Waziri Mkuu Majaliwa: Serikali Imetenga 1Trilioni kwa ajili ya mikopo

Waziri Mkuu Majaliwa: Serikali Imetenga 1Trilioni kwa ajili ya mikopo

P

Prime ana record ya kudanganya sijaona...nyie fatilieni.
Ajira sijui ngapi...hola. Rais yupo afya poa anadunda kazi Kama kawa...haya labda
Kwahiyo Kiongozi wetu haaminiki
 
Benki zipunguze processing fee pia,wanapiga parefu sana.
 
Hii ni habari njema sana.
Shida ni kwamba mtoa hii habari ana Historia ya kudanganya,, hii habari huenda pia ni muendelezo Wa ile tabia yake ya kusema uongo.
 
Hii ni habari njema sana.
Shida ni kwamba mtoa hii habari ana Historia ya kudanganya,, hii habari huenda pia ni muendelezo Wa ile tabia yake ya kusema uongo.

31F4F350-036E-4117-AD2D-DAC22AF840EF.jpeg
 
! Kwa sasa riba za bank kuu ni 7% lakini mikopo ya bank mpaka 21% hivyo tatizo sio riba ya serikali au bank kuu bali tatizo ni banks zenyewe
Nani wa kuzisimamia kama si BOT?
Kama Ikishindikana kwa mabenki hayo,serikali itumie mabenki yake kama Benki ya Kilimo,Benki ya Posta,n.k kuwapa maelezo sahihi ya riba kwa mteja.
Hizo Shailoki benki zisipewe hiyo fedha.
 
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amesema Serikali imetenga Tsh. Trilioni moja kwa ajili ya mikopo kwa mabenki na taasisi za fedha kwa riba ya asilimia tatu ili mabenki na taasisi hizo zitoe mikopo kwa riba isiyozidi asilimia 10.

“Serikali imeendelea kulegeza masharti ya uanzishwaji wa ofisi za wakala wa mabenki, kushusha riba inayolipwa kwa akaunti za fedha za mitandao pamoja na kutenga shilingi trilioni moja kwa ajili ya mikopo kwa mabenki na taasisi za fedha kwa riba ya asilimia tatu ili mabenki na taasisi hizo zitoe mikopo kwa riba isiyozidi asilimia 10"

Ametoa kauli hiyo jana wakati akiahirisha Mkutano wa Tano wa Bunge Dodoma, Bunge limeahirishwa hadi Februari mosi, mwakani, Majaliwa amesema hatua hiyo ni utekelezaji wa Mwongozo wa Maandalizi ya Mpango na Bajeti kwa mwaka 2022/2023.

Akizungumzia kuhusu, riba kubwa za mikopo kutoka kwenye mabenki na taasisi za fedha, Waziri Mkuu amesema Serikali imekuwa ikichukua hatua madhubuti kupitia Benki Kuu ya Tanzania ikiwemo kupunguza kiwango cha akiba kinachowekwa na mabenki katika Benki Kuu.
 
Hii ni habari njema sana.
Shida ni kwamba mtoa hii habari ana Historia ya kudanganya,, hii habari huenda pia ni muendelezo Wa ile tabia yake ya kusema uongo.
Taifa letu halina amani na Waziri mkuu wake.
 
Inatakiwa tujue Majaliwa anatumia id gani humu ili tuwe tunamuita anajisomea vitu kama hivi.
 
Back
Top Bottom