Ndugu yangu Mtanzania,
Tanzania ni shamba la bibi, kila mtu akipata nafasi anavuna apendavyo. Swala la hizo gharama nilikuwa nime-reserve comments zangu na ndio maana nikasema tutaingia hasara mara 2.
Kama NHC ingekuwa inatengeneza faida ya mabilioni, ningeweza kuona kwamba it is worthy it, lakini wako choka mbaya. Hela za kujenga nyumba mpya hawana. Hela za kukarabati nyumba alizojenga Nyerere na zile tulizowadhulumu wahindi, hakuna. Leo Wizara inakwenda ku-spend shilingi milioni 70 kwa ajili ya kumpata MD/DG wa NHC!
Mimi ninafikiri kwamba Idara Kuu ya Utumishi wangeanzisha kitengo ambacho kingekuwa kina deal na kufanya recruitment ya watu kama hao badala ya kupoteza mamilioni ya fedha kwa kampuni binafsi. Tanesco nao wamefanya hivyo, lakini sijui wametumia fedha kiasi gani. Ni system nzuri inayosaidia kupata mtu mwenye sifa zinazotakiwa, but gharama zake zinakuwa inflated sana.