Waziri Ndejembi aagiza kufutwa hati milki ya ardhi Ruvuma

Waziri Ndejembi aagiza kufutwa hati milki ya ardhi Ruvuma

Joined
May 14, 2024
Posts
94
Reaction score
75
WAZIRI wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe. Deogratius Ndejembi amemuelekeza Kamishna wa Ardhi Msaidizi Mkoa wa Ruvuma kuifuta Hati ya Ardhi kwa Bw. Steven Mapunda ambaye alikabidhiwa bila kufuata utaratibu katika Kijiji cha Mwanamango Manispaa ya Songea.

Mhe. Ndejembi ametoa agizo hilo Septemba 22, 2024 baada ya kufika katika kijiji hicho kutatua mgogoro wa ardhi uliodumu kwa muda mrefu.

Mgogoro huo unamuhusisha Bw. Mapunda aliyemilikishwa ekari 45 za mashamba ya wananchi wa Mwanamango bila kuwalipa fidia kama sheria inavyoelekeza.

“Ninamuelekeza Kamishna wa Ardhi wa Mkoa kufuta hati ya Bw. Mapunda kwa sababu wananchi hawakushirikishwa na wala hawakulipwa fidia. Kwa hiyo maamuzi yangu leo ni kwamba hiyo hati iondolewe papimwe tena na wananchi wamilikishwe maeneo yao kwa mujibu wa sheria.

Soma Pia: Waziri Ndejembi Ataka Watendaji Ardhi Kuondoa Urasimu na Kutoa Hati kwa Wakati


"Na hapa ninafahamu ni wananchi takribani 30 ambao maeneo yao yalipimwa bila ridhaa yao na bila fidia. Hivyo ninaelekeza wamilikishwe maeneo yao,” amesema Mhe. Ndejembi.
 
WAZIRI wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe. Deogratius Ndejembi amemuelekeza Kamishna wa Ardhi Msaidizi Mkoa wa Ruvuma kuifuta Hati ya Ardhi kwa Bw. Steven Mapunda ambaye alikabidhiwa bila kufuata utaratibu katika Kijiji cha Mwanamango Manispaa ya Songea.

Mhe. Ndejembi ametoa agizo hilo Septemba 22, 2024 baada ya kufika katika kijiji hicho kutatua mgogoro wa ardhi uliodumu kwa muda mrefu.

Mgogoro huo unamuhusisha Bw. Mapunda aliyemilikishwa ekari 45 za mashamba ya wananchi wa Mwanamango bila kuwalipa fidia kama sheria inavyoelekeza.

“Ninamuelekeza Kamishna wa Ardhi wa Mkoa kufuta hati ya Bw. Mapunda kwa sababu wananchi hawakushirikishwa na wala hawakulipwa fidia. Kwa hiyo maamuzi yangu leo ni kwamba hiyo hati iondolewe papimwe tena na wananchi wamilikishwe maeneo yao kwa mujibu wa sheria.

"Na hapa ninafahamu ni wananchi takribani 30 ambao maeneo yao yalipimwa bila ridhaa yao na bila fidia. Hivyo ninaelekeza wamilikishwe maeneo yao,” amesema Mhe. Ndejembi.
Kumekuchaa!!
 
Kwa ambaye hajawahi kununua ardhi vijijini akajua fitna za wanakijiji atasema haki imetendeka, siku utakapo peleka pua yako vijijini ndio utajua sura halisi za wanakijiji, wanakuuzia wenyewe huku roho zinawauma , kesho utasikia mwekezaji tapeli
Waziri kasema mnunuzi hakufata sheria, kwenye kununua Nyumba mashamba gari lazima utafate utatatibu wa kisheria na siyo kununua kienyeji tu na kulipana pesa uchochoroni.
 
Back
Top Bottom