Waziri Prof. Palamagamba Kabudi, jitokeze na ulieleze Taifa hii mikopo na misaada ya pesa za kupambana na COVID-19 zimetumika vipi

Waziri Prof. Palamagamba Kabudi, jitokeze na ulieleze Taifa hii mikopo na misaada ya pesa za kupambana na COVID-19 zimetumika vipi

Alexander The Great

JF-Expert Member
Joined
Aug 28, 2018
Posts
4,509
Reaction score
23,653
Habari Wana Kijiji,

Binafsi nimeshtuka sana, mpaka nlidodosha bakuli langu la pombe ya kienyeji jana usiku nlipokuwa kilabuni baada ya kupata habari hizi za kuogofya na kushtua.

Habari zenyewe ni baada ya kuambiwa wale jamaa zetu wanaotupa misaada kama taifa, misaada wanayotupa ya kila mwaka tena bila wao kujisifia au kutuzodoa, Wabunge Wa Bunge La Ulaya, ambao Prof Kabudi uliwaita "WAHUNI/WAJINGA" kumhoji Mwenyekiti Wao Wa Bunge kuhusu vigezo alivyotumia kuipa Tanzania msaada ya "€ 27 MILLION" kwaajili ya kupambana na ugonjwa wa Covid-19.

Wakati Serikali ya Tanzania (Ikiongozwa na Mh Rais) kutangaza na kutoa "MAHUBIRI NA MAWAIZA KWA RAIA WAKE" kwamba Tanzania haina ugonjwa huo. Ugonjwa huo ni wa kishetani.

Wabunge Wa Ulaya walikuwa na "HAKI YA KUMHOJI MWENYEKITI WAO" kuhusiana na hizo hela, kwasababu ni hela za walipa kodi wao Ulaya. Hela hizo hawajazokota. Waliwakamua walipa kodi wao. Hela hizo sio kwamba hawakua na kazi nazo, ila kutokana na upendo na heshima waliamua kutupa.

NOTE THAT: Wabunge wale hawakui hoji Tanzania wala hawajakuku hoji wewe kama Waziri Wa Mambo Ya Nje Wa Tanzania. Walimhoji Mwenyekiti Wa Bunge lao.

"MASHARTI YA KUPEWA MSAADA NA MIKOPO" yanajulikana ni lazima "UOMBE KWA KUTOA SABABU ZA MSINGI". Kwa hiyo, sisi kama taifa (Kupitia kwa Wizara Ya Mambo Ya Nje) tuliomba na tulitoa sababu za msingi mpaka kupewa ule msaada na mikopo wa kupambana na Covid-19.

Sasa, uliowaita "WAHUNI/WAJINGA" na kuwatisha kwamba "TANZANIA HAIJAWAHI KUSHINDWA VITA YOYOTE", na wala "HAIJAWAHI KUPIGISHWA MAGOTI KWAAJILI YA MISAADA".

Wameamua kutoa "MAFIGA" na "KUMWAGA CHUNGU CHA MBOGA". Natumai umefurahi sasa kwa ujeuri/ukaidi na dharau uliowafanyia. Sisi kama raia hatukupendezewa kabisa. Sifa ya mtanzania yoyote huwa inajulikana Ukarimu/Heshima/Ukweli/Urafiki/Upendo.

Turudi kwenye mada yangu,

WAHUNI/WAJINGA (Kama ulivyowaita)" wametoa "LIST YA MIKOPO/MISAADA" ambayo sisi kama taifa "TULIOMBA (Narudia tena kwa herufi kubwa TULIOMBA" ili tuweze kupambana na Covid-19. Hawajakurupuka usingizini na kuamua tu kutupa hio misaada. Tuliomba.!!!

Hii kama taifa ni kujivisha "JOHO LA UONGO/UTAPELI NA KUTOKUA WAAMINIFU". Kuomba misaada na mikopo kwa kutumia sababu zisizo za kweli.

BAADHI ya hiyo Mikopo na msaada yenyewe ya kupambana na Covid-19 kama ifuatayo;

1) € 27 Million - Kutoka kwa EUROPEAN UNION (Msaada)

2) $ 143 Million - Kutoka kwa INTERNATIONAL MONETARY FUNDS (Mkopo Mwezi June).

3) $ 3.4 Million - Kutoka kwa WORLD BANK (Mkopo Mwezi September).

4) $ 50.7 Million - Kutoka kwa AFRICAN DEVELOPMENT BANK (Mkopo Mwezi October).

5) $ 11 Million - Kutoka kwa GLOBAL FUND (Mkopo).

KWA UNYENYEKEVU MKUBWA mimi Alexander The Great natoa wito, utoke hadharani na kutupa MAELEZO NA SABABU ZA MSINGI za;

A) Kwanini tuliomba msaada na mikopo ya matrillioni kwa ajili ya kupambana na Covid-19. Wakati Rais alihubiri na kutoa mawaiza kwamba hatuna huo ugonjwa?

