Pre GE2025 Arusha: Waziri mkuu awasema viongozi wanaojipanga na kugombania vyeo

Pre GE2025 Arusha: Waziri mkuu awasema viongozi wanaojipanga na kugombania vyeo

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

the guardian 17

JF-Expert Member
Joined
Aug 15, 2024
Posts
395
Reaction score
570
Kunazidi kuchangamka sasa, ni kama ujumbe umetumwa kwa machalii wa Arusha, Gambo na Makonda

===
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Kassim Majaliwa, amewataka viongozi wa kisiasa na wa dini kuwa mstari wa mbele katika kuhubiri amani na mshikamano, akisisitiza kuwa migogoro mingi ya kisiasa inatokana na tamaa ya madaraka.

Akizungumza mkoani Arusha, Februari 26, 2025 wakati wa maadhimisho ya Siku ya Maridhiano katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Arusha (AICC), Majaliwa ameeleza kuwa migogoro mingi inayojitokeza katika jamii inachochewa na watu binafsi au vikundi vinavyotafuta madaraka kwa njia zisizo halali.

"Suala la migogoro limezungumzwa sana hapa, tunajua. Na Sheikh Kishki aliwasema sana wanasiasa kwa sababu huko ndiko kuna migogoro mingi. Kila mtu anatamani cheo, wanasahau kuwa cheo kinatolewa na Mwenyezi Mungu," amesema Majaliwa.

Ameongeza kuwa watu wengi wanapotamani nafasi za uongozi, huanza kutumia mbinu zisizofaa, ikiwemo kumchafua au kumhujumu aliyepo madarakani kwa fitna na hata mbinu za kishirikina.

"Badala ya kumwendea Mwenyezi Mungu na kumuomba akupatie nafasi, unamfuata aliyepo madarakani, unamfitini, unampiga vita, unampa shida yeye na familia yake. Lakini je, unapomtengenezea madhara huyo, hiyo nafasi inakuwa yako moja kwa moja? Mwenyezi Mungu amekuhakikishia kuwa ni yako?" amehoji Majaliwa.

Aidha, amesisitiza kuwa amani ya taifa inaweza kuvurugika kwa sababu ya migogoro inayosababishwa na watu wachache wenye tamaa ya madaraka, na hivyo ni jukumu la viongozi wa dini kuyasema haya wazi ili kulinda mshikamano wa kitaifa.

"Amani inatoweka na mtu mmoja mmoja, watu wawili, kikundi, na kundi likiwa kubwa inakuwa shida. Viongozi wa dini tuyaseme haya kwa uwazi ili kuhakikisha tunalinda utulivu wa nchi yetu," amehimiza Waziri Mkuu.

Kupata taarifa na matukio ya kimkoa kuhusu Uchaguzi Serikali za Mitaa ingia hapa: LGE2024 - Special Thread: Orodha ya Mijadala ya Mikoa yote Tanzania Bara inayoshiriki katika Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024
 
Majaliwa ajiunge tu Chadema na Wakili LISSU ,Atapeperusha bendera ya Nafasi ya Urais na atashinda.
 
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, amewataka viongozi wa kisiasa na wa dini kuwa mstari wa mbele katika kuhubiri amani na mshikamano, akisisitiza kuwa migogoro mingi ya kisiasa inatokana na tamaa ya madaraka.

 
HUYO anayesemwa ni MAKONDA tu anajifanya eti yeye ni zaidi anaweka vi-crip vya kujifagilia mafi yake
 

Attachments

  • images (2) (1).jpeg
    images (2) (1).jpeg
    44.3 KB · Views: 2
  • Screenshot_20250216-182754_1.jpg
    Screenshot_20250216-182754_1.jpg
    363.2 KB · Views: 2
Kunazidi kuchangamka sasa, ni kama ujumbe umetumwa kwa machalii wa Arusha, Gambo na Makonda

===
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Kassim Majaliwa, amewataka viongozi wa kisiasa na wa dini kuwa mstari wa mbele katika kuhubiri amani na mshikamano, akisisitiza kuwa migogoro mingi ya kisiasa inatokana na tamaa ya madaraka.

Akizungumza mkoani Arusha, Februari 26, 2025 wakati wa maadhimisho ya Siku ya Maridhiano katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Arusha (AICC), Majaliwa ameeleza kuwa migogoro mingi inayojitokeza katika jamii inachochewa na watu binafsi au vikundi vinavyotafuta madaraka kwa njia zisizo halali.

"Suala la migogoro limezungumzwa sana hapa, tunajua. Na Sheikh Kishki aliwasema sana wanasiasa kwa sababu huko ndiko kuna migogoro mingi. Kila mtu anatamani cheo, wanasahau kuwa cheo kinatolewa na Mwenyezi Mungu," amesema Majaliwa.

Ameongeza kuwa watu wengi wanapotamani nafasi za uongozi, huanza kutumia mbinu zisizofaa, ikiwemo kumchafua au kumhujumu aliyepo madarakani kwa fitna na hata mbinu za kishirikina.

