makanisa ya kilokole mengi yameongeza siku za ibada badala ya kupunguza, watu wanasali jumatatu hadi jumapili alafu mafundisho yaleyale ya kutoa zaka malimbuko sadaka. Yaani shida tupu kichwa cha mwafrika, serikali isipojiangalia kwa jicho pana itazilaumu taasisi za dini lakini wananchi watailaumu serikali kwa uzembe huu....serikali kipindi hiki ilitakiwa isionee aibu mtu yeyote ama taasisi yeyote(usipoziba ufa utajenga ukuta), ukionea aibu mtu utaua watu wengi sana.
serikali iwe makini sana, ikiwezekana wasimamie taasisi za dini kama mtoto mdogo, kuna wanajeshi wanaoonekanaga msimu wa matukio maalum pekee...kwanini hao wasipewe kazi za kusimamia taasisi za dini kipindi hiki?, waingiao misikitini na makanisani wavae masks wakati wote ndio waingie ibada zao, wanawe maji, wakae mbalimbali kwenye viti,
muda wa ibada usizidi saa 1 na nusu yaani usizidi dakika 90, ibada iwe siku moja kwa wiki yaani ijumaa waswali waislamu, jumamosi wasabato na jumapili hao wengine wote waliosalia. Jamani serikali saidieni wananchi wenu ambao elimu zao ni duni, maisha yao ni duni, afya zao ni duni, kula yao ni duni (ishi yao duni). Mtahukumiwa mbinguni kwa mkitendacho duniani...tenda wema daima!!