Waziri Kalemani atoa siku 14 bei ya gesi ya majumbani iwe imeshuka

Waziri Kalemani atoa siku 14 bei ya gesi ya majumbani iwe imeshuka

johnthebaptist

JF-Expert Member
Joined
May 27, 2014
Posts
97,869
Reaction score
171,716
Waziri wa nishati Dr Kalemani ameitaka Ewura kuhakikisha bei ya gesi ya majumbani inashuka ndani ya siku 14 kuanzia leo.

---
CHATO. Waziri wa Nishati nchini Tanzania Dkt. Medard Kalemani amemuagiza Mkurugenzi wa Mamlaka ya Udhibiti wa Nishati na Maji (EWURA) nchini kuhakikisha anashughulikia suala la kupandishwa kiholela kwa bei ya mitungi ya gesi ya majumbani nchini ndani ya kipindi cha siku 14 kuanzia hii leo Agosti 9, 2021.

Kalemani.jpg

Dkt.Kalemani ametoa agizo hilo hii leo Agosti 9, 2021 Wilayani Chato Mkoani Geita wakati wa uzinduzi wa kongamano la uzinduzi wa bomba la mafuta ghafi litakalojengwa kutoka Uganda mpaka Tanzania litakalogharimu kiasi cha USD 3.2.

Dkt. Kalemani amewataka Wakurugenzi wa EWURA pamoja TPDC kuweka matangazo yao ya kazi kwa lugha ya kiswahili ili kuepukana na changamoto ya wasiojua lugha ya Kiingereza.

Hivi juzi mitungi ya Gesi zote za majumbani iilipanda bei kwa wastani wa zaidi ya asilimia 12.3 kuanzia mitungi midogo ya kati hadi Mikubwa kabisa, kiasi ambacho kilizua taharuki kwa jamii ambayo inatumia gesi hasa mijini.
 
Waziri wa nishati Dr Kakemani ameitaka Ewura kuhakikisha bei ya gesi ya majumbani inashuka ndani ya siku 14 kuanzia leo.

Source: ITV habari
Hakuna kitu kibaya kama kupambana na mfumuko wa bei.

Viongozi nawaomba wapambane na sababu za mfumuko wa bei, kama ni sababu zinazoendana na mahitaji basi hakuna budi bei ipande na kama ni sababu ambazo haziendani na mahitaji ya wakati basi sababu hizo zitatulkwe maisha yaendelee.

Kila mfanya biashara hapa duniani hakuna anayetamani kila siku auze bei pungufu ya mwaka jana bidhaa yakee, kila mfanya biashara anatamani auze kwa bei ya juu zaidi biashara yake.
 
Tuhamie kwenye matumizi ya biogesi. Ndiyo njia rahisi ya kujinasua kutoka kwenye iutegemezi. Zipo portable biogas plants zinazohimilika kwa bei.

Waoneni ICHI ENERGIES na makampuni mengine yanayojishughulisha na biogas pia hata na wataalamu waliopo kwenye vyuo vya elimu ya juu na kati na taasisi za umma kama CAMARTECH na kadhalika kwa maelezo zaidi. Huu uwe mwanzo wa nia ya watanzania kijitegemea si kwenye nishati tu na mambo mengine kama chanjo ya corona na magonjwa mengine.
 
Ametoa sababu zilizofanya ipande? Assume kwenye soko la dunia price iko juu, utalazimishaje kushusha price ya kuuza sababu tu wewe uko na mamlaka.

Nadhani ndo itakuwa mwanzo wa gesi kuadimika. Halafu mpaka zinapanda, huwezi sema serikali haijui hilo. Ni waziri mpumbavu tu asiyejua nini kinaendelea kwenye wizara anayosimamia.
 
Ametoa sababu zilizofanya ipande? Assume kwenye soko la dunia price iko juu, utalazimishaje kushusha price ya kuuza sababu tu wewe uko na mamlaka. Nadhani ndo itakuwa mwanzo wa gesi kuadimika. Halafu mpaka zinapanda, huwezi sema serikali haijui hilo. Ni waziri mpumbavu tu asiyejua nini kinaendelea kwenye wizara anayosimamia.
Kunavitu ukishavipandisha bei basi umeharibu kila kitu
 
Hakuna kitu kibaya kama kupambana na mfumuko wa bei.

Viongozi nawaomba wapambane na sababu za mfumuko wa bei,kama ni sababu zinazoendana na mahitaji basi hakuna budi bei ipande na kama ni sababu ambazo haziendani na mahitaji ya wakati basi sababu hizo zitatulkwe maisha yaendelee.

Kila mfanya biashara hapa duniani hakuna anayetamani kila siku auze bei pungufu ya mwaka jana bidhaa yakee,kila mfanya biashara anatamani auze kwa bei ya juu zaidi biashara yake.
... gesi ya Mtwara imefika hadi Dar es Salaam; unajiuliza tatizo liko wapi kuisafisha na kujaza kwenye mitungi kwa ajili ya matumizi ya majumbani? Tena kwenye hili iwe totally owned na serkali through a state-owned company na bei iwe very affordable! Au ndio hivyo mafisadi wameiweka mfukoni serikali ya CCM?
 
Bei ilipanda mkalalamika na threads mkafungua, waziri ametoa tamko bei ishuke mnalalamika pia...do we even know tunataka nn, au tupo tupo bora liende siku za ku rest in peace zifike?
Tumekua taifa la kulalamika ktk kila kitu, hatuna jema. Na mbaya zaidi tunalalamika bila kutoa suluhisho nn kifanyike.
 
Mradi wa gesi tuliaminishwa tutakuwa matajiri na ntwara itakuwa new York ndogo.
Sasa bwawa LA Nyerere
 
Back
Top Bottom