Waziri Masauni: NIDA kuna shida ya usimamizi, Uongozi una shida, Watu wanateseka kupata Vitambulisho

Waziri Masauni: NIDA kuna shida ya usimamizi, Uongozi una shida, Watu wanateseka kupata Vitambulisho

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Joined
Apr 18, 2017
Posts
3,984
Reaction score
13,760

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni amelazimika kutoka Ofisini na kufuatilia utendaji wa Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA) ambapo mamlaka hiyo imekuwa ikilalamikiwa na Wananchi kwa utendaji na utoaji wa Vitambulisho usioridhisha.

Waziri Masauni amefika katika Ofisi ya NIDA iliyopo Manispaa ya Ubungo na kukuta zaidi ya Wananchi 100 wakiwemo Wanafunzi waliohitimu Kidato cha Sita, hivi karibuni waliopo katika mchakato wa kuomba mkopo wa Elimu ya Juu wanatakiwa kuwa na Kitambulisho cha Taifa wakiwa hawapati huduma wanayostahili.

Pia soma;

KERO - Ugawaji wa NIDA wilaya ya Busega unasuasua zaidi ya mwezi. Wanafunzi tunaotegemea namba kuomba mkopo HESLB hatarini kukwama
 
Pole sana.

Nadhani NIDA ipo Top 5 ya mamlaka za serikali zinazokera zaidi nchini Tanzania.

Mi nilipata shida sana haya kuandikishwa tu na kupigwa picha.

Unapoteza siku nzima, tunafika unaambiwa kaanzie kwa Sijui nani nani huko..

Nilipopata namba nikatemana nao, nikatafuta Maza mmoja kijumbe wa CCM nikampa 20k afuatilie huko ofisi yao ya kata, kikitoka aniletee.
 
Pole sana.

Nadhani NIDA ipo Top 5 ya mamlaka za serikali zinazokera zaidi nchini Tanzania.

Mi nilipata shida sana haya kuandikishwa tu na kupigwa picha.

Unapoteza siku nzima, tunafika unaambiwa kaanzie kwa Sijui nani nani huko..

Nilipopata namba nikatemana nao, nikatafuta Maza mmoja kijumbe wa CCM nikampa 20k afuatilie huko ofisi yao ya kata, kikitoka aniletee.
Jina wanakosea wenyewe halafu marekebisho sasa utazungushwa hadi ukome na kukoma na bado hurekebishiwi na pesa umelipa washenzi sana hawa wanao itwa NIDA na wana matatizo ya kudumu.
 
Hivi kinachosababisha vitambulisho vichelewe ni kipi?,Mwenye uelewa anaweza niambie?
Kipindi cha JPM walidai machine inaprint sijui vitambulisho 100 tu kwa siku hivyo unaweza piga hesabu watu million 20+ watapata lini kitambulisho.

Nadhani ilipaswa walipwe kutokana na vitambulisho wanavyoprint lazima wangepiga kazi ila mishahara ipo hamna mwenye motisha. Na hapo wana training kila mwaka na maseminar kibao ya posho.

Hii nchi kuna vitu vinakera sana
 

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni amelazimika kutoka Ofisini na kufuatilia utendaji wa Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA) ambapo mamlaka hiyo imekuwa ikilalamikiwa na Wananchi kwa utendaji na utoaji wa Vitambulisho usioridhisha.

Waziri Masauni amefika katika Ofisi ya NIDA iliyopo Manispaa ya Ubungo na kukuta zaidi ya Wananchi 100 wakiwemo Wanafunzi waliohitimu Kidato cha Sita, hivi karibuni waliopo katika mchakato wa kuomba mkopo wa Elimu ya Juu wanatakiwa kuwa na Kitambulisho cha Taifa wakiwa hawapati huduma wanayostahili.

Pia soma;

KERO - Ugawaji wa NIDA wilaya ya Busega unasuasua zaidi ya mwezi. Wanafunzi tunaotegemea namba kuomba mkopo HESLB hatarini kukwama
CCM ni vilaza kweli Hadi waziri mwenye dhamana na taasisi iliyopo chini yake na analalamika kama mwananchi wa kawaida
 

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni amelazimika kutoka Ofisini na kufuatilia utendaji wa Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA) ambapo mamlaka hiyo imekuwa ikilalamikiwa na Wananchi kwa utendaji na utoaji wa Vitambulisho usioridhisha.

Waziri Masauni amefika katika Ofisi ya NIDA iliyopo Manispaa ya Ubungo na kukuta zaidi ya Wananchi 100 wakiwemo Wanafunzi waliohitimu Kidato cha Sita, hivi karibuni waliopo katika mchakato wa kuomba mkopo wa Elimu ya Juu wanatakiwa kuwa na Kitambulisho cha Taifa wakiwa hawapati huduma wanayostahili.

Pia soma;

KERO - Ugawaji wa NIDA wilaya ya Busega unasuasua zaidi ya mwezi. Wanafunzi tunaotegemea namba kuomba mkopo HESLB hatarini kukwama
Kwa hiyo mnaendelea kucheka na nyani!!
Haiwezekani kutolewa kitambulisho ichukue mwaka na zaidi hizo computer kazi zake ni nini!?
Ilitakiwa hiyo ofisi kufukuza wote kuanzia waziri hadi mfagiaji na mleta Chai.
Huu ni uzembe wa Hali ya juu!.
 
Cha kushukuru ni kupata namba ya NIDA ili upate huduma za jamii siyo kitambulisho! Kitambulisho utakata miaka.
 
Kwahiyo ndugu waziri anatuomba msaada wananchi tumsaidie kuwalalamikia nida Badala ya kuchukua hatua?
 
Kmme nilienda ofisini kwao kama mara sita ivi kuchukua hardcopy na kila nikienda wananiambia bado nikasema kmmzenu mkiniona tena nilivopata namba tu mwaka wa sita huu sijatia mguu
 
Hiyo Nida kawe ndio utalia , miongoni mwa ofisi za serikali zina unyanyasaji wa kutisha ni pale , watu wanafokewa kama watoto
Kupata huduma sasa mtihani kabisa kupoteza masiku na masiku kawaida ila utaambulia masimango kama unaenda kuomba hela,
Wazee inauma sana hamjui tu
Jamani Watanzania wenzetu mliopata dhamana ya kutusaidia ,tusaidieni wenzenu

Maisha yametupiga hata nyie mtupige? NIDA BADILIKENI BADILIKENI
 
Back
Top Bottom