Waziri Nape Nnauye anapitia wakati mgumu kiutumishi; walichomfanya BBC bora angekataa kuhojiwa au angekaa kimya; watu wanammaliza kisiasa

Waziri Nape Nnauye anapitia wakati mgumu kiutumishi; walichomfanya BBC bora angekataa kuhojiwa au angekaa kimya; watu wanammaliza kisiasa

Resilience

JF-Expert Member
Joined
Jan 4, 2023
Posts
1,096
Reaction score
4,948
Nape Nauye amepata mashambulizi makubwa sana mengi yakiwa yanatokana na historia yake kisiasa. Yapo makosa ya kisiasa ameyafanya na sasa yanamgarimu sana.

1. Kutumia goli la mkono kushinda uchaguzi
2. Kulazimisha tume ya uchaguzi imtangaze mshindi bila kupingwa
3. Kumtukana JPM akiwa hai
4. Kwenda ikulu kuomba msamaha akimulikwa na camera
5. Kumkejeli JPM baada ya kusikia amefariki
6. Kutukana wanasiasa wenzake ili apate umaarufu
7. Kumtukana Tundu Lisu
8. Kuwa na elimu inayotiliwa mashaka.

Haya na mengine yamemfanya ashambuliwe kirahisi na wapinzani ndani na nje ya chama bila kupata misaada.

Ukitaka kupima chuki waliyonayo wananchi dhidi yake, hana mtetezi kwenye vyombo vya habari anavyoviongoza pamoja na mitandao ya kijamii. Kila anapotamkwa vibaya watu wanashangilia.

Japo baya zaidi, ni mtu anayeamini kwenye kukamata, kutesa na kutweza utu mara tu anapopewa madaraka. Siyo mtu wakushirikiana na jamii bali always anawaza kunufaika kisiasa bila kujali wanaathirika wangapi.

Nimemsikiliza alivyohojiwa BBC kuhusu issue ya Makamu wa Rais, kwa namna alivyojibu kwa jazba na bila kujikita kwenye hoja ni wazi kwamba angekuwa na uwezo waliofungia BBC angaifungia. Waziri kutamka kwamba chombo cha habari kinashabikia mambo ya ovyo kisa wameuliza jambo ambalo ni kinyume na mtizamo wake ni tafsiri ya kiburi cha madaraka.

Kama Taifa naamini hiii interview imetuchafua sana kimataifa......imeonyesha wazi kwamba siyo kwamba vyombo vya ndani vinashindwa kuhoji bali VIKIHOJI WAZIRI ANAWEZA HATA KUELEKEZA ANAYEHOJI AFUNGWE AU AKAMATWE.

Watoto wa viongozi punguzeni ulevi wa madaraka, wazazi wenu wasingekuwa viongozi leo msingeongoza hata kitongoji coz mnakosa qualities.
 
Mhe. Nape Nauye amepata mashambulizi makubwa sana mengi yakiwa yanatokana na historia yake kisiasa. Yapo makosa ya kisiasa ameyafanya na sasa yanamgarimu san...
Muacheni Nape bana!

Nape ni mwanasiasa anenda na upepo uvumao.

Kwamba bado yupo ulingoni ni ushahidi tosha kuwa yupo vizuri.
 
Mkuu hakuna ka-video clip? Lkn hata hivyo asante kwa taarifa hii. Nitamkaanga kwa maneno yake
 
Mhe. Nape Nauye amepata mashambulizi makubwa sana mengi yakiwa yanatokana na historia yake kisiasa. Yapo makosa ya kisiasa ameyafanya na sasa yanamgarimu san..
Nape siyo wa kumuamini hata kidogo.

Ninashangaa sana kama bado Team Msoga wanaendelea kumuamini wakati anajulikana ukigeugeu wake.

Hajawahi kuwatetea wananchi kwenye issue za kuibiwa bando na makampuni ya simu
 
DW kapigwa maswali hadi akaanza kama indirectly kumtisha Sudi, ila Sudi nae akalala naye sahani moja.

Haya mambo hayahitaji jaziba wala vitisho, ukijibu jibu sahihi hautaulizwa maswali mengi.
 
yule ana mizuka hana lolote, utasikia figisu mara bao la mkono....kwenye hoja ni mweupe sana. Nahisi ccm wanajuta sana kimoyo moyo..maana vilaza ni wengi kuliko wajuvi wa mambo 😀
 
Nape siyo wa kumuamini hata kidogo.

Ninashangaa sana kama bado Team Msoga wanaendelea kumuamini wakati anajulikana ukigeugeu wake.

Hajawahi kuwatetea wananchi kwenye issue za kuibiwa bando na makampuni ya simu
Msoga team ndiyo wenye hisa nyingi kwenye hiyo mitandao. Nape anawezaje kuwa kinyume na maslahi yao?
 
Msoga team ndiyo wenye hisa nyingi kwenye hiyo mitandao. Nape anawezaje kuwa kinyume na maslahi yao?
Nina hoja hapa ambazo nimezipata jikoni kabisaa.

Alichokuwa anamfanyia Mkwere si cha kiungwana. Anyways ngoja nilewe kwanza ntarudi kusema
 
Back
Top Bottom