Fiziolojia
JF-Expert Member
- Oct 19, 2019
- 815
- 1,080
Si mwingine bali ni Waziri wa Kilimo nchini Kenya, Mwangi Kiunjuri, ametumbuliwa na Rais Uhuru Kenyatta siku chache tu baada ya Kenya kuvamiwa na kundi kubwa la nzige ambao wanasemekana wametokea Kaskazini mwa nchi hiyo.
Inasemekana kilichomsababisha haswaa mpaka akatumbuliwa ni ile kauli yake aliyoitoa kwa umma kuwa endapo mtu yoyote ataona mdudu anayefanana nzige katika eneo lake alipo basi asisite kumpiga picha na kuituma kwenye mitandao ya kijamii ili serikali iweze kudhibitisha kama ni nzige au la.
Hali hiyo ilizusha sintofahamu nyingi katika mitandao ya kijamii katika nchi hiyo ambapo watu wengi walishangazwa na kauli hiyo ya Waziri Kiunjuri ambapo wengine walifikia hatua na kuamua kutuma picha za vituko na masihara katika mitandao yao ya kijamii.
Sent using Jamii Forums mobile app
Inasemekana kilichomsababisha haswaa mpaka akatumbuliwa ni ile kauli yake aliyoitoa kwa umma kuwa endapo mtu yoyote ataona mdudu anayefanana nzige katika eneo lake alipo basi asisite kumpiga picha na kuituma kwenye mitandao ya kijamii ili serikali iweze kudhibitisha kama ni nzige au la.
Hali hiyo ilizusha sintofahamu nyingi katika mitandao ya kijamii katika nchi hiyo ambapo watu wengi walishangazwa na kauli hiyo ya Waziri Kiunjuri ambapo wengine walifikia hatua na kuamua kutuma picha za vituko na masihara katika mitandao yao ya kijamii.
Sent using Jamii Forums mobile app