Waziri Mkuu Majaliwa: Tanzania lazima ijiimarishe Kiuchumi ili kuepuka utegemezi kutoka mataifa mengine duniani

Waziri Mkuu Majaliwa: Tanzania lazima ijiimarishe Kiuchumi ili kuepuka utegemezi kutoka mataifa mengine duniani

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
2,060
Reaction score
5,648
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa, amesema ni muhimu kwa Tanzania kuzingatia Sera za nje na kuimarisha mahusiano mazuri na mataifa mengine huku ikijikita zaidi katika kujitegemea kiuchumi.

Majaliwa ametoa kauli hiyo Bungeni Jijini Dodoma leo February 06,2025 wakati akijibu swali la Mbunge wa Mbozi, George Mwenisongole ambaye alitaka kufahamu kuhusu mipango ya Serikali kulingana na mabadiliko ya sera za nje ya nchi ambazo zinatajwa kuathiri sera za elimu, afya na uchumi za Tanzania.

Hata hivyo, amesisitiza kuwa licha ya mafanikio haya ya kidiplomasia, nchi inapaswa kujiimarisha kiuchumi ili kupunguza utegemezi.

"Ni muhimu kuzingatia Sera za nje. Rais Samia ameendelea kuifanya nchi hii kuwa na mahusiano na mataifa mengi duniani. Marekani ni moja kati ya nchi hizo. Muhimu kwetu, pamoja na upana huu wa mahusiano, ni kuhakikisha tunajiimarisha na kuwa na uwezo wa ndani wa kutekeleza mipango yetu. Bajeti zetu zinapaswa kumudu sekta zote muhimu kama afya, elimu, na maji, pamoja na maeneo mengine tuliyokubaliana na mataifa husika," alisema Majaliwa.

Aliongeza kuwa Tanzania ina uwezo wa kujitegemea kutokana na maliasili na rasilimali ilizonazo, na akatoa wito kwa Watanzania kushirikiana katika kuzitumia kwa maendeleo ya taifa.

"Kazi iliyopo sasa ni kuhakikisha tunashirikiana na kutumia rasilimali tulizonazo kujenga uchumi wa ndani," alihitimisha Waziri Mkuu.

Soma, Pia:
 
Tanzania haiwezi kujiimarisha kiuchumi kwa kutegemea hiki chama chakavu na viongozi wenye mawazo finyu ya kuwanunulia makatibu waenezi wa chama chakavu wa wilaya V8 za milioni 500 kila moja huku akina mama wanaohitaji huduma ya kujifungua wanaambiwa na mkuu wa mkoa Chalamila kama hawana hela za kununulia gloves za kujifungulia waende kwa wanaume waliowapa mimba ili wawasaidie kujifungua.
 
Tanzania haiwezi kujiimarisha kiuchumi kwa kutegemea hiki chama chakavu na viongozi wenye mawazo finyu ya kuwanunulia V8 za milion 500 kila moja makatibu waenezi wa chama chakavu wa wilaya huku akina mama wanaohitaji huduma ya kujifungua wanaambiwa na mkuu wa mkoa Chalamila kama hawana hela za kununulia gloves za kujifungulia waende kwa wanaume waliowapa mimba ili wawasaidie kujifungua.
ndio unasema cc CHADEMA tutaenda kubadilisha kila kitu?
Make Tanzania Great Again?
 
Tanzania haiwezi kujiimarisha kiuchumi kwa kutegemea hiki chama chakavu na viongozi wenye mawazo finyu ya kuwanunulia V8 za milion 500 kila moja makatibu waenezi wa chama chakavu wa wilaya huku akina mama wanaohitaji huduma ya kujifungua wanaambiwa na mkuu wa mkoa Chalamila kama hawana hela za kununulia gloves za kujifungulia waende kwa wanaume waliowapa mimba ili wawasaidie kujifungua.
Matumizi makubwa ya hovyo na ufisadi tupu
 
Huyu Toka ajue kuwa jimboni hana nafasi, na u PM hapewi tena, basi anapita mule mule kwa Mr Jobo.

Amesoma alama za nyakati.
 
Huyu Toka ajue kuwa jimboni hana nafasi, na u PM hapewi tena, basi anapita mule mule kwa Mr Jobo.

Amesoma alama za nyakati.
Zidhan kama ana mpango wa kuwa pm, na muda wake wa utumish umeshafikia kikomo. So hiyo sio sababu
 
Ni Mzee sana huyu.

