Waziri Mwigulu: Hatubani matumizi kwa kukopesha watu magari yanayowekewa mafuta na Serikali

Waziri Mwigulu: Hatubani matumizi kwa kukopesha watu magari yanayowekewa mafuta na Serikali

H

Kuna wakati watu wanashindwa kutofautisha kati ya kusoma na elimu. Matumizi ya gari sio mafuta tu bro, bali kuna wear and tear za matairi, engine, break, oil, vioo, breakdowns, nk. Ni mjinga nani atakaependa kupeleka gari lake alilokopeshwa kwenda vijijini mbali, njia mbovu, matope kwenda kuhudumia jamii kwa gari lake binafsi? Ni nani atagharamia ununuzi wa matairi, spea na service ya gari ili ofisa aende safari za umma? Hii ni njia nyingine ya watumishi kuacha kwenda kuwahudumia wananchi kwa visingizio vya gari mbovu, matairi yamekwisha, gari inahitaji kufanyiwa service, nk.

Yaani niweke matairi yangu mapya kwenye gari langu halafu nitembelee kwenda kilomita 600 kwa kazi za serikali. Tutapunguza efficiency kwenye kuhudumia watu kwa kisingizio cha gari bovu.
Atapeleka tuu kwani magari ya Wabunge huwa hayaendi Vijijini?

Na kwa taarifa yako Serikali itakopesha magari yanayoweza kukabiliana na hayo mazingira.
 
matumizi mabaya ya magari ya serikali ndo yanayoongoza.magari mengi yanatumika kwenye mifugo,biashara binafsi,kubeba ndugu wa mabosi kutoka pointi moja hadi nyingine na hasa siku za wikiendi.wizi wa mafuta na matengenezo ni sehemu nyingine na hapa wahusika wakuu ni madereva na kwenye matengenezo ni TEMESA.
Ndio serikali inalenga kuondoa huo upuuzi.
 
Kwa hiyo mwenzio kakosea nini hapo? Maana mapendekezo yake ya kubana matumizi ni bora na effective zaidi..

Wewe umejikita kwenye issue moja tu, MAGARI na affiliates zake i.e za maintanance, mafuta, ununuzi wa vipuri nk lakini mwenzako kaleta mapendekezo ya maeneo mengine ili kubana zaidi ambayo;
✓ Magari hayo hayo hata kama watakopeshwa, anasema basi magari hayo yafungwe mfumo wa kutumia gesi. Je, si kupunguza gharama hapo??

Akaendelea kutoa mapendekezo mengine kwa haya;

✓ Kupunguza baraza la mawaziri..
✓ Kupunguza idadi ya wabunge especially wasio na majimbo, wasiochaguliwa na watu..
✓ Kuondoa utaratibu wa chaguzi ndogo baada ya mtu kujiuzuru mwenyewe, kufukuzwa au kufa ambazo hutumia mabilioni ya fedha badala yake itafutwe njia nyingine isiyo ya gharama ya kufanya replacement.?
✓ Kuwa na effective supervision ya sheria ya public procurement..

## Sasa ndugu, kwa maelezo haya, hivi ni nani hajui maana ya "kubana matumizi"; wewe The Sunk Cost Fallacy au mleta hoja ndugu kavulata?

##Aidha, mwenzio katoa hoja zaidi ya 6 za kubana matumizi lakini wewe unang'ang'ana na moja tu halafu wewe kwa sababu hiyo, unam - combine mwenzio na "majizi" ambao ni nyie CCM na serikali yenu msiopenda kabisa kushauriwa namna bora na sahihi za kubana matumizi kwa njia hizo? Don't you think that you're so evil and wicked?
Hilo la gas tayari serikali imekwaisha Anza kulifanyia Kazi 👇
 

Attachments

  • Screenshot_20220612-133616.png
    Screenshot_20220612-133616.png
    122.1 KB · Views: 6
Ungekosoa kwa namba ungekuwa umenisaidia, sio kesi

Mbunge analipwa kiasi gani kwaajili ya mafuta ya gari kwa mwezi, lita ngapi?

Au labda nizame kwako, MUONGOZO unasemaje?
Magari yatakayonunuliwa na Serikali Kwa ajili ya watumishi yatakuwa economy kuendana na pesa atakazopewa mtumishi.
 
