Waziri Lukuvi aagiza Hati za Ardhi kutolewa ndani ya wiki moja

Waziri Lukuvi aagiza Hati za Ardhi kutolewa ndani ya wiki moja

mkiluvya

JF-Expert Member
Joined
May 23, 2019
Posts
809
Reaction score
729
1592932178687.png

Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeeo ya Makazi William Lukuvi ameagiza kutolewa Hati za umiliki wa ardhi ndani ya wiki pamoja pale mwananchi atakapokuwa amekamilisha taratibu zote za umilikishwaji ardhi.

Aidha, ameagiza wananchi kupatiwa hati zao za ardhi katika halmashauri waliolipia gharama za kupatiwa hati ili kuondoa usumbufu pamoja na gharama kwa mwananchi kufuatilia Hati kwenye Ofisi za Ardhi za mikoa.

Lukuvi alitoa agizo hilo jana wakati akizindua ofisi ya ardhi mkoa wa Tanga katika hafla fupi iliyofanyika jijini Tanga. Uzinduzi wa Ofisi hizo ulihudhuriwa na Waziri wa Afya Ummy Mwalimu, Katibu Mkuu Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mary Makondo, Mkuu wa mkoa wa Tanga Martine Shighela, Kamishna wa Ardhi nchini Nathaniel Nghode, Katibu Tawala mkoa wa Tanga Judica Omari, Wakuu wa wilaya za mkoa wa Tanga pamoja na viongozi wa taasisi mbalimbali za mkoa wa Tanga.

Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi alisema, wizara yake imekamilisha ndoto za Rais John Pombe Magufuli za kuondoa usumbufu kwa wananchi kupata hati za ardhi pamoja kufuata huduma za ardhi umbali mrefu na kutolea mfano kuwa, mwananchi wa mkoa wa Tanga alilazimika kuifuata huduma ya ardhi mkoani Kilimanajaro.

‘’Umekamilisha taratibu zote za kupatiwa Hati hapa Tanga, unaambiwa ukachukue Moshi ilipo ofisi ya Kanda, Rais ameliona hilo maana gharama za ufuatiliaji ni kubwa kuliko hata ghrama ya kulipia hati yenyewe’’ alisema Lukuvi.

Aliwataka Wakurugenzi wa Halmashauri nchini kuhakikisha pale hati za maeneo yao zinapokamilika wamfuate Msajili Msaidizi wa Hati katika ofisi ya ardhi ya mkoa kwa lengo la Msajili huyo wa Hati kwenda kuzikabidhi hati hizo kwa wahusika kwenye halmashauri badala ya wananchi kuzifuta mkoani. Kwa mujibu wa Lukuvi, kumbukumbu zote za ardhi katika mkoa zilizokuwa ofisi za Kanda nazo zimepelekwa mikoa husika na kutolea mfano kumbukumbu za mkoa wa Tanga ambazo awali zilikuwa zikihifadhiwa Dar es salaam na baadaye kuhamishiwa Moshi, Kilimanjaro sasa zimetunzwa Ofisi ya ardhi mkoa wa Tanga.
 
Lengo ni zuri, ila utekelezaji wake maana idara ya ardhi wanasema waz wazi kuwa amekuja ataondoka na kutuacha tunakula!
Angeliweka modalities kma umemaliza kulipia, kama hukupata hati uende wapi kuripoti! Amecha hiv hivi hamna kitu hapo
 
Lengo ni zuri, ila utekelezaji wake maana idara ya ardhi wanasema waz wazi kuwa amekuja ataondoka na kutuacha tunakula!
Angeliweka modalities kma umemaliza kulipia, kama hukupata hati uende wapi kuripoti! Amecha hiv hivi hamna kitu hapo
Hili jambo nimelisema sana humu ila nashukuru walau wameanza kusikia kilio hiki.

Jukumu la kuaandaa na kusajili hati za umiliki wa ardhi lifanywe na mamlaka au wakala maalumu wa serikli badala ya Halmashauri na Msajili wa hati

Jukumu la kuaandaa na kusajili hati za umiliki wa ardhi lifanywe na mamlaka au wakala maalumu wa serikli badala ya Halmashauri na Msajili wa hati
 
Yani namumtakia Waziri Lukuvi akashinde Ubunge kisha Rais amteue tena kuwa Waziri wa Ardhi na Maendeleo ya Makazi nchini.

