gimmy's
JF-Expert Member
- Sep 22, 2011
- 3,312
- 3,345
Salaam,
Hivi majuzi kulitokea taharuki ya ugonjwa uliosababisha sintofahamu kwa wakazi wa Lindi baada ya kusababisha vifo vya watu kadhaa.
Dalili zilizoonekana kwa wagonjwa ilikua ni pamoja na homa kali,kuumwa viungo vya mwili pamoja na kutokwa na damu puani.
Mwanzoni ugonjwa huu haukuweza kufahamika lakini baada ya uchunguzi kufanyika leo waziri wa afya mh Ummy Mwalimu ameueleza uma kwamba hugonjwa huu unaitwa Leptopirosis.
Kwenye maelezo ya mh Ummy ameeleza kwamba asili ya ugonjwa huu ni kwa wanyama wa porini,lakini wanyama wa porini huweza kuwaambukiza pia wanyama wa majumbani kama paka na panya.
Kwangu kutokutajwa mbwa nimeona huwenda wananchi wakaacha kuchukua tahadhari kwa mbwa jambo ambalo ni hatari.
Ningependa kukazia kwamba kwa wale wanaofuga mbwa watakua wanafahamu kwamba ugonjwa huu ni common zaidi kwa mbwa kuliko hata paka.Mbwa huwa tunawachanja chanzo DHLPP.Hii chanjo huzuia magonjwa matano kwa wanyama na L ni kifupi cha leptopirosis.
Na ni kweli ugonjwa huu huweza kusambaa kutoka kwa wanyama walioathirika kuja kwa binadamu kwa kugusana na majimaji kama damu nk.
Nashauri mh Ummy kama wanaona tatizo hili ni kubwa ni vema wangechanja mifugo DHLPP hasa mbwa na paka kwani wanyama hawa wapo kwenye jamii hivyo huongeza uhatarishi wa maambukizi.
Asanteni.
Hivi majuzi kulitokea taharuki ya ugonjwa uliosababisha sintofahamu kwa wakazi wa Lindi baada ya kusababisha vifo vya watu kadhaa.
Dalili zilizoonekana kwa wagonjwa ilikua ni pamoja na homa kali,kuumwa viungo vya mwili pamoja na kutokwa na damu puani.
Mwanzoni ugonjwa huu haukuweza kufahamika lakini baada ya uchunguzi kufanyika leo waziri wa afya mh Ummy Mwalimu ameueleza uma kwamba hugonjwa huu unaitwa Leptopirosis.
Kwenye maelezo ya mh Ummy ameeleza kwamba asili ya ugonjwa huu ni kwa wanyama wa porini,lakini wanyama wa porini huweza kuwaambukiza pia wanyama wa majumbani kama paka na panya.
Kwangu kutokutajwa mbwa nimeona huwenda wananchi wakaacha kuchukua tahadhari kwa mbwa jambo ambalo ni hatari.
Ningependa kukazia kwamba kwa wale wanaofuga mbwa watakua wanafahamu kwamba ugonjwa huu ni common zaidi kwa mbwa kuliko hata paka.Mbwa huwa tunawachanja chanzo DHLPP.Hii chanjo huzuia magonjwa matano kwa wanyama na L ni kifupi cha leptopirosis.
Na ni kweli ugonjwa huu huweza kusambaa kutoka kwa wanyama walioathirika kuja kwa binadamu kwa kugusana na majimaji kama damu nk.
Nashauri mh Ummy kama wanaona tatizo hili ni kubwa ni vema wangechanja mifugo DHLPP hasa mbwa na paka kwani wanyama hawa wapo kwenye jamii hivyo huongeza uhatarishi wa maambukizi.
Asanteni.