Tetesi: Waziri Maghembe kutumbuliwa

Tetesi: Waziri Maghembe kutumbuliwa

Katika watu waliokuwa hawaamini ushirikina basi ni mimi. Kwa jinsi huyo Maghembe alivyoanza kuitwa mzigo na jinsi akiongea hana mvuto, lakini bado ni mbunge na uwaziri juu, hapo nimechoka kabisa. Cha ajabu huyo Waziri mkuu anashughulikia hilo suala mwenyewe wakati dalilizote za uongo ziko wazi. Saa hii huyo mzee anapiga ramli tu ili asifukuzwe uwaziri.
 
Nauliza hiviiiiiiiiii eti ile mahakama ya mafisadi ipo au haipo ? Kama ipo kwanini hawa wasipelekwe huko ?
 
ningekua ni mimi, waziri mkuu anakuja kwa wizara yangu, anagundua chezo, siwezi kubaki, ona sas anakua bubu
 
Alinifukuza chuo huyu akafanya nihamie bara lingine kabisa . Naamini zamu yake nae imefika kuishi kama shetani.

[HASHTAG]#BringBackBenAlive[/HASHTAG].

Mkuu bily alikuchezesha sebene nini?

Sijaelewa hata kidogo hapo...
 
Mkuu sio kweli kwamba waziri mkuu hawezi kusema uongo.
Hadi ataje kabisa na kiasi cha pesa ambacho John aliuzwa unadhani aliropoka eeh? Kama ni kuropoka kwanini hajakisia bei lakini akataja bei halisi? We subiri uone huyo waziri na majangili wenzake jinsi watakavyopukutishwa kutoka kwenye nafasi zao.

[HASHTAG]#bringbackourrhinoalive[/HASHTAG]
 
Hadi ataje kabisa na kiasi cha pesa ambacho John aliyzwa unadhani aliropoka eeh? Kama ni kuropoka kwanini hajakisia bei lakini akataja bei halisi? We subiri uone huyo waziri na majangili wenzake jinsi watakavyopukutishwa kutoka kwenye nafasi zao.

#Bringbackourrhinoalive#
Wewe umejuaje kama hicho kiasi kilichotajwa ni halisi?
 
Kuna kila dalili kwamba Waziri wa Maliasili na Utalii, Profesa Jumanne Maghembe amekalia kuti kavu, tena kavu kwelikweli.

Sakata la kuuzwa kwa faru John na kisha yeye kubariki uuzwaji huo ni udhaifu mkubwa sana na kigezo tosha cha kumfanya aondolewe kwenye nafasi yake ya sasa. Kwa mujibu wa Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa Majaliwa, inasemekana faru huyo aliuzwa kwa thamani ya Tsh milion 200, ambapo wauzaji walitanguliziwa malipo ya Tsh milioni 100. Waziri mkuu hawezi kusema uongo. Ni dhahiri anazo taarifa za uhakika za kiintelejensia kwamba faru ameuzwa kwa bei hiyo ya kutupwa. Ndio maana wahifadhi wanashindwa kuonyesha kaburi lake lilipo kama kweli mnyama huyo wa porini alikufa.

Sintofahamu hii inakolezwa zaidi na Maghembe mwenyewe aliyediriki kumdanganya Waziri Mkuu, kwa kushirikiana na wezi wenzake, kwamba faru yule 'amekufa' huku akijua kwamba anasema uongo. Kwa sababu hizi, pamoja na sababu nyingine ambazo bado hazijawekwa wazi ili kumtumzia heshima profesa huyu, kuna kila dalili kwamba huenda Rais, Dr Joseph Pombe akatengua uteuzi wake kabla hajamaliza faru wetu.

Ikiwa waziri mwenye dhamana ya kulinda rasilimali zetu, ama kwa kujua au kwa makusudi, ameamua kushirikiana na majangili kufilisi rasilimali zetu kuna haja gani ya kuendelea kukalia kiti cha uwaziri? Kwa dhati kabisa bila unafiki wowote, mimi namuunga Rais Pombe katika utumbuaji huu. Ifike wakati kila mtu aheshimu rasilimali za taifa kwa manufaa ya watanzania wa sasa na vizazi vijavyo.

Mungu mbariki Rais wetu, Mungu wabariki watanzania, Mungu bariki rasilimali zetu za Taifa. Amen.
Huyo faru alipotea lini?
 
Waziri Mkuu hawezi sema uongo?? Hebu acha kutulaghai, PM ni binadamu kama binadamu wengine. Anaweza potoshwa na wasaidizi wake pia. Tuiache tume ilioteuliwa na PM ifanye kazi
 
Ishu ya kusemwa ukweli au uongo siyo ishu sana ishu kifo cha faru ndo utata,kuna dalili zote kuwa alipigwa dili sasa kuthibitisha hilo ndo ngumu kidogo ila pia pm anataka kumshika mchawi wake kitu ambacho kina kuwa ngumu now kwani kaburi la faru halipo labda atumie mbinu nyingine ila pia kama aliuzwa na pm anajua aliko akamchukue ili amalizane nao vizuri sahani moja.
 
Acheni kuhukumu bila ya kujua undani wa suala lenyewe. Hivi leo kipindi cha Star Television cha Tuongee Asubuhi kilikuwa na Mada isomekayo Sintofahamu ya sakata la Faru John. Katika kipindi hicho waongoza mada wa Mwanza na Dar es Salaam pamoja na wachambuzi wao walitumia muda mrefu wakimtaka Waziri Maghembe ajiuzulu; Kwa maoni yangu naona hii sio kumtendea haki Waziri huyo bila ya kujua undani wa suala lenyewe; Je, kama Waziri Maghembe ndio alimpa taarifa mkuu wake wa kazi yaani Waziri Mkuu alishughulikie kutokana na wahusika/Mhusika mkuu wa ufisadi wa Faru huyo ni wale wasiogusika (Untouchable?) hivyo akaona ni vyema suala hilo lianzie kwa PM? Si tulishasikia lile sakata la pembe za ndovu zilizotolewa taarifa na mwandishi nguli kutoka Uingereza kwamba majangili wakubwa wa pembe za ndovu ni watu maarufu nchini. Sasa kwa nini tunamhukumu Maghembe?
 
Ni ile ile ohhhhh, ni ile ile., akitumbuliwa atapangiwa kazi nyingine.
 
Magufuli aanze kuwaamini na wapinzani awateuwe nao.. Maana Ccm ni ukoo wa panya..
Magufuli ni mtu wa visasi...kamwe hawezi kuwateua wapinzani zaidi ya alivyompoza Mrema kwa jitihada zake za kubomoa upinzani.
 
Back
Top Bottom