Waziri Mkuu Kassim Majaliwa ni msafi kisiasa; Hana kashfa ya rushwa; anaaminika zaidi na wananchi/dola. Je, tupo tayari kuona mafisadi wanamstafisha?



Kabisa, akapumzike na usafi wake na wajukuu.
 
Leo amenisuuza roho Kwa kulikamata fisadi zulumaji la Ardhi Jiji la Dodoma likurugenzi Jose Mafuru
 
Tena bora ukae kimyaas....tiss waba file lake loote na lipo mezabi kwa mana siku nyingi sababu ni bro in faith acha tutoe ngoma juani.....tena machawa mkae kimya.....TMK kuhujumiwa stsnd mwaka wa 10 huu yeye ndio mfaidika usitake tuteme nyongo na ndoano.....uchafu wake woote TMK kukosa stand bus ......na ma lorry kwenda kwao kusini mfaidika ni yeye ......tena atuliee....
 
Majaliwa ni muadilifu sana

Mungu amtetee
Usiyoyajuaaaa.........team unajua nani anahudumia ?? Unajua gharama team hasa premier huko na salary plus usajili ?? Tafuta hela zako achana wanasiasa
 
Aliyeongopa siyo KASSIM Majaliwa, aliyeongopa alikuwa Waziri Mkuu katika kutekeleza majukumu yake ya kazi.

Hapa tunamjadili Mwalimu Kasim Majaliwa
Ipo siku utasema aliyekula rushwa ni waziri si fulani.
Scandal ya bandari na makontena ya yule maza vipi?
 
Nimesoma comment zote hakuna aliyejitokeza kwa fact kupinga uadilifu wa Majaliwa. Tukuze watoto kwenye maadili ya watu kama hawa.

Narudia tena; Majaliwa siyo mwizi na anawajali watanzania . Tumpe moyo asirubuniwe na mafisadi
 
Wanapiga hesabu za kumchomoa mama kinachomkwaza ni hofu kuogopa umma. Hawa wa kula kwa urefu wa kamba lao ni moja..kukabidhi dola kwa wahuni.
 
Aliyeongopa siyo KASSIM Majaliwa, aliyeongopa alikuwa Waziri Mkuu katika kutekeleza majukumu yake ya kazi.

Hapa tunamjadili Mwalimu Kasim Majaliwa
Haijawahi kutokea duniani kiongozi Mkuu wa Nchi awe mahututi kisha waliochini yake waanze kutangaza eti Mkuu wa Nchi yupo mahututi !!
Mimi huwashangaa wanaomlaumu Mheshimiwa Majaliwa !!
 
bado ana elements nyingi za magufuli jambo ambalo sio zuri. kufokea fokea watu ovyo, na mambo mengine mengi ya ubabe. pia, sidhani kama ni maskini, na usisababishe watu wafukue makaburi. msitirini tafadhali msikisanue. watu watakuja na diary hapa.
 
Wanapiga hesabu za kumchomoa mama kinachomkwaza ni hofu kuogopa umma. Hawa wa kula kwa urefu wa kamba lao ni moja..kukabidhi dola kwa wahuni.
Mleta uzi huu kwenye paragraph ya 9 amesema anaaminiwa sana na mifumo ya dola !
Kama hivyo ndivyo ilivyo ni nani tena mwenye ubavu wa kumchomoa ??!
Ngoja tuone !!
 
Wengine huwa wanastuliwa kwa kugongwa na nyundo lakini bado huwa hawastuki !
Afadhali yeye hustuka kwa konzi tu !
 
Yuko makini sana nafuraishwa na utendaji wake, anafaa kuwa Rais wa nchi.Hababaishwi, hajivuni, anajua anachofanya.Kutoka kwa Magu kwenda kwa Samia tungesikia mengi lkn yeye kimyaa utadhani hakukwazika, kifua chake ni kipana sana.
Ana kifua kipana katika uovu:

1) Aliratibu utekaji na kuumizwa kwa wapinzani wake ili asipate mpinzani, atangazwe kuwa amepita bila kupingwa.

