Waziri Ummy Mwalimu: Maduka ya Dawa nje ya hospitali yaliyo ndani ya mita 500 kuondolewa

Waziri Ummy Mwalimu: Maduka ya Dawa nje ya hospitali yaliyo ndani ya mita 500 kuondolewa

Chachu Ombara

JF-Expert Member
Joined
Dec 11, 2012
Posts
6,067
Reaction score
10,938
Leo, Waziri Ummy Mwalimu amesema Maduka yote ya dawa nje ya hospitali yanatakiwa kuwa umbali wa mita 500. Amesema Sheria hii aliipitisha yeye kabla sijaondoka Wizarani na kuongeza kuwa Maduka yaliyo ndani ya Mita 500 ndani ya Hospitali Nchi nzima wanakwenda kuyaondo.

Waziri Ummy amehoji: "Hospitali dawa hakuna, kwanini maduka ya nje dawa zipo? Haikubaliki"

NUKUU
“Ninatuma salamu maduka yote ya dawa lazima yawe mita 500 kutoka ndani ya hospitali, tunakwenda kuyaondoa ifikapo Julai Mosi mwaka huu tulishatoa muda wa kutosha kufikia Juni 30 yawe yameondoka.

“Wamiliki wanafanya kinyume cha sheria nipo na mfamasia Mkuu wa serikali hapa, tulitunga na tulipitisha kanuni maduka yote yawe mita 500 kutoka hospitalini nikaambiwa waziri kuna wengine walipewa leseni kabla, hivyo tumebakisha miezi mitano hakuna cha msalie mtume wala kuomba radhi,”

''Mwananchi anakosaje dawa? Suala hili ni la pande mbili MSD na hospitali na nilishatoa maagizo. Uwepo wa haya maduka yanachangia udokozi wa dawa na yanaondoa imani kwa wananchi kwamba angalau kuna usimamizi mzuri wa dawa vituoni,”


Pia soma


 
Hapo maana yake wagonjwa wameongezewa umbali wa kwenda kuchukua dawa..
Ikitokea dawa ya dharura inahitajika basi ndio uwezekano wa mgonjwa kwenda ahera mapema unavyokuwa Karibu..
Najua wengi watafurahi lakini kuna hatari kwa wagonjwa wa dharura
 
Maduka yote ya dawa nje ya hospitali yanatakiwa kuwa umbali wa mita 500, sheria hii niliipitisha kabla sijaondoka Wizarani, maduka yaliyo ndani ya Mita 500 ndani ya Hospitali Nchi nzima tunakwenda kuyaondoa, Hospitali dawa hakuna, kwanini maduka ya nje dawa zipo? Haikubaliki"

Pia soma

Fikiria vizuri hapo Mhe Waziri! Kuna wakati Hospitali za Serikali hukosa dawa kwasababu ya kukosa fedha au wanapoenda MSD hukosa dawa husika. Maduka mengine ya watu binafsi huwa wanaagiza dawa kutoka sehemu mbalimbali. Hata Kama Kuna watumishi wasio waaminifu ambao huiba dawa na kuziuza kwa maduka hayo, ni kitu gani kitazuia wasiuze au kuiba dawa wakati maduka ya watu binafsi yakiwa mbali na Hospitali?
Pia tukumbuke kwamba maduka haya ya nje ya hospital Mara nyingi huwa mkombozi kwa wagonjwa pindi dawa zinapokosekana wodini, ambapo ndugu hutumwa kwenda kununua dawa husika bila kuchelewa.
 
Maduka yote ya dawa nje ya hospitali yanatakiwa kuwa umbali wa mita 500, sheria hii niliipitisha kabla sijaondoka Wizarani, maduka yaliyo ndani ya Mita 500 ndani ya Hospitali Nchi nzima tunakwenda kuyaondoa, Hospitali dawa hakuna, kwanini maduka ya nje dawa zipo? Haikubaliki"

Pia soma

Huyu Ummy ana matatizo toka mwendazake aondoke.
Hivi is that the most pressing issue kwa Wizara yake?
Aaache kuwa novice!
 
Maduka yote ya dawa nje ya hospitali yanatakiwa kuwa umbali wa mita 500, sheria hii niliipitisha kabla sijaondoka Wizarani, maduka yaliyo ndani ya Mita 500 ndani ya Hospitali Nchi nzima tunakwenda kuyaondoa, Hospitali dawa hakuna, kwanini maduka ya nje dawa zipo? Haikubaliki"

Pia soma

Sasa hilo ni tatizo la maduka ya Dawa au ni tatzo la hospitali?Unataka watu wanyimwe DAWA?au wasiuze DAWA
 
Yaani mambo haya ya kutaka serikali kujaribu ku' micromanage' everything, hata maisha ya watu na waendelee kutaabika kutokana na serikali yenyewe, kutowajibika kuhakikisha hospitali zina dawa za kutosha, sasa wananchi wafanyeje baada ya kukosa dawa hospitalini?? Kama dawa zingekuwa zapatiksns hospitalini, sidhani kama kuna mtu angelazimika kufuatia nje kwenye maduka hayo...Kaazi kwelikweli....
Kwahiyo yakiwa nje umbali wa mita 500 ndio dawa zitakosekana kwenye hayo maduka? Au mimi kuna kitu sijaelewa?
M
 
Mi nafikiri wange focus kwenye kwanini dawa hakuna hospitali. Then wakisha jua tatizo liliko walitatue kama ni wizi basi wahusika wawajibishwe. Kama kweli ni uhaba wa madawa serikali iweke bajeti dawa zipatikane.

Sioni mantiki ya kuyaondoa maduka. Kuna wakati dawa zinakua hamna kutokana na uzembe wao wenyewe basi uo mda hayo maduka hugeuka mkombozi iweje yatolewe?
 
Yakae mita 510 tuone anatatua nini! Je, waziri anamaanisha kwamba duka binafsi la dawa likiwa umbali wa viwanja vitano vya mpira, ndio dawa zitapatikana hospitali?!!

Zipo zahanati hazipo karibu na duka lolote binafsi la dawa huko Bukombe, na bado hazina dawa. Hizi shida ni nini?

Waziri analenga kutatua tatizo gani? Au upeo wa kutatua matatizo yetu umfikia kikomo!!
 
Waziri ni cheo kikubwa sana, Waziri ni kiongozi wa wizara anayezungukwa na kila aina ya resources zinazomuwezesha kufanya kazi zake kwa ufanisi....mpaka kutoa uamuzi maana yake watu wamefikiri na hapo ndio mwisho wamemaliza....
 
Back
Top Bottom