Waziri Kigwangalla aagiza kampuni ya Uwindaji ya OBC ya Loliondo kurudi walikotokea kabla ya Januari 2018

Waziri Kigwangalla aagiza kampuni ya Uwindaji ya OBC ya Loliondo kurudi walikotokea kabla ya Januari 2018

Hao waarabu wa Loliondo walimilikilishwa hilo eneo kisheria na serikali(Hata kama sote tunajua Rushwa ilitembea), tena umiliki wake ni wa miaka 99, Hivyo mkataba wao kisheria utaishia kwenye mwaka 2080 hivi.
Sasa kuwanyang'anya kienyeji enyeji haiwezekani, lazima iwe kisheria.

Kauli ya Kigwangwalla ni kauli ya kupuuzwa tu(japokuwa sote tunajua ni Magufuli mwenyewe huenda labda kamtuma kwenda kusema hayo ili kuleta choko choko).
Ngoja tusubiri, muda utatupa majibu.
Ukiangalia report ni kwamba mpaka sasa wanasini mkataba wa miaka mitano mitano na sio 99 unaweza kusoma pia hapa
fc772c98e381015ef46c69d2d00c8e5d.jpg
e2804edf345aa492c1dd3b047f43d496.jpg
 
Mnyonyaji siku zote humnyonya mnyonge. Lakini wanyonge wakiungana na wakawa wa moja na wenye KAULI moja, Mnyonyaji hubadilika na kuwa mnyonge. UMOJA NI NGUVU. Hongera Mh. KIGWANGALA
 
Hiyo imekaa vizuri sana. Wazawa wameumizwa sana na kudhalilishwa katika ardhi yao. Tumwombe waziri afanikishe kuondoa unyonyaji huo na unyanyasaji uliokuwa wakifanyiwa wazawa kwa robo karne sasa katika eneo hilo.
Kila la kheri mhe. Waziri.
 
Kwanza tujiulize inakuwaje OBC wawe na ofisi mkabala na Ikulu pale Arusha? Ninavyofahamu maeneo karibu na Ikulu uwa ni ya serikali, na nyumba zilizo karibu na Ikulu nategemea watu wa usalama ama maafisa wa serikali wanapaswa kuishi. Sasa hawa OBC wana ofisi yao yaani mita chache tu kutoka kwenye geti la kuingia Ikulu ya Arusha. Nilifika ofisini kwao once; ila sijajua kama bado wapo pale.
 
Waziri wa Maliasili asili na utalii Mh. Kigwangala akiwa katika ziara yake wilayani Ngorongoro pamoja na kuagiza kuvifuta vibali vyote vya uwindaji nchi nzima ikiwamo vya kampuni ya ORTELLO BUSINESS CORPORATION (OBC) ya Loliondo, ameagiza kampuni hiyo ya MWARABU kujiandaa kurudi walikotokea, kwasababu hata kama wakibaki mchakato mpya wa ugawaji vitalu vya uwindaji utakapoanza hautawahusu.

Ikumbukwe kampuni ilipewa eneo hilo miaka ya 1990 kwa mkataba wa miaka 99.


=====

WAZIRI wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangala, amesema Serikali inakusudia kusitisha utoaji wa leseni kwa Kampuni ya uwindaji ya Otterlo Business Corporation (OBC).

OBC iliyoanza uwindaji mwaka 1992 baada ya kupewa leseni na Waziri wa Maliasili na Utalii wa wakati huo, Abubakar Mgumia, imekuwa ikiendesha shughuli hizo kwenye pori tengefu la Loliondo lililopo katika Wilaya ya Ngorongoro mkoani Arusha.

Akizungumza wilayani hapa juzi, wakati wa majumuisho ya ziara yake, Kigwangala, alisema uamuzi huo unatokana na kampuni hiyo kutoka Umoja wa Falme za Kiarabu, kuwa na migogoro isiyoisha na wananchi, hususani jamii ya wafugaji wa Kimaasi.

Waziri Kigwangala alisema OBC haitakuwa sehemu ya kampuni za uwindaji zitakazopewa upya leseni ya uwindaji hapo mwakani, hiyo ni kutokana na kuwapo kwa madai ya uvunjifu wa haki za binadamu, ikiwamo kujihusisha katika migogoro eneo hilo kwa zaidi ya miaka 25.

Alisema kampuni hiyo haitapatiwa tena leseni mpya mwakani, kutokana na kuwa na mkono katika migogoro inayoendelea kwenye eneo hilo la pori tengefu la Loliondo.

“OBC ipo nyuma ya vurugu hizi, siku zao zinahesabika, hawatapewa leseni mpya ya uwindaji Januari mwakani,” alisema Waziri Kigwangala.

Aidha akiwa Loliondo katika ziara yake, Kigwangala aliagiza mifugo yote iliyokuwa ikishilikiwa na bado wamiliki wake hawajafikishwa mahakamani, iachiwe mara moja wakati mazungumzo kwa pande zote yakiwa yanaendelea.

Pia aliagiza wafugaji walioondolewa mifugo yao katika pori hilo, ikiwamo pia maeneo ya mipakani mwa Hifadhi ya Taifa ya Serengeti, waanze kunyweshea mifugo yao katika mito iliyomo ndani ya pori tengefu la Loliondo.

Akiwa mkoani Dodoma hivi karibuni, Kigwangala alisitisha leseni zote za uwindaji katika vitalu na kutaka utaratibu mpya wa kununua vitalu hivyo ufanyike kwa mtindo wa mnada.

