Tetesi: Waziri Maghembe kutumbuliwa

Tetesi: Waziri Maghembe kutumbuliwa

Ogopa sana waziri mwenye dhamana anafoji report, anadanganya idadi ya watalii imeongozeka kumbe ni uongo mtupu ukilinganisha na mapato ya TRA kutoka TANAPA, anatafuta sifa za kisiasa.

Mzee kama huyu anapaswa kumpumzika ana akili za kufoji repoti kama Dr. Mpango.
 
Si wamesema "mahakama ya mafisadi imekosa wateja" maybe saizi itapata.
 
Wewe umejuaje kama hicho kiasi kilichotajwa ni halisi?
Kama wewe unajua bei mliyouza kwanini usiitaje? Waziri Mkuu hawezi kuropoka ovyo. Wewe subiri muone moto utakaowawakia punde.

[HASHTAG]#bringbackourrhinoalive[/HASHTAG]
 
Sakata lote hili anayelengwa ni Maghembe tu!
Wanazunguka tu bure na kupoteza muda kama hawamtaki wamtumbue tu
 
Acheni kuhukumu bila ya kujua undani wa suala lenyewe. Hivi leo kipindi cha Star Television cha Tuongee Asubuhi kilikuwa na Mada isomekayo Sintofahamu ya sakata la Faru John. Katika kipindi hicho waongoza mada wa Mwanza na Dar es Salaam pamoja na wachambuzi wao walitumia muda mrefu wakimtaka Waziri Maghembe ajiuzulu; Kwa maoni yangu naona hii sio kumtendea haki Waziri huyo bila ya kujua undani wa suala lenyewe; Je, kama Waziri Maghembe ndio alimpa taarifa mkuu wake wa kazi yaani Waziri Mkuu alishughulikie kutokana na wahusika/Mhusika mkuu wa ufisadi wa Faru huyo ni wale wasiogusika (Untouchable?) hivyo akaona ni vyema suala hilo lianzie kwa PM? Si tulishasikia lile sakata la pembe za ndovu zilizotolewa taarifa na mwandishi nguli kutoka Uingereza kwamba majangili wakubwa wa pembe za ndovu ni watu maarufu nchini. Sasa kwa nini tunamhukumu Maghembe?
Kama waziri maghembe anashindwa kusimamia rasilimali zetu, na wakati huohuo akishirikiana na majangili, hadi aje waziri mkuu kuna haja gani yeye kuwepo kwenye nafasi yake?

[HASHTAG]#bringbackourrhinoalive[/HASHTAG]
 
Ndio maana mnyama yeyote akipata matatizo lazima Magembe kama waziri apewe taarifa na yeye ndio wa mwisho kuizinisha na kutoa tamko hiyo ndio kazi yake.
Huna Elimu ya juu

Go back to school Dude.


swissme
Kuna watu wapowapo tu kama Mazombie...

Hajui hata wajibu na majukumu ya waziri wa wizara husika.
 
Kuna kila dalili kwamba Waziri wa Maliasili na Utalii, Profesa Jumanne Maghembe amekalia kuti kavu, tena kavu kwelikweli.

Sakata la kuuzwa kwa faru John na kisha yeye kubariki uuzwaji huo ni udhaifu mkubwa sana na kigezo tosha cha kumfanya aondolewe kwenye nafasi yake ya sasa. Kwa mujibu wa Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa Majaliwa, inasemekana faru huyo aliuzwa kwa thamani ya Tsh milion 200, ambapo wauzaji walitanguliziwa malipo ya Tsh milioni 100. Waziri mkuu hawezi kusema uongo. Ni dhahiri anazo taarifa za uhakika za kiintelejensia kwamba faru ameuzwa kwa bei hiyo ya kutupwa. Ndio maana wahifadhi wanashindwa kuonyesha kaburi lake lilipo kama kweli mnyama huyo wa porini alikufa.

Sintofahamu hii inakolezwa zaidi na Maghembe mwenyewe aliyediriki kumdanganya Waziri Mkuu, kwa kushirikiana na wezi wenzake, kwamba faru yule 'amekufa' huku akijua kwamba anasema uongo. Kwa sababu hizi, pamoja na sababu nyingine ambazo bado hazijawekwa wazi ili kumtumzia heshima profesa huyu, kuna kila dalili kwamba huenda Rais, Dr Joseph Pombe akatengua uteuzi wake kabla hajamaliza faru wetu.

Ikiwa waziri mwenye dhamana ya kulinda rasilimali zetu, ama kwa kujua au kwa makusudi, ameamua kushirikiana na majangili kufilisi rasilimali zetu kuna haja gani ya kuendelea kukalia kiti cha uwaziri? Kwa dhati kabisa bila unafiki wowote, mimi namuunga Rais Pombe katika utumbuaji huu. Ifike wakati kila mtu aheshimu rasilimali za taifa kwa manufaa ya watanzania wa sasa na vizazi vijavyo.

Mungu mbariki Rais wetu, Mungu wabariki watanzania, Mungu bariki rasilimali zetu za Taifa. Amen.
Usihukumu cinema ifike mwisho. Ila tu lazima tuseme ukweli, watu kama Prof. Maghembe wanapaswa kukaa nyumbani na kubaki kuwa washauri wa vijana. Mzee kama huyu ameshalichangia taifa vya kutosha, kama haikutosha haiwezi kutosha tena saa hii. Kasi hii ya sasa awaachie akina Makonda tu waende nayo maana akina Prof. Maghembe ni sehemu ya hali hii tuliyonayo kama taifa ambayo Rais Magufuli inamhangaisha hivi sasa.
 
Mic u Mr President Mrisho Jakaya Kikwete..Ridhiwani 2020 chukua fomu, si kwa uongozi huu Wa awam ya 5. Faru John unawanyima watu usingizi na amani ya maisha kweli haki hii Mr faru john...heee r.I.p..
 
Wazir mkuu alisema kuwa serikali imetoa trilion 1 kununua madawa. Magufuli akasema serikali imetoa billion 200 kunuNua dawa. Nani apo ni muongo?
Inategemea Rais alizungumzia dawa za kipindi gani na waziri mkuu alizungumzia dawa za kipindi gani
 
Back
Top Bottom