Waziri January Makamba anamaanisha Magufuli alikuwa akiwakatia umeme watumiaji wakubwa na kuwatisha wakae kimya?

Waziri January Makamba anamaanisha Magufuli alikuwa akiwakatia umeme watumiaji wakubwa na kuwatisha wakae kimya?

Johnny Sack

JF-Expert Member
Joined
Jan 21, 2017
Posts
8,984
Reaction score
19,288
January Makamba akijibu hoja za wabunge kuhusu kukatika kwa umeme, kwanza alimlaumu mbunge Musukuma kwa kumshambulia yeye binafsi na kueleza kazi ya ubunge sio kushambuliana na kama ana matatizo na yeye kuwa waziri au samia kuwa rais apeleke kwingine lakini sio kwenye masuala ya nchi.

Pamoja na maelezo mengine, Makamba alitoa takwimu za TRA zinazoonyesha kipindi cha urais wa Samia suluhu na yeye akiwa waziri, makusanyo yamepanda, na kueleza hii inatokana na kuwa wao hawawakatii wenye viwanda umeme na kuwaambia wanyamaze ndio maana uzalishaji umepanda.

Makamba aliongeza pia matatizo ya kukatika kwa umeme yametokana na legacy, ambapo kipindi kilichopita repair and maintainance ilikuwa haifanywi ipasavyo, na akamaliza kwa kusema kama waziri aliyepita alipewa miaka 4, basi na yeye apewe miaka 4 waone kama hali ya kukatika itakuwepo na kama Magufuli walimpa miaka 6 basi na Samia wampe miaka 6 waone kama haya matatizo yatakuwepo

 
Kwahiyo anataka Mungu amchukue hangaya baada ya miaka 6 ya uongozi wake?

Sisi hatukumpa miaka 6 magu ni M/Mungu ndo alimpa. Na hapo mwaka mmoja aliuiba ye alipewa 5 ya uongozi wa 6 akaiba ndo mana akawahishwa.

Nae huyu ajichunge aongoze miaka aliyopangiwa tu akiiba atakipata.

Na huyo makambako aache kuchafua wenzie nyambaf akijitetea kivyake atakosa nini mpaka autie dosari uongozi uliopita.
 
Hii nchi ni ngumu kusonga, uzuri nje ya haya malalamiko tutamkumbuka Mzee Warioba na timu yake kama watu waliona ubovu wa katiba iliyopo na umuhimu wa katiba mpya.

Naamini uchaguzi wa 2019 na wa 2020 ungelikuwa huru na haki upuuzi mwingi usingelikuwepo sasa ila cha kuchekesha wanaolalamika sasa ni waliochekea wizi wa uchaguzi, na hilo liwe funzo kuanzia sasa. Waacheni wale urefu wa kamba zao, misita tena
 
Back
Top Bottom