Waziri Mkuu: Tumesitisha Sunday school na Madrasa, tulichoruhusu ni Ibada tu tena zifanyike kwa muda mfupi kisha waumini waondoke

Muonee huruma bibi wetu hajawahi ona maji yakitiririka kwenye bomba tangu tupate uhuru wa bendera Hapa kwanini asichanganyikiwe? Kwanza angalia bonge la sendozi la nguvu analo liosha kilemba cha kinaijeria alafu wewe unamwita mbishi!!!

Hao ni wale wabishi wa kusema...
nimeanza kuliona jua kabla yenu... utaniambia nini..


Cc: mahondaw
 
Huyu waziri Mkuu ndiye wanamtegemea ashike kijiti cha Magufuli kwa mwaka 2025 mbona kama anashindwa kufanya maamuzi magumu.

Kiuhalisia Nchi yetu haina dini hivyo haifungamani na upande wowote iwe ni ukiristo ama uislamu..

Sasa hili la Waziri Mkuu kuruhusu ibada ziendelee ili hali wanajua fika ugonjwa huu uenezaji wake ni mkubwa mno katika mikusanyiko ya wetu wengi ni kuikosea sana Jamhuri ya Muungano...

Ni kawaida sana katika majanga kama haya tunaona sekta mbalimbali zimeanza athirika mfano Utalii, sekta ya usafirishaji hivyo basi hata hawa wafia dini lazma waathirike tu katika kipindi hiki ( Hapa ni lazma makanisa na misikiti kufungwa hadi pale hali itakapotengemea)

Tunaona wazi kabisa wenzetu waliotuletea dini wao wamefunga hayo makanisa na misikiti kwanini sisi tushindwe? Na ukiangalia wachubgaji wetu ni hawa feki ambao muda wanapata muda badi wakurekodi filamu za ngono..

Na kama wataeuhusu hili ibada kuendelea ili hali kuna mikusanyiko basi sijaona umuhimu wowote wa serikali kuzifunga shule na vyuo kuendelea na masomo yao.

Embu serikali iwe serious kidogo kwa hili jambo hizi ibada huwenda ndio ikawa njia moja wapo kubwa ya kuneeza huu ugonjwa ndani ya Nchi.



Sent using Jamii Forums mobile app
to
 
Ndugu yangu Michelle tunaongozwa na watu wasio na maono kabisa yaani Mtoto asimuambukize mzazi Mzazi ruksa kumuambukiza Mtoto hii ni akili au matope?
Kwa sababu ya kuto kuelewa kwenu kama mnaakili mtajua hapa imetumika psychological prohibition.

Sasa hawa viongozi wa dini na theology zao kama bado mazwazwa basi wasubiri katazo rasmi
 
Kama viongozi wa dini na serikali wanakua wazito kuchukua hatua tuwasaidie. Tusiende makanisani wala misikitini. Hakuna haja ya kusubiri tamko kwa sababu hakuna atakayekuja kukulazimisha uende
 
Hivi sisi ndiyo tuna upako sana kuliko roma na meka?

Sent using Jamii Forums mobile app
Who is Rome and Mecca? Je sio wanadamu kama sisi? Hii argument ya kitoto sana. Acheni kuwakuza as if wao ni miungu wadogo. Jenga hoja based on merits. Kwa hiyo Rome na Mecca wakiamua kuuza nchi zao na sisi tutafuata simply kwa sababu wao ni Mecca na Rome?
 
Sisi wakristo maandiko yako clear kabisa.
Yesu alisema "wakikusanyika wawili watatu kwa jina langu na mimi nitakuwa pamoja nao"

Hii inaonesha sio lazima tukusanyike wote makanisani. Tunaweza kusalia nyumbani kwa jina la Yesu na Yesu atakuwa pamoja na sisi..

Haya mambo tutakuja kujuta..

Kwanza kabisa inatakiwa mipaka ya dar ifungwe.. yaruhusiwe kutoka maroli ya mizigo na magali yanayoleta huduma mikoani tu na sio abiria.. tena wanaotoka wanapimwa kwanza..

Wasioofunga lile jiji next time kukiwa na press conference Dodoma na moro kutakuwa na corona.
 
huyu hawezi kuwa Majaliwa nayemjua mimi. amepokea agizo somewhere. Anayeweza kunipa sababu ya kufanya hivyo,naomba. Kwa nini Sunday school peke yake?
 
Ni ujinga uliotukuka kutotambua roma na meka katika habari za imani

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ni ujinga uliotukuka kutotambua roma na meka katika habari za imani

Sent using Jamii Forums mobile app
Sio ujinga hata kidogo. Wanaoishi kule ni wanadamu wenye maamuzi huru. Sisi pia ni wanadamu wenye maamuzi huru. So tunapojadili mambo yetu hayapaswi kuwa remote controlled na Mecca, Medina, Vatican, au Jerusalem.
 
Kwahiyo wazazi waende wabebe ugonjwa wapeleke nyumbani kwa watoto na wafanyakazi waliobaki nyumbani? Kuombea taifa lipi sasa? Linaloenda kuambukizwa ibadani likaambukize nyumbani? Nini shida na hizi ibada? Tunataka kumfurahisha nani?
Ingekuwa zamani za kale wazee au wahenga wangesema kuwa hili ni janga na tufanye matambiko ili lituepuke lakini kizazi hiki cha technolojia na ukoloni hatuna hao watu tena badara yake tuna Dini za mapokeo ambazo kwetu sote tunaoamini kupitia hizo Dini za mapokeo tumeanishwa kuwa kupitia Misikiti na Makanisa ni sehemu ya kuomba msamaha na reheme ili tupate kuponywa na kubarikiwa.

Hivyo kanisani na misikitini hakuna tunachokwenda kutafuta zaidi ya kuomba msamaha ili Gonjwa hili lituepuke kwa maana ndio adhabu pengine mwenyezi mungu ameamua kuidhibu dunia kutokana na maasi mengi yanayotokea duniani.

Kuna mashoga, Makahaba wameongezeka sana na mambo mengi machafu Dunia inapitia hivyo Mungu pekee ndio kimbilio letu basi ikibidi tumuombe pengine atasikia sisi wanyonge tusioweza kujitetea kiuchumi.

Pia tunaenda makazini kwa sababu kula yetu inategemea kazi ndio tupate kula sisi sio kama wale ambao Serikali inaweza kuwalipa wananchi wake wasipofanya kazi.
 
Mh. waziri mkuu hata Ibada funga tu. Maana kanisa x kuna sala fupi tu ya kuombea Corona kama kisehemu tu. Ila mwendo ule ule.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…