Akizungumza na wadau wa utalii na uhifadhi, alisema kwamba hatua hiyo inalenga kulinufaisha zaidi taifa kutokana na rasilimali zilizopo.

Katika mkutano huo, Kigwangala aliwaambia wadau hao kwamba ni Tanzania pekee katika nchi zilizopo Kusini mwa Sahara ambayo imekuwa haikodishi vitalu vyake vya uwindaji kwa kutumia mnada.

Chanzo: Mtanzania
Hongera sana Kigwangwala,I can now see light in the tunnel in this Ministry.It was in a mess.Ila usigeuke tena ukaanza kupokea rushwa.
 
hawa watu wamepata vibari kutoka kwenye serikali kufukuza tu na wana hati miliki sio kitu kidogo , tunarudi kwenye azimio la Arusha inavyoonekana
Ardhi ni mali ya wananchi chini ya udhamini wa Rais na akiona inafaa kwa manufaa mapana ya umma anaweza kuchukua ardhi yeyote nchini kwa madhumuni hayo na kwa kuzingatia sheria zilizopo.
 
Ardhi ni mali ya wananchi chini ya udhamini wa Rais na akiona inafaa kwa manufaa mapana ya umma anaweza kuchukua ardhi yeyote nchini kwa madhumuni hayo na kwa kuzingatia sheria zilizopo.
Ndiyo, lakini LAZIMA atoe compensation! Mgogoro utaweza kutokea endapo land and property valuations za serikali na OBC zitakapotofautiana!
 
Hao jamaa wamepata eneo hilo kihalali.
Na wanalipa fedha nyingi.
Hili ni eneo la mbuga za wanyama sio la kulima.
Sasa hivi kuwapo kwao kumesaidia sana kuhifadhi wanyama na mazingira.
Ndo maana Mkapa aliwapa na aliwatetea sana kuwa lato lao ni muhimu kuliko lingeachwa kwa poachers na wavamizi.
Wenyewe wanakuja mara chache kwa mwaka.
Kampeni hizi zilianza ki udini ..kwanini apewe mwarabu....angekua mzungu isinge kuwa noma.
Wana vijiji wamepata misaada mingi sana kama shule maji na hospital..
Na wanalipa kodi...
Kuwaondoa haileti faida yoyote ile zaidi ya furaha ya nafsi za uchoyo
Kuna watu wanatoa ushuhuda huku kuwa hao waarabu wameua ndugu zao wakati wewe unasema wamesaidia sana wananchi? Hapa nani mkweli?
 
Nilijua tuu kuwa baada ya mambo kuwa poa ,na mzee prof. kutumbuliwa sasa ni zamu ya maliasili na utalii. Kanaanza kamoto kidogo kama utani lakini baadaye utakuja kulipuka kila mtu atashangaa NAIONA TANZANIA MPYA YA NDOTO YANGU HIYOOO!! BIG UP PRESIDENT lazima rasilimali za taifa zisaidie taifa na sio wanyonyaji wachache
Hao wanyonyaji ndio wanamiliki hicho chama anachotokea
 
Hao waarabu wa Loliondo walimilikilishwa hilo eneo kisheria na serikali(Hata kama sote tunajua Rushwa ilitembea), tena umiliki wake ni wa miaka 99, Hivyo mkataba wao kisheria utaishia kwenye mwaka 2080 hivi.
Sasa kuwanyang'anya kienyeji enyeji haiwezekani, lazima iwe kisheria.

Kauli ya Kigwangwalla ni kauli ya kupuuzwa tu(japokuwa sote tunajua ni Magufuli mwenyewe huenda labda kamtuma kwenda kusema hayo ili kuleta choko choko).
Ngoja tusubiri, muda utatupa majibu.
Unakumbuka kete ya ewura kwa iptl? Pamoja na mikataba yao walinyimwa leseni ya ewula ya kuzalisha umeme wakaufyata! Subiri dawa ya waarabu ipo jikoni wananyimwa leseni ya kuwainda wanabakiza leseni ya kupiga selfie na fisi na nguruwe poli! [HASHTAG]#kigwangalathemessiah[/HASHTAG]
 
Mheshimiwa @Kigwangala.......usimsahau na huyu Green Miles......nadhani ujangili wake una ushahidi wa video kabisa........
 
Kuna watu wanatoa ushuhuda huku kuwa hao waarabu wameua ndugu zao wakati wewe unasema wamesaidia sana wananchi? Hapa nani mkweli?
Wacha uongo wameua wapi...waraabu wanakuja mwaka mara 4 to 10...na hawa ni very high profile sio kila mwarabu.
Wacheni chuki.

Sent from my SM-J500H using JamiiForums mobile app
 
Kama ukiingia hilo eneo mtandao unaandika karibu Uarabuni, na wameweka bendera yao wakati sio ubalozi. Kuna ushindi hapo kwa kufuata sheria za ardhi za nchi.

Hakuna fidia maana wenyewe ndio wame breach contract kwa kuweka kipande cha ardhi ndani ya nchi huru.
 
Kwa issue ya Loliondo acha iwe mbaya tu, waondokewe huyu mwekezaji siyo mwekezaji tu, watanzania wengi sana wameuwawa kwenye hicho kitalu chake.
 
Kwa issue ya Loliondo acha iwe mbaya tu, waondokewe huyu mwekezaji siyo mwekezaji tu, watanzania wengi sana wameuwawa kwenye hicho kitalu chake.
Za kuambiwa changanya na zako!
 
Back
Top Bottom