ya viongozi wa serikali mara kwa mara kutoa kauli za hovyo zisizo na staha zinazoleta ukakasi katika jamii ila kwa sababu hatuna uwajibikaji, tatizo hilo tumeendelea kulilea.

Nilikuwa naangalia clip moja ya hivi karibuni ya Waziri wa Kilimo Hussein Bashe akiongelea masuala ya ajira, akasema hivi "Hauwezi kujiajiri kwa jina la Roho Mtakatifu, you have to prepare".

Bwana Bashe ni mtu ambaye nimekuwa namuona anaongea kwa kufikiri na umakini tofauti na viongozi wengine kwa hiyo nilishtuka nilipoisikia hii kauli yake. Nilisita hata kuleta huu uzi ila nimeona niandike hivi kwa faida yake na viongozi wengine. Kwa mtazamo wangu akirekebisha kauli hii itakuwa mfano mzuri kwa viongozi wengine ambao huwa hata hawarudi kuomba radhi pale wanapotoa kauli za kuudhi.

Nimkumbushe Bwana Bashe kuwa ni muhimu sana akawa sensitive na imani za watu wengine. Katika Ukristo, dhambi ambayo HAISAMEHEKI ni kutoa maneno ya kejeli au kashfa dhidi ya Roho Mtakatifu (Mathayo 12:31-32).

Kipande cha video hiki hapa chini.


View attachment 2492415
Mbona inaeleweka tu. Kwa upande wangu alikua anawaonya vijana wasitegemee miujiza au kuajiriwa ila kujiajiri.
 
Siwezi Tetea mtu kakosea aombe msamaha huwezi sema roho mtakatifu ukamtolea sentensi .

Kivingine ni maisha tu tunayopitia ila kwanini hajatolea mfano kwenye dini yake Kwa sababu anajua atakufuru
Juzijuzi hapa Mkuu wa Wilaya Jokate Mwegelo alipojifungua, kuna kejeli nyingine dhidi ya Roho Mtakatifu ilikuwa inahusishwa na mimba yake.

Jamani tunakumbushana tu si kwa ubaya, tusitafute kutrend mitandaoni kwa kuropoka hovyo katika hotuba zetu au post za mitandao. Kila neno unalonena lina gharama katika maisha yako. Chagua maneno sahihi.
 
Miaka ya hivi karibuni kumetoka tabia ya viongozi wa serikali mara kwa mara kutoa kauli za hovyo zisizo na staha zinazoleta ukakasi katika jamii ila kwa sababu hatuna uwajibikaji, tatizo hilo tumeendelea kulilea.

Nilikuwa naangalia clip moja ya hivi karibuni ya Waziri wa Kilimo Hussein Bashe akiongelea masuala ya ajira, akasema hivi "Hauwezi kujiajiri kwa jina la Roho Mtakatifu, you have to prepare".

Bwana Bashe ni mtu ambaye nimekuwa namuona anaongea kwa kufikiri na umakini tofauti na viongozi wengine kwa hiyo nilishtuka nilipoisikia hii kauli yake. Nilisita hata kuleta huu uzi ila nimeona niandike hivi kwa faida yake na viongozi wengine. Kwa mtazamo wangu akirekebisha kauli hii itakuwa mfano mzuri kwa viongozi wengine ambao huwa hata hawarudi kuomba radhi pale wanapotoa kauli za kuudhi.

Nimkumbushe Bwana Bashe kuwa ni muhimu sana akawa sensitive na imani za watu wengine. Katika Ukristo, dhambi ambayo HAISAMEHEKI ni kutoa maneno ya kejeli au kashfa dhidi ya Roho Mtakatifu (Mathayo 12:31-32).

Kipande cha video hiki hapa chini.


