Waziri Profesa Mkenda, acha kutumika kuua Viwanda vya ndani vya Mbolea

Ndo maana akamtumbua yule KAIMU MENEJA??

Nchi hii ni deal zinapigwa kila mahali

Sent from my Moto E (4) using JamiiForums mobile app
Labda alijua atamletea kauzibe. Huyu Waziri mwanzoni alionekana Kama anaupiga mwingi lkn huku mbele mbele nahisi labda Kuna maagizo kapata toka mahali Fulani maana haeleweki nae Sasa.
 
Mbolea itaadimika kipindi Cha msimu wa kilimo.
 
Mkuu kuwa mkweli wa nafsi yako. Maadam umeleta mada hii, ni vyema ungesema ukweli ni aina gani ya mbolea inatengenezwa Mijingu na kama ni hiyo tu mbolea ndiyo inahitajika kwa mazao yote Tanzania? Eleza ukweli ni viwanda gani vya mbolea vipo nchini. Otherwise tuache utani na maslahi binafsi kwa maisha ya watanzania zaidi ya asilimia 70.
 
Fucken sana! Huko ubaruku Mbarali Mbeya, mbolea msimu huu usio wa kilimo ni 80000+ halafu kilo ya mchele 8000---1300. Nazan msimu wa shamba itakuwa laki.

Safi sana kundi la wakulima ndoi moja kati ya makundi yanayo vaaga sana tisht za kijani kipndi cha uchaguzi pambaneni na hali zenu
 
Ukizingatia paragraph kwenye uandishi wako utaeleweka vizuri!
Hapana.

Siyo hivyo tu. Hii ni mada muhimu sana anayoiwasilisha huyu mkuu, halafu inaonyesha wazi hajui anachokianzishia mada kwa undani zaidi. Ilitakiwa atafute uhakika wa mambo anayoonyesha kuyazua hapa, badala ya kuyaandikia bila ya kujuwa uhalisia wake ni upi.

Mimi sihoji uwezekano wa hujuma ndani ya wizara na sehemu zingine, lakini ningependa kuonamleta mada akiweka taarifa inayoonyesha angalau uonekano wa mazingira ya hujuma. Hakufanya hivyo. Hiyo ya maspika huko mashambani sio ushahidi wa waziri kuwa 'promoter' wa hizo biashara za mbolea za washindani.

Katika mawaziri ninaoamini kwa sasa hivi ndani ya serikali hii, ambao wameshishikilia wizara muhimu kama hii ya Kilimo, na kuipa uzito unaostahili ni huyu Prof. Mkenda na Naibu wake. Siamini kamwe kwamba huyu waziri ndiye ageuke mara hii na kuanza kuhujumu wizara na waTanzania.
Sikubali kabisa kwa haya yaliyowasilishwa hapa.
 
Maprofesa wetu wakiwa vyuoni wanakuaga na akili sana lakini wakishaingia kwenye siasa tena hizi za maji taka wanakuwa kama darasa la nne tu la mkoloni, ndiomaana musukuma anasemaga wasomi hawana akili , hivi Profesa mzima anafukuza watumishi pale wizarani kwake ati anadai wanamhujumu anasikika sana Bashe naibu Waziri kuliko yeye, yaani ukishaona mtu ana thinking ya namna hii ujue hamna kitu hapo.
 
Kuna watu walisema huyu ndo awe waziri wa fedha
 
Mbolea ipi hyo mkuu nahisi Kama Kuna mtu anamhujumu maza kwa kweli maana Kuna ambazo bei yake zipo chini na zinatengenezwa nchini lkn hazipewi kipaumbele
"...bei yake zipo chini na zinatengenezwa nchini lkn hazipewi kipaumbele"!

Haiingi akilini hata kwa sekunde moja kuamini haya yaliyoandikwa hapa, lakini inawezekana kuna sababu kwa nini unataka watu waamini hivyo hata bila ya maelezo yoyote juu yake.

Kama wewe ni mkulima mzoefu kama ulivyoandika, uanatumia mbolea ambazo tayari unajuwa hukupa mavuno bora kabisa, tena bei yake ni nafuu, na zinatengenezwa hapa hapa nchini.

