Waziri Mkuu: Tumesitisha Sunday school na Madrasa, tulichoruhusu ni Ibada tu tena zifanyike kwa muda mfupi kisha waumini waondoke

Waziri Mkuu: Tumesitisha Sunday school na Madrasa, tulichoruhusu ni Ibada tu tena zifanyike kwa muda mfupi kisha waumini waondoke

johnthebaptist,
Hivi unaposema kuwa Ibada zifanyike tu kwa muda mfupi tena kwa Kuliombea Taifa kisha Watu watawanyike ina maana kwamba kwa muda huo huo mfupi hakutoweza kuwa na Maambukizi kama baina yao hao Waumini wapo ambao wameshapatwa na CORONA?

Kwani Serikali ikisema na Kuamrisha kutokuwepo na Ibada kwa sasa na Kusisitiza (Kuwaomba) Watu Waabudie wakiwa Makwao itachukiwa au itaongezewa Dhambi zake na Allah / Mwenyezi Mungu huko Mbinguni Kwake?

Kuna Kauli zingine za Kidhaifu mno na bahati mbaya zinatoka kwa wenye Dhamana kabisa Kimamlaka na Taifa.
 
Baada ya hili janga kupita salama wapwa watakaa chini kujadili hili la dini vizuri ikiwezekana kautaratibu ka kuabudu home home kaendelee tu. Sema wenye makanisa watalalamika sadaka za live
Twende twende twende.

Hii imeonyesha wazi kuwa dini faida yake ni kustaarabisha jamii tu.
They can't do far from that.

Watu wa dini wangekuwa wanaweza kufanya zaidi ya hilo wasingepangiwa ratiba

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ukiwa unaendesha familia yako halafu ukataka kuiga mtindo wa jirani yako anavyoongoza familia yake, ujue wewe ni kidume suruali,

Semea nchi yako wewe unaonaje?
Kwa taarifa yako hadi sasa hakuna hatua yoyote au maarifa ya kipekee iliyochukuliwa na serikali yetu katika kupambana na corona ambayo ni tofauti na nchi nyingine.

Kinachofanyika ni kupuuza baadhi ya hatua ambazo ni muhimu wakidhani kufanya hivyo kutaonesha "ushupavu" wa Rais Magufuli kwamba hatishiki na "kakitu kadogo kanakowasumbua mabeberu".
 
Viongozi wa dini walipaswa kutumia busara kulinda watu wao.Ila naona wengi wana kiburi wanachokibatiza kwa jina la imani.

Ibada ya kweli hufanyika moyoni mwa mtu na si kanisani ama msikitini.

Wengi hasa wakristo ni wauza sura tu kanisani.Wanaenda kuoneshana mavazi,mitindo ya nywele, Urembo na umaridadi.

Utakuta mbwembwe za waimbaji na fasheni za mavazi kuanzia kwa mchungaji hadi kwa sister du mwimba kwaya na brazameni kiongozi wa nyimbo za sifa.

Viongozi wa dini,muwe spiritual,muwe na busara.Kiburi cha uzima sio kizuri

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hawa ni wale binadamu wabishi...



Cc: mahondaw
Muonee huruma bibi wetu hajawahi ona maji yakitiririka kwenye bomba tangu tupate uhuru wa bendera Hapa kwanini asichanganyikiwe?

Kwanza angalia bonge la sendozi la nguvu analo liosha kilemba cha kinaijeria alafu wewe unamwita mbishi!!!
 
..kufunga madrasa na sunday schools ni jambo zuri.

..lakini nadhani kuachia ibada ziendelee tutakuwa tunarudisha nyuma mafanikio na faida za kufunga madrasa na sunday school.

..Je, watoto hawaruhusiwi kwenye hizo ibada ambazo serikali imeruhusu ziendelee?
Niliishanga sana Serikali kufunga vyuo na shule na kuacha misikiti na makanisa

Kuna tatizo kubwa sana la siasa. ''Karantini'' zina maana yake. Huwezi kuzuia chuo halafu wanachuo hao hao wakaenda misikitini na makanisa ukasema umefanya jambo la maana.

Hey ! Corona haina muda wa kuambukiza, unaipata muda wowote na hakuna muda wa kuambukizwa
Hakuna mantiki ya kukaa muda mfupi.


Suala hapa ni kufunga makanisa na misikiti watu wasali Majumbani.

Vatican wamefunga, Mecca wanafunga hija sisi hatuwezi kufunga misikiti na makanisa! Real !
 
Tatizo siasa zimewekwa mbele kwenye kila kitu kinachofanyika hapa Tz.
 
Japo ni muhimu kufuata maagizo lakini kuna mambo mengine ni kujiongeza tu wewe mwenyewe. Ukipata hilo gonjwa leo hii huyo aliyekuambia ukusanyike hautamwona na pengne ukafa kabisa.

Hapa jizuie mwenyewe na zuia familia yako isikusanyike, piga stop wageni hapo hom, fullstop.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hv anajua wasabato wanakaa. Kanisan siku nzima from 10am to 5pm or 6pm. Nahis wanaotumia muda.

Mchache wa kuswali zaid ni waislam ukiondoa mawaidha wakristo minimum 2.5hrs mpaka 4hrs


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Back
Top Bottom