Waziri Makamba waelekeze Tanesco waache kusambaza umeme kwa nyaya nyembamba za 25mm badala ya 100mm wanaua vifaa vyetu

Acha ubishi wako nimeandika nikiwa ni mtu ninaona kinachofanyika mara nyingi, huko walikoweka 25mm kwenye usambazaji wako na shida
 
Tatizo la Tanzania ni viongoz
Kila mtu mpiga dili
 
Hakika...

Ngoja waje kukutatulia tatizo kwa kukuomba number ya simu na location...
 
eti maeneo mengi
mengi kuanzia mangapi ?
ume-generalize sana, thread inaendeshwa kwa hisia binafsi
Lengo langu sio mipasho mkuu,lengo langu ni kufikisha ujumbe kwa wahusika,sijakurupuka nimefuatilia,najua wanajua ila wanafikiri wateja wote maamuma,uzuri kama ni mzoefu hizi waya wala huhitaji vipimo,hata zikiwa juu ya nguzo kwa macho unazijua.

Nilishawahi pata hili tatizo kwenye three phase nilichoma sana mota nikaingia hasara za mamilioni mpaka walipobadilisha size ya waya tatizo likaisha,baada ya hapo ndipo nilipokua makini kufuatilia kwa karibu Tanesco hawazingatii hili maeneo mengi.

Rafiki yangu yupo Chanika juzi amenipigia kwamba machine zake zinashindwa kufanya kazi,kwakua yeye si mzoefu nikamuelekeza namna yakutizama voltage kwenye remote kwa phase zote tatu,phase iliokua na voltage ya juu ni 160 voltage wakati ili machine zifanye kazi vizuri inatakiwa iwe walau 200 voltage,alipoenda tanesco baada ya kufika sight wakamwambia tatizo ni size ya waya kwenye distribution,wanamwambia ili wamfanyie fasta wanamtaka atoe laki tisa shit!Inakera!

Kama wewe ni ukoo wa makamba samahani mkuu,lengo langu sio kumwaga ugali,huenda Makamba hajui tukimfahamisha anaweza tatua tatizo.
 
Waziri wa mchongo hana sauti yoyote Tanesco kazi anayoiweza ni kujipimia kwa kamba yake tu
Tena huyu kakata kamba kabisa, eti anataka kukodi crane la tani 26 toka nje ya nchi tena permanent linakuwa, halafu la kukodi eti
 
Ni 100 mm2 (squared millimeters) kwa maana ni cross-sectional area ya wire na si diameter ya wire.
Kwahiyo ni vyema akatofatisha kati ya kipimo cha (urefu) na (eneo), maana hiyo Squared (2) hajaweka. Ahsante kwa ufafanuzi.
 
sasa mkuu ndiyo wapitishe 100mm kweli ?
napinga uliposema 'maeneo mengi sana' yanasambazwa na 25mm kitu ambacho siyo kweli
huo ni upotoshaji
 
Wanakula kutokana na urefu wa kamba zao.
Your browser is not able to display this video.
 
Unaijua 100mm vizuri kuwa serious kaka, na Mara nyingi TANESCO wanatumia 95mm na sio 100mm
 
Kwa Kuwa TANESCO hadi saizi hawaja comment basi kuna ukweli mkubwa hapa na wameamua kukaa kimya. Wizara ipo chini ya mtu anayekusanya hela kwa ajiri ya uchaguzi
Mbona hizo Waya zimeanza kutumika kipindi cha Kayafa Mwendakuzimu.
 
Usambaze umeme majumbani Kwa waya wa 100mm ( 10 cm) ? Mkishakunywa Kvant msisahau kunywa maji😁😁😁😁😁😁
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…