Mara anaingia waziri mpya kwenye wizara, anaamua ku'promote' mbolea ambayo ni ghali, toka nje, na pengine huna uzoefu nayo, na wala waziri hakuelezi chochote juu ya ku'promote' hiyo mbolea mpya!
Na wewe kama mkulima mzoefu, utanyamaza tu na kulalamikia pembeni? Huyu waziri bila sababu yoyote atakuja kukulazimisha ununue ile mbolea ya ghali?

Wewe una maslahi fulani ndani ya mfumo wa wizara hiyo ambayo yameguswa na waziri.

Kama si hivyo, basi tulizana utueleze malalamiko yako hasa ni juu ya kitu gani!
 
Kwenye maelezo yangu namba 15 humu nmeweka clip ambayo waziri anataja bei ya mbolea kwa brand ambazo zinatoka kwenye hiyo kampuni ya Morocco kwanini. Msimamizi mkuu wa hiyo kampuni kwa hapa nchini anaitwa Dr Mshindo Msolla ambae nae ana vinasaba na Wizara ya kilimo miaka ya nyuma. Wewe hapo inakuletea picha gani mkuu
 
Safi sana kundi la wakulima ndoi moja kati ya makundi yanayo vaaga sana tisht za kijani kipndi cha uchaguzi pambaneni na hali zenu
Kwa uchaguzi huu wa juzi wangehesabu Kama Zambia asaivi hii nchi ingekua ya Asali na Mana lkn tulipigwa kwa kila namna, tusinyoosheane vidole
 
Mimi sijaongelea kwa minajili ya aina ya mbolea nmesema Ile waziri kutaja brand ya mbolea ya kampuni moja na price huoni Kama amewapandisha chati hao. Swali langu ndo lipo hapo
 
Mkuu 'Shark', HESHIMA kwako.

Kwanza niseme ya kwamba nilipoandika mchango wangu ulioujibu hapa nilikuwa sijaiona hiyo 'clip' uliyoiweka hapo #15.
Ninaheshimu sana mtu anayetoa ushahidi kwa jambo ambalo analiandikia kama wewe ulivyofanya hapa. Jukwaa hili la JF lingekuwa na heshima kubwa sana linapoendesha majadiliano yenye ushahidi, kama hivi ulivyofanya wewe.

Baada ya kuyasema hayo hapo juu, inanipa tatizo sana sasa kumtetea huyu Prof. Mkenda, ambaye kwa hakika niliweka matumaini makubwa juu ya utendaji wake katika wizara hiyo muhimu sana katika maendeleo ya nchi yetu, na hasa katika kuinua maisha ya waTanzania wengi wanaojishughulisha na kilimo.

Kwa hakika hapa Prof. hata sijui nimweleze vipi, ili isionekane kwamba anajiweka katika ku'promote' biashara za kampuni binafsi. Huyu, ingekuwa ni nchi yenye uhuru na haki, ingetakiwa kuwa 'challenged' hata kisheria kwa tabia mbovu ya aina hii anayoonyesha waziwazi.

Hata hivyo, maadam hajazuia mbolea nyingine ziwepo sokoni, uamzi ni wa mkulima binafsi.

Nirudie tena, nakushukuru kwa mchango wako huu wa maana kubwa sana.
 
Thanx mkuu for appreciation hii sekta ya wakulima yenye 70% ya wananchi wote ni Kama inahujumiwa sana kila Kona, hakuna zao ambalo utatamani ukalime ili uwe nawe na hela bila mwanasiasa kuingiza mkono wake. Korosho ilikua angalau linasaidia kumuinua mwananchi mkulima lkn likaingiliwa. Naamini Prof Mkenda Kama aliongea vile sio kwa kukuhujumiwa anaeza badilisha maneno yake ili wakulima tuwe na ahueni. Mpaka sasa bado kampuni ya Moroco inatumia maneno yake Kama promo kwa bidhaa zao zenye bei ya juu.
 
Kama ni kweli basi inabidi TAKUKURU ichunguze mambo haya.
 
Moja ya kazi za usalama wa taifa ni kufutilia uhujumu wa namna hii (economic sabotage). Kilimo, na mnyororo wake wa thamani, kinaajiri zaidi ya asilimia 70 ya watanzania. Itasikitisha sana kama itaruhusiwa kuchezea hii sekta kiduwanzi hivyo,
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…