Waziri wa Fedha, Dkt. Mwigulu: Napendekeza Serikali kutumia mifumo ya TEHAMA

Waziri wa Fedha, Dkt. Mwigulu: Napendekeza Serikali kutumia mifumo ya TEHAMA

Nyendo

JF-Expert Member
Joined
Jun 4, 2017
Posts
1,336
Reaction score
4,731
Napendekeza matumizi ya TEHAMA kuwa chaguo namba 1 kwa shughuli za Serikali, mambo yote ya Kiserikali yatumie mifumo ya TEHAMA. Waziri wa Fedha amesema kuwa Matumizi ya TEHAMA yanawezekana na itaokoa gharama kubwa kwa serikali.

Amesema kuwa unakuta mtu anasafiri siku 3 au 4 kwenda kuhudhuria kikao cha masaa 3 au 4 anaacha kuhudumia wananchi wakati angeweza shiriki kikao hicho akiwa mahali popote, au mtu anakusanya kundi kubwa la watu kutoka sehemu mbalimbali na wakati mzungumzaji ni 1 tu mkutano huo ungweza kufanyika kwa kutumia TEHAMA na mambo yakawa sawa.

Amesema Serikali inajenga chuo cha TEHAMA na bado tunaogopa TEHAMA, amesisitiza kuwa matumizi ya TEHAMA hayaepukiki katika zama hizi.

Amesisitiza kuwa mbona Mahakama wameweza kutumia Tehama kwanini Serikali inaogopa TEHAMA?
 
Kama maendeleo ni kuzunguka sana nje ya nchi, hiyo nchi ya Oman kiongozi wao mkuu huwa anafanya ziara wapi?
 
Napendekeza matumizi ya TEHAMA kuwa chaguo namba 1 kwa shughuli za Serikali, mambo yote ya Kiserikali yatumie mifumo ya TEHAMA. Waziri wa Fedha amesema kuwa Matumizi ya TEHAMA yanawezekana na itaokoa gharama kubwa kwa serikali.

Amesema kuwa unakuta mtu anasafiri siku 3 au 4 kwenda kuhudhuria kikao cha masaa 3 au 4 anaacha kuhudumia wananchi wakati angeweza shiriki kikao hicho akiwa mahali popote, au mtu anakusanya kundi kubwa la watu kutoka sehemu mbalimbali na wakati mzungumzaji ni 1 tu mkutano huo ungweza kufanyika kwa kutumia TEHAMA na mambo yakawa sawa.

Amesema Serikali inajenga chuo cha TEHAMA na bado tunaogopa TEHAMA, amesisitiza kuwa matumizi ya TEHAMA hayaepukiki katika zama hizi.

Amesisitiza kuwa mbona Mahakama wameweza kutumia Tehama kwanini Serikali inaogopa TEHAMA?
Waanze na bunge watumie TEHAMA wamejazana miezi 4 kujadili budget ya miezi 12, shame on them
 
Asee Mwigulu sasa nimeanza kumwelewa.
Huyu jamaa anaweza kuwa game changer.
Napenda sana viongozi wa namna hii,siyo waziri anakuja na vitu vya zamani visivyo na tija.
 
Kitengo cha Passport kianze unabeba mi physical documents kibao bila sababu
 
PIA KAPENDEKEZA SASA KIDATO CHA I MPAKA CHA VI HAKUNA KULIPA ADA KWA SHULE ZA SERIKALI. HAPA NAONA MAAMUZI YA KISIASA KUENDELEA KUFIDIDIZA ELIMU. NILITEGEMEA ATATOA KANUNI YA WATOTO WA MAWAZIRI NA MAKADA KUWA LAZIMA WASOME SHULE HIZI, SIO WAO WANAWAPELEKA INTERNATIONAL SCHOOL,
 
PIA KAPENDEKEZA SASA KIDATO CHA I MPAKA CHA VI HAKUNA KULIPA ADA KWA SHULE ZA SERIKALI. HAPA NAONA MAAMUZI YA KISIASA KUENDELEA KUFIDIDIZA ELIMU. NILITEGEMEA ATATOA KANUNI YA WATOTO WA MAWAZIRI NA MAKADA KUWA LAZIMA WASOME SHULE HIZI, SIO WAO WANAWAPELEKA INTERNATIONAL SCHOOL,
Kama ww unauwezo peleka wanao kwenye shule za mawaziri. Kuna wanafunzi wanachaguliwa kidato cha 5 wanashindwa kwenda sababu ya ada
 
Kama ww unauwezo peleka wanao kwenye shule za mawaziri. Kuna wanafunzi wanachaguliwa kidato cha 5 wanashindwa kwenda sababu ya ada
Hizo shule zina walimu!! Wanajaliwa? Si kama shule za kata. Kama wanajali elimu kwa nini walimu wasilipwe mishahara kama ya wabunge, ili walimu wazuri wasikimbie sekta hio
 
Back
Top Bottom