Waziri Mkuu Kassim Majaliwa avamia mwendokasi, ahoji mapato yalipo kama wanashindwa kununua mabasi. Mkurugenzi wa fedha atumbuliwa

Majaliwa anaogopeka ila kuna baadhi ya viongozi wanamzidi kete akitembelea maeneo yao.
Wanamuandalia wapambe wenye nguo za rangi ya kijani na njano wana demkaaaaaaa yeye anatabasam na kuondoka
 
Waturejeshee route sisi watu binafsi, watz wengi si wazalendo kwakweli.
 
Kuna clip inazunguka ikimuonyesha kukasirishwa kwa upuuzi wa wale walioaminiwa kuendesha mradi wa mabasi ya mwendo kasi kwa niaba yetu! Nimemuangalia kwa umakini nikagundua pm alukuwa na kuzuni na uchungu mkubwa moyoni kiasi cha kulia kutokana na hujuma walioufanyia mradi wetu huu! Kwa mzigo huu juu ya nchi yake, ninaona nuru kuwa nchi yetu inayo hazina ya viongozi wenye uchungu na nchi yetu!

Mh. Majariwa, tunaomba uendelee hivyo hivyo, sisi wenye nchi tunatambua juhudi zako!

Mungu akubariki Mh. Majariwa, Mungu akubariki Mama yetu Samia! Mungu aibariki Tz!

Cheki hapo mwenyewe👇!

 
Kama mabasi yanatushinda vipi ndege!?
 
Unazipenda sana hasira!?
 
Huo mradi unakufa kama uda ilivyokufa. Viongozi wanazungukana tu hapo. Ilishasemekana kuna kiongozi anamiliki huo mradi kwa mgongo wa msukuma mmoja ambaye nadhani ansota ndani kwa uhujumu uchumi kuna fitina zinazunguka hapo mafahari wanapigana kutuibia.
 
Sadists on freak!

Utasikia aaaah, kazi ni ile ile watu wataisoma.

Kwani kazi ya urais ni kuumiza na kusomesha namba watu?

Inaonekana Sadists hamna mood na Samia kabisa, hawapi furaha.

Huyo Majaliwa tangu aanze kuzurula na media anafokafoka, miaka 6 sasa ameshatatua tatizo gani?

Wabongo bana, mtu akiwa anazurula huku anafokafoka kwenye media tayari anafaa kuwa Rais: Majaliwa, Jaffo, Makonda🤣🤣🤣🤣🤣
 
Ninaona nuru kuwa nchi yetu inayo hazina ya viongozi wenye uchungu na nchi yetu! Mh. Majariwa, tunaomba uendelee hivyo hivyo, sisi wenye nchi tunatambua juhudi zako!
Nonsense
 
We ndio sadist maana kitu cha umma unakiiba na kukiterekeza na raia wakiendelea kuteseka wakati ww unafurahia na familia yako!

Kama hufurahii raia kuteseka huwezi kuwa sehemu yao wanaohujumu miradi ya kimkakati kama huu! Hivi hilo basi lingekuwa lako nyumbani ungelitelekeza hivyo! Majariwa, tunakuelewa endelea hivyohivyo mpaka kieleweke! Wezi bado wanamuimbisha mama!
 
Wanajuana wasitubabaishe sasa miaka 5 wao walikuw wapi?
 
Siyo hasira unazozijua ww! Ni kuwa na mzigo kwa taifa lake! Huyu pm ni mzalendo! Na kama isingekuwa haki za binadamu, mtu angepokea bakora hadharani. Hivi ndivyo mimtu yenye akili za kipunda yanavyotakiwa kupelekwa!
Unazipenda sana hasira!?
 
Na sisi wananchi tuna haki ya kufahamu,kama mambo tunayolalamikia yanapatiwa ufumbuzi au S/kali inashughulika nayo vipi.

Wezi hawabembelezwi DART ni kichaka cha wezi hata hasiye na akili anaweza kuona jinsi tiketi zinavyokatwa ni upigaji mtupu hata Waitara alishawai kuongelea hilo swala ila akaishia juu juu hakuna action iliyochukuliwa.

Kongole PM
 
Hahahahahahaha hii huitwa like father like son
Majaliwa akitembelea ofisini kwako ni heri angekutembelea Magufuli.
Magufuli alikuwa anatazama upepo , Majaliwa anapekua mpaka nukta na hakuachi.
Majaliwa akitembelea ofisini kwako ni heri angekutembelea Magufuli.
Magufuli alikuwa anatazama upepo , Majaliwa anapekua mpaka nukta na hakuachi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…