Unasemaje kuhusu alichokisema?
  • Kuepuka utegemezi?
  • Kuimarisha Uchumi?
kama GT wetu hapa, una maoni gani?
Nashukuru, maoni yangu ni haya, 1. Tuache betting watu wafanye kazi 2. Matumizi makubwa na ya anasa serikalini yadhibitiwe hakuna cha misafara 3. Ajira zisiwe za upendeleo nafasi zote zitangazwe watu waombe washindanishwe tupate watu wazuri kuanzia Waziri mpka mfagiaji. 4. Pombe kali ziondolewe na hakuna kuingia bar kabla ya saa 12 jioni na mwisho saa 5 kamili usiku. 5. Wabunge wasilipwe sitting allowance na mishahara yao ishushwe isizidi 2M ili waingie watu wazuri na siyo hawa wasaka utajiri, viti maalum vifutwe bungeni. 6. Ajira zote ziwe za mikataba mwisho miaka 10. 7. Wezi na mafisadi wafiliwe na kufungwa na kusiwe na kinga kwa viongozi. 8. Elimu yetu iwe ni ya vitendo kwa 90% na siyo kukaa darasani. 9. Wataalam walipwe vizuri kuliko wanasiasa. 10. Viongozi wakutumia magari ya umma wawe ni Rais, Makamu, Spika, PM na Jaji Mkuu pekee na vyeo vya RC/DC/DAS vifutwe kabisa. Asante
 
Poapoa tumekusikia. Haya turudi kwenye mada husika.
Nashukuru, maoni yangu ni haya, 1. Tuache betting watu wafanye kazi 2. Matumizi makubwa na ya anasa serikalini yadhibitiwe hakuna cha misafara 3. Ajira zisiwe za upendeleo nafasi zote zitangazwe watu waombe washindanishwe tupate watu wazuri kuanzia Waziri mpka mfagiaji. 4. Pombe kali ziondolewe na hakuna kuingia bar kabla ya saa 12 jioni na mwisho saa 5 kamili usiku. 5. Wabunge wasilipwe sitting allowance na mishahara yao ishushwe isizidi 2M ili waingie watu wazuri na siyo hawa wasaka utajiri, viti maalum vifutwe bungeni. 6. Ajira zote ziwe za mikataba mwisho miaka 10. 7. Wezi na mafisadi wafiliwe na kufungwa na kusiwe na kinga kwa viongozi. 8. Elimu yetu iwe ni ya vitendo kwa 90% na siyo kukaa darasani. 9. Wataalam walipwe vizuri kuliko wanasiasa. 10. Viongozi wakutumia magari ya umma wawe ni Rais, Makamu, Spika, PM na Jaji Mkuu pekee na vyeo vya RC/DC/DAS vifutwe kabisa. Mchango wangu huo hapo
 
Hivi juzi na jana alikuwa wapi Kweneye sheree zao za dodoma ccm.
IMG_0521.jpeg
 
Hivi Waziri Mkuu Majaliwa ana maoni yake binafsi kweli? :think3D: Kila anapohutubia au kuongea lazima amtaje Daktari Samia Suluhu Hassan. 🤔 Ni kweli kwamba yeye hana maono au mawazo yake binafsi au yeye ni mwangwi wa SSH⁉️
 
Nashukuru, maoni yangu ni haya, 1. Tuache betting watu wafanye kazi 2. Matumizi makubwa na ya anasa serikalini yadhibitiwe hakuna cha misafara 3. Ajira zisiwe za upendeleo nafasi zote zitangazwe watu waombe washindanishwe tupate watu wazuri kuanzia Waziri mpka mfagiaji. 4. Pombe kali ziondolewe na hakuna kuingia bar kabla ya saa 12 jioni na mwisho saa 5 kamili usiku. 5. Wabunge wasilipwe sitting allowance na mishahara yao ishushwe isizidi 2M ili waingie watu wazuri na siyo hawa wasaka utajiri, viti maalum vifutwe bungeni. 6. Ajira zote ziwe za mikataba mwisho miaka 10. 7. Wezi na mafisadi wafiliwe na kufungwa na kusiwe na kinga kwa viongozi. 8. Elimu yetu iwe ni ya vitendo kwa 90% na siyo kukaa darasani. 9. Wataalam walipwe vizuri kuliko wanasiasa. 10. Viongozi wakutumia magari ya umma wawe ni Rais, Makamu, Spika, PM na Jaji Mkuu pekee na vyeo vya RC/DC/DAS vifutwe kabisa. Asante
Asanti kwa maoni yako.🙏

unaonaje hili suala la kujitegemea kiuchumi? kumbuka SaDC in soko kubwa sana lina watu takriban 300milion + na per capita last time I checked approx $2000 unafikiri tutaweza kama nchi kuepuka utegemezi, na kuvushwa kwenda mu nchi tunayoitaka?
 
Back
Top Bottom