Walau amethubutu kuleta mabadiliko yenye kupunguza kero na migogoro ya ardhi nchini .

Kiukweli kazi bado ipo lakini walau ameleta awareness kwa kiasi fulani.

Matharani swala la kuanzishwa zoezi la upimaji na urasimishwaji wa maeneo ya watu kwa kuchangia kiasi cha fedha cha wastani kwa kweli limekuwa jambo zuri sana tana sana.

Udumu ndugu Lukuvi endelea kututumikia wananchi.

Mwenyezi Mungu azidi kukustiri na kukuepusha na Mabaya .

Lakini jitahidi kumcha Mungu na kuendelea kuamua kwa haki.
 
Tunaomba mheshimiwa Rais tunakuomba pamoja na mheshimiwa Lukuvi mpunguze malipo ya kodi ya Ardhi kama Mheshimiwa Rais alivyofanya kwenye kodi za majengo kuwa flat rate ya shilingi 10,000 kwa nyumba za kawaida na 50,000 kwa ghorofa.

Tunakuomba mheshimiwa Rais utuwekee flat rate ya Shilingi 10,000 kwa kila kiwanja.

Hiyo itahamasisha ulipaji kodi hiyo kwa wakati.

Kwa kuzingatia kuwa kumekuwa na uhamasishaji wa upimaji na urasimishaji wa maeneo hali hii imepelekea mtu mmoja kuwa na viwanja viwili vitatu mfano mtu kama alikuwa na eneo la nusu eka au eka moja n.k amejikuta na viwanja viwili vitatu hadi viwanja 5 n.k

Sasa changamoto inakuja kwenye kulipa kodi ya umiliki wa ardhi kwa viwanja hivyo.

Hivyo tafadhali Mheshimiwa Rais nakuomba unisaidie kushusha viwango hivyo na kuwa flat rates za shilingi 10,000 tu kwa kila kiwanja.

Mheshimiwa Lukuvi tunaomba mshauri Rais kwenye hili tafadhali.

Tunasubiri utekelezaji wa hilo.
 
Nichukue nafasi hii kuwapongeza kwa kupeleka mashauri ya ardhi kwenda mahakamani badala ya baraza la ardhi.

Sote tunajua urasimu mkubwa ulokuwa unafanyika kwenye mabaraza ya ardhi.

This is the best archivement .

Hii itapunguza na hata kuzuia migogoro ya ardhi .


Binafsi nionavyo Haya ndipo nashawishika kufikiria kura yangu ya ndiyo kuitoa kwa wenye rangi za kajani.

Tutakuwa pamoja.
 
Maana mtu alikuwa anaamua tu kuvamia eneo la mtu na kujifanya lake kibabe.

Sasa hivi ni mahakamani na kule wanafanya kazi kwa weledi.

Mwenyehaki yake atapewa.
 
Actually nikumegee siri kidogo kuna watu wanafikiria kutelekeza hati zao wasijekuzichukua sababu ya kuhofia ulipaji wa kodi kubwa ya ardhi .

Maana chukulia mtu aliyekuwa na shamba la eka 2 mfano hata eka moja akitoa plots kadhaa na pengine watoto wake bado wadogo Je itakuwaje mtu mmoja kumudu kulipia viwanja 5-10 kwa kila mwaka?

Yani labda mzipeleke serikali ya mtaa wawatafute wahusika.
 
Wengine hawajalipia upimaji sababu hali ni ngumu,

Pamoja na hali ngumu lakini pia wanasema wanahofia wakishapata hati bado gharama za kulipia hati kila Mwaka wanaona hawatamudu.

Kwa hiyo nawashauri muwahamasishe kwa kushusha kiwango cha kodi ya ardhi ya kila Mwaka kuwa walau 10,000/-

Maaana hapo kama pamejengwa nyumba itatakiwa kulipia kodi ya jengo ya 10,000/-

Na bado na mengineyo, imagine!
 
Back
Top Bottom