View attachment 2492415
uzuri ni kwamba, sisi upande wetu huwa hatumpiganii Mungu, Mungu wetu ana nguvu huwa anajipigania yeye mwenyewe, na ni Mungu mwenye upendo, anampenda kila mtu hata huyo mwenyewe na anatamani siku moja aokoke amuamini yeye badala ya kuamini vitu vingine visivyoeleweka.
 
uzuri ni kwamba, sisi upande wetu huwa hatumpiganii Mungu, Mungu wetu ana nguvu huwa anajipigania yeye mwenyewe, na ni Mungu mwenye upendo, anampenda kila mtu hata huyo mwenyewe na anatamani siku moja aokoke amuamini yeye badala ya kuamini vitu vingine visivyoeleweka.
Mungu wako ni nani ili tumjue kabisa?

Kwahiyo mleta thd amekosea sana kuanzisha thd ya kumpigania huyo Mungu wako?
 
Mungu wako ni nani ili tumjue kabisa?

Kwahiyo mleta thd amekosea sana kuanzisha thd ya kumpigania huyo Mungu wako?
Mungu wangu, Mungu wetu, ni Mungu yule aliye wa kweli, Mungu aliyeumba mbingu na nchi, Mungu wa Ibrahim Isaka na Yakobo, ambaye humpati bila njia ya yule aliyemwaga damu ya kafara, Yesu Kristo. Huyo Roho Mtakatifu mnayemkashifu ndio Mungu huyohuyo kwa namna ya Roho, ambaye akishuka hahitaji mwanadamu apiganiwe. kwake yeye mwanadamu kumpigania ni kosa, ni tusi, ana nguvu nyingi mno za kujipigania.
 
uzuri ni kwamba, sisi upande wetu huwa hatumpiganii Mungu, Mungu wetu ana nguvu huwa anajipigania yeye mwenyewe, na ni Mungu mwenye upendo, anampenda kila mtu hata huyo mwenyewe na anatamani siku moja aokoke amuamini yeye badala ya kuamini vitu vingine visivyoeleweka.
Mungu wenu wa kulialia na kuomba msaada.

Pale juu ya msalaba wahuni walipomtundika alikua analia kama mtoto alonyimwa peremende.
 
Mungu wenu wa kulialia na kuomba msaada.

Pale juu ya msalaba wahuni walipomtundika alikua analia kama mtoto alonyimwa peremende.
pale alikuwa amevaa mwili wa mwanadamu, na Roho ile ya kimungu ilikuwa imemwacha ili apate maumivu sawasawa na yale ambayo wanadamu huwa tunapata, aaibishwe sawaswa na sisi wanadamu tunavyoaibishwa, ili akipata maumivu sisi tusipate maumivu kama tukimwamini. ilikuwa lazima ayapate yale, na hata hayo uliyoyataja sio hayo tu aliyoyapata; angalia hapa chini;

1. walipomkamata walimvuta ndevu hadi damu zikatoka usoni. ili wewe usifanyiwe hayo.
2. walimtemea mate usoni kwa dharau. ili wewe na mimi tusiaibishwe through him.
3. walimvua nguo na kuaibishwa. ili mimi na wewe tusiaibishwe. alibeba aibu yetu.
4. walimpiga mijeledi yenye misumari, damu nyingi ikamtoka. kwa kupigwa kwake sisi tumepona.
5.walimdhihaki na kumwambia ajiokoe, sawasawa na vile wewe unamdhihaki leo. ili mimi na wewe tusidhihakiwe.
6. walimpigilia misumari mikononi, damu nyingi ilimtoka. kwa mikono yetu hiihii, kama ukimwmaini Yesu, utaweka mikono juu ya wagonjwa, nao watapata afya. hakuna mtume mwengine au nabii au masihi ambaye anaweza kuponya hata uywele mmoja tu. wote longolongo tu, ila kwa Jina la Yesu, watu wanapona tukiwawekea mikono yao na majini yanawakimbia.
7. walimpigilia misumari miguuni, damu nyingi ilimtoka.popote tunapokanyaga Mungu yupo nasi na tunao uwezo kumkanyaga nyoka nge na nguvu zote za shetani wala hakuna kitakachotudhuru tukiwa ndani yake.
8. walimvika taji ya miiba kichwani, damu nyingi ikamtoka. Miiba ni ishara ya laana, yeye alilaaniwa badala yetu, alibeba laana ili kuondoa laana kwa wote watakaomwamini. kuishi na laana sasaivi ni uamuzi wako tu ila yupo aliyelipa garama ya laana zako, Yesu Kristo pekee.
9. alikufa, na wakamchoma mkuki ubavuni, damu na maji vikatoka. damu na maji ni udhihirisho wa mtu aliyekufa, hivyo alikufa kweli. Mauti na kuzimu hazina nguvu kwa walio katika Kristo Yesu. ukifa umekufa kwasababu Mungu ametaka, ila mashetani, majini wachawi n.k hawana uwezo kukuua kama upo ndani yake, kwasababu Yesu Kristo alishinda mauti na kuzimu kwa kufufuka kwake.
10. siku ya tatu alifufuka na alipaa mbinguni, yu hai hata leo na ni mwokozi wa ulimwengu.

