LGE2024 Waziri Mchengerwa atangaza tarehe ya kuchukua na kurudisha Fomu za Uchaguzi wa Serikali za Mitaa, siku zaongezwa

LGE2024 Waziri Mchengerwa atangaza tarehe ya kuchukua na kurudisha Fomu za Uchaguzi wa Serikali za Mitaa, siku zaongezwa

Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
2,060
Reaction score
5,648
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais TAMISEMI, Mohammed Mchengerwa, ametangaza rasmi tarehe ya kuchukua na kurejesha fomu za kugombea kwenye Uchaguzi wa Serikali za Mitaa kuwa ni kuanzia tarehe 26 Oktoba hadi Novemba 1, 2024. Mchengerwa amewasihi wananchi wote wenye sifa za kugombea, kama ilivyoainishwa katika kanuni za uchaguzi, kujitokeza na kutimiza haki yao ya kikatiba.

"Kulikuwepo na malalamiko kwamba tarehe ya kuchukua na kurudisha fomu ni siku moja. Baada ya kupokea maoni, Serikali ilikubaliana kwamba tarehe ya kuchukua na kurejesha fomu itakuwa kuanzia tarehe 26 Oktoba hadi Novemba 1, 2024. Hivyo, nawasihi wananchi wote wenye sifa za kugombea kujitokeza na kutimiza haki yao ya kikatiba." alisema Mchengerwa.

Aidha, Mchengerwa amesisitiza umuhimu wa wasimamizi wa uchaguzi na wasaidizi wake kusimamia kanuni kwa usahihi na kuhakikisha mchakato unafanyika kwa haki na uwazi.

Pia, Soma:

+
Waziri Mchengerwa: Hakuna Uthibitisho wa madai ya Uandikishaji Wanafunzi Kupiga Kura
+ Waziri Mchengerwa: Uchaguzi wa Serikali za Mitaa Bara utafanyika 27 November, 2024
 
15 October 2024

MCHENGERWA AWAJIBU UPINZANI ''ACHENI KULETA TAHARUKI''


View: https://m.youtube.com/watch?v=RJZV4wqhwd4

Mimi waziri wa TAMISEMI nimepokea malalamiko ya kuhusu wasimamizi wakuu na wasimamizi wasaidizi wa uchaguzi wa serikali kuchagua viongozi wa vijijini, vitongoji na mitaa.

Na pia sanjari na hilo kuwakumbusha wasimamizi uchaguzi (Wakurugenzi wa wilaya / Halmashauri) na wasimamizi uchaguzi wasaidizi kukumbuka viapo vyao walivyokula kuhusu kanuni, sheria na majukumu ya kufanya kazi kwa ukaribu na mawakala wa vyama vyote na wale watia nia kuchukua fomu za kugombea uongozi ngazi hizo..

Kusisitiza hilo kupitia katibu mkuu wa wizara ya TAMISEMI, Tarehe 14 Oktoba 2024 nimewaandikia wakurugenzi wote ambao wanakofia ya pili kama wasimamizi wa chaguzi hii ya November 2024 kuwa warejee
’wa mujibu wa Tangazo la uchaguzi lililotolewa kwa kuzingatia kanuni ya 4 ya Kanuni za uchaguzi wa viongozi wa Mamlaka za Serikali za Mitaa (Tangazo la Serikali Na. 571, uchaguzi utafanyika tarehe 27 Novemba 2024 na Kwa mujibu wa Kanuni ya 11 (GN. Na. 571/Mamlaka za Wilaya, zoezi la uandikishaji wa wapiga kura litafanyika kuanzia tarehe 11 hadi 20 Oktoba 2024 katika vituo vilivyopangwa’’


Pia natoa rai wasimamizi wa uchaguzi kuzingatia miongonzo na kanuni kama zikivyoainishwa kayika tangazi " Na. 572, Na. 573, Na. 574 ya mwaka 2024" alisema Mchengerwa.
 
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais TAMISEMI, Mohammed Mchengerwa, ametangaza rasmi tarehe ya kuchukua na kurejesha fomu za kugombea kwenye Uchaguzi wa Serikali za Mitaa kuwa ni kuanzia tarehe 26 Oktoba hadi Novemba 1, 2024. Mchengerwa amewasihi wananchi wote wenye sifa za kugombea, kama ilivyoainishwa katika kanuni za uchaguzi, kujitokeza na kutimiza haki yao ya kikatiba.

"Kulikuwepo na malalamiko kwamba tarehe ya kuchukua na kurudisha fomu ni siku moja. Baada ya kupokea maoni, Serikali ilikubaliana kwamba tarehe ya kuchukua na kurejesha fomu itakuwa kuanzia tarehe 26 Oktoba hadi Novemba 1, 2024. Hivyo, nawasihi wananchi wote wenye sifa za kugombea kujitokeza na kutimiza haki yao ya kikatiba." alisema Mchengerwa.

Aidha, Mchengerwa amesisitiza umuhimu wa wasimamizi wa uchaguzi na wasaidizi wake kusimamia kanuni kwa usahihi na kuhakikisha mchakato unafanyika kwa haki na uwazi.

Pia, Soma:

+
Waziri Mchengerwa: Hakuna Uthibitisho wa madai ya Uandikishaji Wanafunzi Kupiga Kura
+ Waziri Mchengerwa: Uchaguzi wa Serikali za Mitaa Bara utafanyika 27 November, 2024
Hakuna intregrity, imani kwenye uchaguzi.

Rais na Familia yake moja anaamua matokeo ya Tanzania yote.
 
Uchaguzi uahirishwe ifanyike yote mwakani na usimamiwe na Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi.
Hata hiyo tume haiminiki bado. Huu ni mwanzo tu, tegemea wapiga kura wachache zaidi uchaguzi mkuu.
 
15 October 2024
Dodoma, Tanzania

AISHA MANDONGA ALIYEKUWA MGOMBEA 2020 DODOMA, AIBUKA MAZITO UCHAGUZI WA TAMISEMI 2024


View: https://m.youtube.com/watch?v=Xh_HpuVH_M8
Mwanachama huyo kiongozi mwandamizi wa CHADEMA aelezea mambo kibao yanayoenda ndivyo sivyo Dodoma, nguvu ya dola kutumika kukamata wanaCHADEMA wanaohamashisha kujiandikisha daftari la mpiga kura uchaguzi wa TAMISEMI 2024 ....
 
Chama dola kongwe FRELIMO kinajuta baada ya kufanya uchafuzi wa uchaguzi :

07 November 2024
Maputo, Mozambique

MAHAKAMA YA KIKATIBA MOZAMBIQUE YAKUBALI MAOMBI YA CHAMA CHA PODEMOS, KURA ZIRUDIWE KUHESABIWE


Chama cha upinzani PODEMOS nchini Mozambique pamoja na cha PAO wamepeleka ushahidi wa kilo Mia tatu za ushahidi katika karatasi, wakionesha uchafuzi wa uchaguzi uliofanyika Oktoba 9 2024 .

Vyama vya PODEMOS na PAO wameonesha ushahidi ambapo idadi ya kura zilizidi idadi ya watu walioandikishwa katika maeneo mbalimbali, ushahidi huu ni mojawapo ulioishawishi Mahakama ya Kikatiba kutaka kurudia kuhesabiwa kura kujua uhalali wa matokeo na washindi waliotangazwa.

Ghasia na maandamano yameliandama taifa hili la kusini mwa Afrika lilopata uhuru miaka ya 1970 na chama kongwe dola FRELIMO kutangazwa mshindi kwa zaidi ya miaka 40 toka uhuru.
 
Back
Top Bottom