Waziri Silaa awatia mbaroni matapeli wa ardhi inayomilikiwa na NSSF Tuangoma Manispaa ya Temeke, waliwekewa mtego wa wateja

Waziri Silaa awatia mbaroni matapeli wa ardhi inayomilikiwa na NSSF Tuangoma Manispaa ya Temeke, waliwekewa mtego wa wateja

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Joined
Apr 18, 2017
Posts
3,984
Reaction score
13,760

Waziri wa Ardhi Jerry Slaa amewatia mbaroni watu watatu wakidaiwa kuwa ni matapeli sugu wa Ardhi Wilayani Temeke ambao wamekuwa wakiuza maeneo kadhaa yanayo milikiwa na Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF) na kufanikiwa kujipatia Mamilioni ya fedha.

Jerry Silaa amefanikiwa kuwakamata watuhumiwa hao kwa kushirikiana na NSSF baada ya kuweka mtego kama wanunuzi wa ardhi kwa malipo ya Shilingi Milioni nane.

Kufuatia tukio hilo, Jerry Silaa amewataka wananchi kuacha kununua Ardhi chini ya Viongozi wa Serikali za mitaa sambamba na kuwazuia wenyeviti wa Serikali za mitaa kuacha kuuza Ardhi kote nchini

"Ninamtaka Kamishna wa Ardhi nchini kukamilisha mchakato wa kupata stakabadhi ya manunuzi ya Ardhi ambayo itatumika nchi nzima" amesema Waziri Silaa.

Kwa Upande wake Meneja Miliki wa NSSF Geoffrey Timoth, amesema NSSF Ilipokea taarifa ya uwepo wa matapeli wanaohujumu maeneo ya mfuko kwa kuyauza, huku wengine wakivamia maeneo hayo kwa kuamini wataachiwa maeneo hayo na kuongeza kuwa wataanza zoezi la kuvunja nyumba zilizojengwa na wavamizi hao.

Naye Mwenyekiti wa Serikali ya mtaa ya Malela kata ya Tuangoma, Wilaya ya Temeke Owing Henry Mkinga, amesema matukio hayo ya utapeli ni ya muda mrefu na yamekuwa yakifanywa na baadhi ya wajumbe wa Serikali ya mtaa, ambapo pia alitumia muda huo kukemea vitendo vinavyofanywa na baadhi ya Viongozi wasio waaminifu

Huu ni mwendelezo wa oparesheni zinazofanywa na Waziri wa Ardhi Jerry Slaa katika maeneo mbalimbali nchini kwa lengo la kutatua migogoro ya ardhi iliyokithiri.
 
Tanzania yoote ina matatizo ya ardhi, waziri hawezi kuzunguka tanazania nzima

Tujenge mifumo tuache maigizo. Tunapoteza rasilimali nyingi sana na muda sababu y akushindwa kujenga mifumo imara

Mifumo imara hawezi kuleta matatizo ya namna hii
 
Njoo Ndachi Nkuhungu broad acre Dodoma uone ujinga unaobebwa na maafisa Ardhi Majizi Magige na kundilake
 
Matapeli wanarudisha watu nyuma, hapo kuna hasara kiwanja chenyewe, kwa aliyejenga majanga na janga lengine ni pesa inayoenda kupotea baraza la ardhi kwasababu hamna atakaekubali matokeo..
 
Sema hapa aliwaweza, na huyo mama alivyojichanganya na wino kwenye kidole 😀
Mushi huko mikocheni naye yamemkuta 😄
Maqna mali za mzee wangu huyo wakisema wambane au wenye mali walitokee zote zitaondoka

Ova
 
Kama wenyekiti wa serikali ya mtaa wanashirikiana na matapeli basi nchi imeoza ila hongera Slaa at least umejaribu kuonyesha unapambana hayo ya kuanzisha mifumo imara waachie mabosi wako liko nje ya uwezo wako
 
Back
Top Bottom