Kwa nini asilipwe transport allowance badala ya kupimiwa mafuta kama swala ni kusafiri kutoka nyumbani kwenda kazini, maana kama wanakopeshwa hayo magari wayatumie pia kwa kazi za ofisi, badala ya kupimiwa mafuta peke yake wanatakiwa kupimiwa na pesa ya service.
Options zote zitaandaliwa ndio maana mjadala uko wazi na utekelezaji ni mpaka mambo yote yapatiwe majibu.
 
H

Kuna wakati watu wanashindwa kutofautisha kati ya kusoma na elimu. Matumizi ya gari sio mafuta tu bro, bali kuna wear and tear za matairi, engine, break, oil, vioo, breakdowns, nk. Ni mjinga nani atakaependa kupeleka gari lake alilokopeshwa kwenda vijijini mbali, njia mbovu, matope kwenda kuhudumia jamii kwa gari lake binafsi? Ni nani atagharamia ununuzi wa matairi, spea na service ya gari ili ofisa aende safari za umma? Hii ni njia nyingine ya watumishi kuacha kwenda kuwahudumia wananchi kwa visingizio vya gari mbovu, matairi yamekwisha, gari inahitaji kufanyiwa service, nk.

Yaani niweke matairi yangu mapya kwenye gari langu halafu nitembelee kwenda kilomita 600 kwa kazi za serikali. Tutapunguza efficiency kwenye kuhudumia watu kwa kisingizio cha gari bovu.
Mbona wabunge wanafanya ziara kwa magari ya kukopeshwa.sema wewe ni mbinafsi tu huna lolote! Kwanza unabidi utambue utakopeshwa kama umepandishwa cheo kinachostajili uwe na gari,kwa mantiki hiyo utapewa mkopo wenye masharti nafuu ili ununue gari let say mkopo usio na riba.ubaya uko wapi hapo?
 
Tatizo lipo hapo kwenye kupimiwa...unafahamu kuwa tangu enzi zileee za msoga, walikuwa wanapimiwa mafuta ila kwa bei ya tsh 2,500 kwa lita, mind you bei ya lita siku zile ilikuwa sijui kati ya 1,200 na 1,600

Sasa ukipewa lita 75 kwa wiki kwa bei ya sh 5,000 kwa lita, kuna kubana matumizi hapo?
Nionavyo Mimi mafuta wapewe fixed amount kwa mwezi Kama wanavyowekewa wabunge. Ukiwe fixed amount itajenga nidhamu ya Safar za viongozi na kupunguza wizi huo wa madereva. Viongozi watafanya Safari za lazima tuu. Kumbuka wameelekezwa kufanya mikitano mingi mtandaoni
 
Watatakiwa wa charge mileage Mkuu...mimi alternatively naona watembelee vanguards,kluger,fords waachane na hiyo midude yaani moja 400M tayari una gari karibu 10 hapo.
Sasa magari makubwa ya 400M kununulia (kukopesha) watumishi wote wanaostahili kupewa magari watamaliza madeni Yao kwa muda gani? Je, akiondolewa kwenye nafasi kabla ya muda deni lake litalipwaje?
 
Mbona wabunge wanafanya ziara kwa magari ya kukopeshwa.sema wewe ni mbinafsi tu huna lolote! Kwanza unabidi utambue utakopeshwa kama umepandishwa cheo kinachostajili uwe na gari,kwa mantiki hiyo utapewa mkopo wenye masharti nafuu ili ununue gari let say mkopo usio na riba.ubaya uko wapi hapo?
Ubaya ni wananchi kugongojea huduma ya mtumishi ambae hawana uhakika kama gari lake ni nzima au ni mbovu Leo, ipo au imeibiwa.
 
Hapana bado halijafanyiwa maamuzi.
Nilitegemea kusikia kwenye bajeti ya serikali kuwa kila gari la umma na serikali linaenda kufungwa mfumo wa kutumia gesi ili litumie gesi na ushuru sifuri wa vifaa vinavyotumika kubadilishia mifumo kutoka mafuta kwenda gesi.
 
Back
Top Bottom