"Badala ya kumwendea Mwenyezi Mungu na kumuomba akupatie nafasi, unamfuata aliyepo madarakani, unamfitini, unampiga vita, unampa shida yeye na familia yake. Lakini je, unapomtengenezea madhara huyo, hiyo nafasi inakuwa yako moja kwa moja? Mwenyezi Mungu amekuhakikishia kuwa ni yako?" amehoji Majaliwa.

Aidha, amesisitiza kuwa amani ya taifa inaweza kuvurugika kwa sababu ya migogoro inayosababishwa na watu wachache wenye tamaa ya madaraka, na hivyo ni jukumu la viongozi wa dini kuyasema haya wazi ili kulinda mshikamano wa kitaifa.

"Amani inatoweka na mtu mmoja mmoja, watu wawili, kikundi, na kundi likiwa kubwa inakuwa shida. Viongozi wa dini tuyaseme haya kwa uwazi ili kuhakikisha tunalinda utulivu wa nchi yetu," amehimiza Waziri Mkuu.
View attachment 3251615
Kupata taarifa na matukio ya kimkoa kuhusu Uchaguzi Serikali za Mitaa ingia hapa: LGE2024 - Special Thread: Orodha ya Mijadala ya Mikoa yote Tanzania Bara inayoshiriki katika Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024
Kura zenyewe zinaibwa wazi wazi ila wakikaa majukwaani wanasema mambo ya kudra
 
Kunazidi kuchangamka sasa, ni kama ujumbe umetumwa kwa machalii wa Arusha, Gambo na Makonda

===
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Kassim Majaliwa, amewataka viongozi wa kisiasa na wa dini kuwa mstari wa mbele katika kuhubiri amani na mshikamano, akisisitiza kuwa migogoro mingi ya kisiasa inatokana na tamaa ya madaraka.

Akizungumza mkoani Arusha, Februari 26, 2025 wakati wa maadhimisho ya Siku ya Maridhiano katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Arusha (AICC), Majaliwa ameeleza kuwa migogoro mingi inayojitokeza katika jamii inachochewa na watu binafsi au vikundi vinavyotafuta madaraka kwa njia zisizo halali.

"Suala la migogoro limezungumzwa sana hapa, tunajua. Na Sheikh Kishki aliwasema sana wanasiasa kwa sababu huko ndiko kuna migogoro mingi. Kila mtu anatamani cheo, wanasahau kuwa cheo kinatolewa na Mwenyezi Mungu," amesema Majaliwa.

Ameongeza kuwa watu wengi wanapotamani nafasi za uongozi, huanza kutumia mbinu zisizofaa, ikiwemo kumchafua au kumhujumu aliyepo madarakani kwa fitna na hata mbinu za kishirikina.

"Badala ya kumwendea Mwenyezi Mungu na kumuomba akupatie nafasi, unamfuata aliyepo madarakani, unamfitini, unampiga vita, unampa shida yeye na familia yake. Lakini je, unapomtengenezea madhara huyo, hiyo nafasi inakuwa yako moja kwa moja? Mwenyezi Mungu amekuhakikishia kuwa ni yako?" amehoji Majaliwa.

Aidha, amesisitiza kuwa amani ya taifa inaweza kuvurugika kwa sababu ya migogoro inayosababishwa na watu wachache wenye tamaa ya madaraka, na hivyo ni jukumu la viongozi wa dini kuyasema haya wazi ili kulinda mshikamano wa kitaifa.

"Amani inatoweka na mtu mmoja mmoja, watu wawili, kikundi, na kundi likiwa kubwa inakuwa shida. Viongozi wa dini tuyaseme haya kwa uwazi ili kuhakikisha tunalinda utulivu wa nchi yetu," amehimiza Waziri Mkuu.
View attachment 3251615
Kupata taarifa na matukio ya kimkoa kuhusu Uchaguzi Serikali za Mitaa ingia hapa: LGE2024 - Special Thread: Orodha ya Mijadala ya Mikoa yote Tanzania Bara inayoshiriki katika Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024
Tatizo la binadamu ni hilo, kuona bila yeye kujiona.

Kuwasema wenzake huku akichukia yeye kusemwa na akimsemwa, anajenga hila na fitina kubwa sana na mifano mingine kama hiyo.

Tayari fitina za Sisiem wanazozitengeneza kwa vyama vya upinzani Majaliwa kasahau.

Viongozi wa dini wakitia neno, wataambiwa wasichanganye dini na siasa.

Yeye mwenyewe atueleze, kupita kwake bila kupingwa katika jimbo la Ruangwa , ilikuwa ni kwa amani kule au ni nini hicho kilichofanyika nk nk.

Mungu kazisuta nafsi zetu tangu kutuumba kwetu, kwa kutuelekeza madole gumba yetu tunapowanyooshea wengine vidole.
 
Back
Top Bottom