B) Hizo hela zilitumika vipi? Na madeni yatarudishwa vipi? Kwa kodi zetu walalahoi?

C) Kwanini uliwatukana na kuwadharau wanaotupa misaada bila sababu ya msingi?

D) Kwanini hujaandika barua ya kuachia nafasi yako kwa maslahi ya taifa?

Ahsante, natumai utaita PRESS YA WAANDISHI WA HABARI WA NDANI NA NJE kutoa maelezo na majibu ya malalamiko yangu.
 
Kama zile Trillion 1.5 hazina jibu mpaka leo sidhani hela hizo watakupa majibu maana ndio hela wanazotumia kununulia wapinzani alafu wananchi ndio walipaji.

Nchi hii jibu sahihi ni kuwatoa majambazi hawa CCM utaona zaidi ya haya.
 
Kama zile Trillion 1.5 hazina jibu mpaka leo sidhani hela hizo watakupa majibu maana ndio hela wanazotumia kununulia wapinzani alafu wananchi ndio walipaji.

Nchi hii jibu sahihi ni kuwatoa majambazi hawa ccm utaona zaidi ya haya.
Kijijini kwetu viongozi wa CCM wa Kata/Vitongoji wanakaa vikao week sasa kujadili jinsi gani kuongeza ushuru ili serikali ipate hela. Serikali haina hela.

Mazao ushuru unapadishwa. Magari ushuru unapandishwa. Kuku sasa hivi wamewekewa ushuru wa sh 500. Bado ushuru wa "KICHWA" kurudishwa.
 
Anajitokeza na kujitutumua kusema Tanzania ni taifa huru liheshimiwe na mabeberu, haya mabeberu yanataka breakdown ya hela zao zilitumika vipi. Mbona umekula kona mkuu. Kimyaaa kama haupo vile 🤣 🤣 🤣
 
Kama zile Trillion 1.5 hazina jibu mpaka leo sidhani hela hizo watakupa majibu maana ndio hela wanazotumia kununulia wapinzani alafu wananchi ndio walipaji.

Nchi hii jibu sahihi ni kuwatoa majambazi hawa CCM utaona zaidi ya haya.
Utakapo kuwa tayari niwekee na mimi nafasi tuyafurumushe sote
 
Hili swali ungelielekeza kwa waziri wa fedha ndio mahali pake.
 
Na kuna wengine walifanya kazi ya kuhudumia wagonjwa wa covid-19 lakin malipo yao ni kichekesho yan kweli sijui kama serikali inajua watu hawa walikuwa wanalipwa sh. Ngapi kwa siku sababu malipo yao baadhi yao malipo yao ni kichekesho wakati wengine ni kicheko. Serikali ifuatilie katika vyake ambavyo watu walokuwa wakiwahumia hao wagonjwa kuna dhuluma nyingi zimefanyika.
 
Bado wana kesi ICC na balozi zote za Ulaya na serikali zao hazitambui matokeo ya uchaguzi.

Hii kazi ya Waziri wa mambo ya Nje kipindi hiki ni ngumu kuliko ukulima wa jembe la mkono.
Kha! kha! nimecheka utadhani mazuri. Wizara ile aliimudu Hayati Mahiga aka Mnyalukolo, huyu wa sasa ni mropokaji tu.

Sent from my TECNO WX3 using JamiiForums mobile app
 
Kha! kha! nimecheka utadhani mazuri. Wizara ile aliimudu Hayati Mahiga aka Mnyalukolo, huyu wa sasa ni mropokaji tu.

Sent from my TECNO WX3 using JamiiForums mobile app
Huyu alimfanyia fitna kubwa Mahiga (RIP) aondolewe pale, alimwambia jiwe kuwa ile wizara akipata mtu anaejua sheria atasimamia vizuri mikataba ya madini na kuwa Mzee Mahiga hajui sheria anampotezea mapato.
 
Tanzania tulipewa $143M kupambana na COVID-19 kutoka IMF June. September tukakopa $3.79M kutoka WB kwa ajili ya ‘laboratory diagnosis & management of COVID-19 cases’, Oktoba tukaongeza mkopo wa $50.7M kutoka AfDB kupambana na COVID-19 ambayo ILIFUKUZWA. Pia kuna €27 millions toka EU. Fedha tulifanyia nini?

Bila shaka pesa zote hizi hawa wahuni wamezitafuna. Ndiyo sababu baadhi ya Watanzania wanataka tuwekewe vikwazo vya kiuchumi maana hata tunachokipata kama Nchi wahuni wanatafuna kimya kimya.
 
Back
Top Bottom