bahati mbaya, mitume wengine wote na manabii au wale mnaowaamini, hawakufa kwa ajili yenu.

zamani zile, au niseme asili ya Mungu ilivyo, ni kwamba hakuna ondoleo la dhambi/hakuna kusamehewa hadi damu imwagike. zamani ili kusamehewa dhambi ilikuwa lazima utoe kafara la wanyama, uwachinje uwachome ndio wawe wamekufa kwa ajili yako. lakini ikawa watu wasio na wanyama au wale masikini kama wewe wasingeweza kuwa na wanyama kila wakati kuchinja kwa ajili ya dhambi zao, kwasababu ziko nyingi. pia, kafara la wanyama lilikuwa kwa ajili ya kufunika tu dhambi ila sio kuondoa.

Mungu tangu awali akawa amefanya mpango kwamba, iwepo kafara moja tu once and for all, itakayotumiwa na wanadamu sio mmoja au wawili, bali wote dunia nzima, wale watakaoliendea hilo kafara dhambi zao zisamehewe kwasababu kafara hilo lilibeba dhambi zote. garama yake ilikuwa kubwa kulipa madeni yote ya dhambi. ndio akawa reincanated (roho kufanyika mwili), akaingia kwa njia ya Roho Mtakatifu ndani ya tumbo la maria ili azaliwe kama mwanadamu, aishi kama mwanadamu, ayashinde yote ya maisha ya mwanadamu na kuyashinda, na alipofikia miaka 33 pasipo kufanya dhambi yeyote, akiwa mtakatifu, damu yake ikamwagika badala ya dhambi za ulimwengu wote ili yeyote atakayemwendea apate ticket ya kusamehewa dhambi bila kulipa garama nyingine. ndio akateswa na kuumizwa kama hapo juu nilivyokuelezea.

hapana jina lingine liwalo lote lile tulilopewa sisi wanadamu litupasalo kuokolewa kwalo, ila Jina la Yesu Kristo. hilo ndilo jiwe lililokataliwa na ninyi waashi, lakini ndio jiwe kuu la pembeni/jiwe la msingi. bila msingi huo humwoni Mungu. Kwa Jina la Yesu kila goti litapigwa la vitu vilivyoko mbinguni, duniani na chini ya nchi, na kila ulimi utakiri ya kwamba Yesu Kristo ni Bwana.

Yesu Kristo ndiye njia kweli na uzima, mtu haji kwa Baba ila kwa njia yake tu. hakuna mtume wala nabii mwingine aliteswa na kuuawa kwa ajili yako, na hakuna mwingine aokoaye ila yeye tu.

