#COVID19 Waziri wa afya wa Uingereza: Corona ni kama mafua tu tutaishi nayo milele

#COVID19 Waziri wa afya wa Uingereza: Corona ni kama mafua tu tutaishi nayo milele

Dam55

JF-Expert Member
Joined
Oct 8, 2015
Posts
5,641
Reaction score
11,958
Waziri wa Afya wa Uingereza @sajidjavid amesema kuwa corona inaweza kuwepo milele hivyo inatubidi tuanze kuiona kama mafua na kujifunza kuishi nayo.

Aidha Javid amesema "inasikitisha lakini ni ukweli kuwa kuna miaka mingine huwa tunakumbwa na wimbi la mafua makali sana nayo huwa yanaua watu pia, ni lazima maisha yaendelee, muhimu ni kuangalia hali na kuchukua tahadhari stahiki, hatuwezi kuendelea kufunga nchi zetu sababu ya mafua.

“Ni muhimu tujipange kama tunavyofanya kwa mafua makali, watu huwa wanapewa nafasi ya kuchanjwa chanjo mara moja kwa mwaka haswa wazee.

“Huenda na chanjo ya Uviko19 ikawa hivyo, mara moja kwa mwaka, hatujui ila ndio mambo tunayotakiwa kuyafanyia kazi" amesema @sajidjavid

FB_IMG_1643047971961.jpg


Screenshot_20220124-211308.jpg


Itakumbukwa kuwa maneno haya aliwahi kuyasema mara Kwa mara hayati JPM kuhusu janga la Corona.
Kwasasa Dunia inaanza kuishi katika mawazo yake.
 
Ni ukweli Atakumbukwa mzee MAGUFULI
Aliyasema na kuyaimba haya popote alipokuwa watu wakakunja shingo
Nina imani kwamba mpaka mwisho watu watacheza mipira na corona yao,
Watafunga ndoa na corona zao
Watakwenda mashambani na corona zao
Ila maisha lazima yaendelee
 
Mara nyingi ukweli unachelewa kujulikana kuliko uongo, hofu na vitisho.

Mwisho wa siku ukweli hujidhihirisha na kuushinda upotoshaji.

Magufuli huenda aliuona na kuongea ukweli kuhusu Corona aliposema gonjwa huu kama mafua tu lazima tuishi nao na maisha lazima yaendelee kama kawaida.
 
Hayati John Pombe Magufuli aliyaseme sana haya maono tena hadharani. Kwa makusudi kabisa nchi za magharibi zilijitenga na kukaa mbali na ukweli huu. Taratibu waliompinga baadhi yao akili zinaanza kuwakaa sawa!.... Kinachoshangaza zaidi ni mwelekeo tuliouchukua kama nchi wa kuchanja watu kwa hiali ya lazima hata pale tunapoona watu wakiandamana kupinga chanjo huko huko majuu.... Haya tuendelee tu kufungua nchi.😡
 
Mara nyingi ukweli unachelewa kujulikana kuliko uongo, hofu na vitisho.

Mwisho wa siku ukweli hujidhihirisha na kuushinda upotoshaji.

Magufuli huenda aliuona na kuongea ukweli kuhusu Corona aliposema gonjwa huu kama mafua tu lazima tuishi nao na maisha lazima yaendelee kama kawaida.
Kabisa mkuu
 
Yule jamaa hakika alikuwa ni mkemia. Ila kwakuwa aliongoza nchi kwenye upinzani mkubwa ukemia wake ulifutwa na wasiokuwa wema kwa maneno kama hajui kiingereza. Elimu yake ya kuungaunga. Leo hii matabibu wa kidunia wanaanza kutibu watu kwa maneno ya aliyedharauliwa. Maneno yake katika tasinia ya afya yameanza kufanana na maneno ya newton kwenye somo la phiskia. Ngoja apumzike kwa amani yohana yusuph barimi ma rock
 
Ukweli lazima usemwe, hii korona imechukuliwa kama a serious public health emergency hata zaidi ya ebola wakati ni self-limiting disease ambayo inahitaji supportive therapy tu hususan kwa wazee..........wao wakaenda kufanya lockdown ambayo imeua uchumi wa dunia. Hii move lazima imechezwa na devil worshipers kwa malengo yao ya gizani........​
 
Anataka kusema ile Covid wimbi la kwanza iliyoanzia pale Wuhan, ikapiga Italy, Spain, Uk, USA nk watu wangeichukulia kama mafua ya kawaida tu kwa rate ile ya vifo?

Kwa sasa ni rahisi kusema hivyo kulingana na measeures za kitalaam, machanjo haya, na watu kuishi kwa tahadhari sana..lakini sikweli ile 1st wave ilivyokuwa inamaliza watu halafu eti ingechukuliwa kama ugonjwa wa kawaida bila measures zozote zile...

Kwa sasa hizi waves nyingine hazina nguvu kulingana na kirusi chenyewe kuwa dhaifu, watu kuishi kwa tahadhari, na michanjo + watu kujua aina tofauti tofauti ya madawa..

Africa Corona haikuwa tishio na tulikuwa na haki ya kuongea maana inawezekana miili yetu na hali yetu ya hewa ilitufavor kiasi cha Corona kutochukua maisha ya watu kivilee japo wapo pia waliokufa na kuumwa serious pia..

Maneno haya ni sawa na kusema ule Ukimwi wa zamani wa 80's na 90's watu wangeuchukulia kama ugonjwa wa kawaida kwa kuwa kwa sasa hauna makali....huku tukisahau watu sasa wanatumia ARV, Condom, na tahadhari nyinginezo ambazo huko nyuma hatukuzijua..

All in All, tumshukuru Mungu kwa kuinusuru dunia na kuwapa maarifa watalaam na watu waliopambana kuhakikisha Corona haina ukali tena...
 
Waziri wa Afya wa Uingereza @sajidjavid amesema kuwa corona inaweza kuwepo milele hivyo inatubidi tuanze kuiona kama mafua na kujifunza kuishi nayo.

Aidha Javid amesema "inasikitisha lakini ni ukweli kuwa kuna miaka mingine huwa tunakumbwa na wimbi la mafua makali sana nayo huwa yanaua watu pia, ni lazima maisha yaendelee, muhimu ni kuangalia hali na kuchukua tahadhari stahiki, hatuwezi kuendelea kufunga nchi zetu sababu ya mafua.

“Ni muhimu tujipange kama tunavyofanya kwa mafua makali, watu huwa wanapewa nafasi ya kuchanjwa chanjo mara moja kwa mwaka haswa wazee.

“Huenda na chanjo ya Uviko19 ikawa hivyo, mara moja kwa mwaka, hatujui ila ndio mambo tunayotakiwa kuyafanyia kazi" amesema @sajidjavid

View attachment 2094406

View attachment 2094408

Itakumbukwa kuwa maneno haya aliwahi kuyasema mara Kwa mara hayati JPM kuhusu janga la Corona.
Kwasasa Dunia inaanza kuishi katika mawazo yake.
Pumzika kwa amani, JPM, mwana Chato, mzalendo wa kweli!
 
Tutaishi nayo na huko mbeleni itaondoka kabisa...
 
Back
Top Bottom