Roving Journalist
JF Roving Journalist
- Apr 18, 2017
- 3,984
- 13,760
Huduma hizo ni pamoja na uombaji na ulipaji wa pasi za kusafiria, huduma za kutuma na kupokea fedha ndani na nje ya nchi, huduma za afya, biashara ya kimtandao, leseni za magari na nyinginezo.
Waziri Nape ametoa kauli hiyo Julai 17, 2024, wakati akizungumza na wananchi wa vijiji vya Luhuha, Kata ya Nyakagomba wilayani Geita na Kijiji cha Busonzo Kata ya Busonzo Wilayani Bukombe, katika Mkoa wa Geita.
"Huko tunakokwenda tunayaendea mabadiliko makubwa sana ya sayansi na teknolojia na matumizi ya TEHAMA, usipoyajua utajikuta umeachwa nyuma na Serikali ya Rais Samia haitaki kumuacha nyuma Mtanzania yeyote," amesema Waziri Nape na kuongeza;
Amesema minara inayokaguliwa ni sehemu ya mradi wa minara 758 ambayo Serikali inatoa ruzuku kupitia Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF) na kusisitiza "niwe mkweli tangu mfuko huu uanzishwe haijawahi kutekelezwa minara mingi kiasi hiki kwa wakati mmoja".
Aidha, Waziri Nape amemuomba Mkuu wa Mkoa wa Geita Mhe. Martin Shigela kuzungumza na Wakala wa Barabara Vijijini na Mijini (TARURA) na Wakala wa Umeme Vijijini (REA) ili watoe kipaumbele cha kupeleka huduma za miundombinu ya barabara na umeme kwenye maeneo yote inakojengwa minara ili kusaidia kupunguza gharama za uendeshaji wake na hivyo wananchi wapate mawasiliano saa 24.
Amesema, mnara mmoja unatumia takribani shilingi milioni 1.8 kwa mwezi kwa ajili ya mafuta ya kuendeshea jenereta lakini ukipelekwa umeme gharama za uendeshaji zinapungua hadi shilingi 400,000 kwa mwezi.