Yesu Kristo anakupenda sana. soma Isaya 53, alijeruhiwa kwa makosa yetu, alichubuliwa kwa maovu yetu, adhabu ya amani yetu ilikuwa juu yake, na kwa kupigwa kwake sisit umepona. Isaya 52 mwishoni utaona jinsi ilivyowashangaza wengi, wafalme na wakuu na watu wa dunia namna alivyokuwa, kwasababu alizaliwa na kuishi kama mtu mwororo/dhaifu, hakuna mtu ambaye unaweza kumdhania kuwa ndiye mwokozi wa ulimwengu. Biblia inasema hata ukimtazama hakuwa mtu anayetamanisha kumtazama kwasababu alikataliwa na watu. alikuwa mtu wa huzuni nyingi ajuaye sikitiko. uzuri ni kwamba, alihuzunika hadi hatua ya mwisho kabisa akawa amebeba huzuni zetu zote ili mimi na wewe tukimwamini tusibebe mzigo wa huzuni, alidharauliwa hadi na kila mtu ili mimi na wewe tusidharaulike, uliuchukua udhaifu wetu wote, na kwakupigwa kwake sisi tumepona.

maneno haya unayoyasoma, kama hautamwamini Yesu Kristo na kuyaponya maisha yako, kuna siku utayakumbuka na itakuwa too late for you. namwomba Mungu akusaidie umrudie yeye na uache njia mbaya, uache kufuata mitume na manabii waongo ambao hawakufa kwa ajili yako.
 
Miaka ya hivi karibuni kumetoka tabia ya viongozi wa serikali mara kwa mara kutoa kauli za ovyo zisizo na staha zinazoleta ukakasi katika jamii ila kwa sababu hatuna uwajibikaji, tatizo hilo tumeendelea kulilea.

Nilikuwa naangalia clip moja ya hivi karibuni ya Waziri wa Kilimo Hussein Bashe akiongelea masuala ya ajira, akasema hivi "Hauwezi kujiajiri kwa jina la Roho Mtakatifu, you have to prepare".

Bwana Bashe ni mtu ambaye nimekuwa namuona anaongea kwa kufikiri na umakini tofauti na viongozi wengine kwa hiyo nilishtuka nilipoisikia hii kauli yake. Nilisita hata kuleta huu uzi ila nimeona niandike hivi kwa faida yake na viongozi wengine. Kwa mtazamo wangu akirekebisha kauli hii itakuwa mfano mzuri kwa viongozi wengine ambao huwa hata hawarudi kuomba radhi pale wanapotoa kauli za kuudhi.

Nimkumbushe Bwana Bashe kuwa ni muhimu sana akawa sensitive na imani za watu wengine. Katika Ukristo, dhambi ambayo HAISAMEHEKI ni kutoa maneno ya kejeli au kashfa dhidi ya Roho Mtakatifu (Mathayo 12:31-32).

Kipande cha video hiki hapa chini.

View attachment 2492415
Kosa ni lako ambaye umekuwa ukimuona kama mtu makini. Huyu ni mtu useless! Useless in really sense! Anawezaje kutumia ukristu kuendesha ajenda yake ya kisiasa? Tena akiwa ni mwislamu!
 
Juzijuzi hapa Mkuu wa Wilaya Jokate Mwegelo alipojifungua, kuna kejeli nyingine dhidi ya Roho Mtakatifu ilikuwa inahusishwa na mimba yake.

Jamani tunakumbushana tu si kwa ubaya, tusitafute kutrend mitandaoni kwa kuropoka hovyo katika hotuba zetu au post za mitandao. Kila neno unalonena lina gharama katika maisha yako. Chagua maneno sahihi.
Bora wew una ofisi ya unasihi
 
Bashe angesema " huwezi kujiajiri Kwa jina La Allah au mtume, inatakiwa kujiandaa" tungemuelewa. Wanacheza na Ukristo sana.


Sasa Mimi namuambia Kwa Uongozi wa Roho Mtakatifu mtu anaweza kujiajiri.
 
Bashe angesema " huwezi kujiajiri Kwa jina La Allah au mtume, inatakiwa kujiandaa" tungemuelewa. Wanacheza na Ukristo sana.


Sasa Mimi namuambia Kwa Uongozi wa Roho Mtakatifu mtu anaweza kujiajiri.
Katika uislamu pia yupo Roho mtakatifu,mbona waislamu,hawajalalamika.,mwalalamika nyinyi na kulia lia.Yeye ametamka Roho mtakatifu,bila kutaja ni wa dini gani.
Ni kama kutaja Nabii na Mtume,bila kutaja wa dini gani.
 
Back
Top Bottom