2) Alisema uwongo kuwa Rais ni mzima wakati akijua kuwa anadanganya.

3) Kajengewa nyumba ya rushwa na mfanyabiashara.

4) Ana kashfa ya kujimilikisha mali za chama (rejea report ya Dr. Bashiru).

5) Alikurupuka kumfukuza daktari bingwa kwenye mkutano wa hadhara baada ya Mama mmoja kulalamika kuwa alitozwa pesa ili kufanyiwa operation (wakati yalikuwa ni malipo halali kwa mujibu wa taratibu za kuchangia gharama za matibabu). Lakini, Majaliwa kwaajili ya kutafuta sifa kutoka kwa wananchi waliohudhuria mkutano wake, aliamua kumdhalilisha daktari bingwa na akamsimamisha kazi. Na alipogundua amekosea, akamtaka daktari bingwa arudi kazini kimya kimya, bila hata ya kumwomba msamaha kwa kumdhalilisha kwa umma. Daktari aligoma, na hospitali ilikuwa na huyo daktari bingwa mmoja tu wa upasuaji.

6) Mpaka sasa, ni Waziri Mkuu batili kwa mujibu wa katiba. Katiba inatamka kuwa Waziri Mkuu atateuliwa na Rais kutoka miongoni mwa wabunge wa kuchaguliwa, Majaliwa hakupigiwa hata kura 1 na wananchi, na mahakama ilikwishatoa ufafanuzi kuwa kwa mujibu wa katiba, hakuna mbunge wa kupita bila kupingwa. Mbunge ni sharti apigiwe kura au ateuliwe na Rais kuwa mbunge. Lakini aliyeteuliwa na Rais hawezi kuteuliwa kuwa Waziri Mkuu. Majaliwa hajachaguliwa wala hajawahi kuteuliwa kuwa mbunge. Hivyo siyo mbunge halali na wala siyo Waziri Mkuu halali. Ingekuwa kwenye nchi zinazojitambua ambazo zinaongozwa na watu wanaojitambua, siku ile mahakama iliposema tu wabunge wanaotajwa walipita bila kupingwa ni batili, waziri mkuu alitakiwa kujiuzulu mara moja.

In short, ni mwovu sawa na wenzake.
 
Nimesoma comment zote hakuna aliyejitokeza kwa fact kupinga uadilifu wa Majaliwa. Tukuze watoto kwenye maadili ya watu kama hawa.

Narudia tena; Majaliwa siyo mwizi na anawajali watanzania . Tumpe moyo asirubuniwe na mafisadi
Afadhali hata ungesema tumpe moyo asiendelee kurubuniwa na kula rushwa, siyo kuanza. Aanze mara ngapi wakati amebobea. Mwenzio anakula rushwa ya mabilioni halafu unasema asije akarubuniwa.

Wewe unadhani lile ghorofa la rushwa alilojengewa na yule mwarabu pale Dodoma lina thamani kiasi gani?
 
Amepwaya sana mpaka kaletewa Naibu Waziri Mkuu.
Kaongezewa nguvu wala sio kupwaya, ila shida aliyeenda kuongeza nguvu hana tofauti na makamu wa Rais, kila siku nikutoa maushauri tuu.
 
Huyu rostam ni mtu hatari kwa mustakabali ya tanzania huru. Mama anamuamini huyu eti anajidai tukikubali uwekezaji (wa kijambazi )tutagawani kitu ila tukikataa tutagawana umaskini.
Nimekua namsikiliza lakini hata uchumi inaonekana hajui. Ukweli anachojua ni upigaji tu. Wawekezaji anaotaka kuwaleta ni wa kuumiza wananchi tu na kupora utajiri bila kutoa mchango wa maendeleo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…