Waziri Makamba aeleza alivyovumilia mashambulizi, ajifananisha na Kocha Mourinho sakata la kukatika kwa umeme

Waziri Makamba aeleza alivyovumilia mashambulizi, ajifananisha na Kocha Mourinho sakata la kukatika kwa umeme

saidoo25

JF-Expert Member
Joined
Jul 4, 2022
Posts
624
Reaction score
1,456
Waziri wa Nishati, Januari Makamba amesema kwenye siasa kuna maneno mengi na unahitaji ngozi ngumu na kifua kwani kila umeme unapokatika jina linaloibwa ni lake.

“Kwenye siasa kuna maneno mengi na unahitaji ngozi ngumu na kifua, kila umeme unapokatika jina lililoimbwa ni la kwangu wala sio TANESCO au wafanyakazi wake, ilifika hatua ikasemwa Rais (Samia Suluhu Hassan) tazama huyu mtu (January)” alisema Januari

“Kuna kocha anaitwa Mourinho napenda staili yake sana, yeye akiwa katika mechi ya ugenini ambayo unakuta uwanja umejaa anakuwa wa kwanza kuingia ndani ya uwanja, anazomewa na mashabiki wa timu pinzani kisha anawaambia wachezaji wake watoke vyumba vya kubadilisha nguo na waingie uwanjani. Ndivyo ilivyokuwa kwangu nilikubali kupokea mashambulizi” alisema Makamba

Chanzo Gazeti la Mwananchi Julai 15, 2022
 
Kalemani alipeleka umeme kwenye vijiji elfu 10 vikabaki vijiji elfu 2 tu.

Kwa sarakasi hizi za Makamba vijiji elfu 2 havitaisha kupelekewa umeme
 
Sjoni sababu ya watu kumshambulia makamba. Sioni
Kama Kuna tatizo watu wanaweza kutoa maoni bila kumshambulia
 
Kwa hili yuko sawa,Yeye ndio Waziri anaetukanwa Sana na Sukuma gang na Chadomo ..

Sukuma gang wanamuona ni threat Kwenye mambo ya Urais ikizingatiwa aliingia Tano Bora na ana ushawishi kama Lowasa ila Chadomo wanakumbukia maumivu waliyoyapata aliposimamia kile kituo Cha kujumuisha matokeo.
 
Kwa hili yuko sawa,Yeye ndio Waziri anaetukanwa Sana na Sukuma gang na Chadomo ..

Sukuma gang wanamuona ni threat Kwenye mambo ya Urais ikizingatiwa aliingia Tano Bora na ana ushawishi kama Lowasa ila Chadomo wanakumbukia maumivu waliyoyapata aliposimamia kile kituo Cha kujumuisha matokeo.
Nimejaribu kukuelewa nimeshindwa
 
Back
Top Bottom