Roving Journalist
JF Roving Journalist
- Apr 18, 2017
- 3,984
- 13,760
Majaliwa amesema “Watanzania tuna kila sababu ya kujivunia ushupavu aliouonesha wakati wa Mkutano huo na jinsi alivyodumisha msimamo thabiti wakati wote. Sina shaka kuwa Uongozi wake utaacha alama ya kudumu katika historia ya Umoja wa Mabunge Duniani.”
Aidha, Majaliwa amewaomba Wabunge na Watanzania wote kwa ujumla kuendelea kumuunga mkono Spika ili aweze kutimiza majukumu yake kwa ufanisi zaidi.
Soma Pia: Tulia Ackson kwenye Bunge la Dunia amejibu maswali vema sana. Ila ni vema adhibiti 'emotions'
“Sote kwa pamoja, tuendelee kumuomba Mwenyezi Mungu amjalie uzima, hekima na nguvu katika kuutumikia Umoja huo duniani,” amesisitiza Majaliwa.