Waziri wa Fedha, Dkt. Mwigulu Nchemba amesema Serikali iko mbioni kupeleka Bungeni pendekezo la chanzo kipya cha mapato kitakachowezesha Wizara ya Ujenzi kupata fedha itakayotumika kusaidia masuala ya dharura.
Dkt. Mwigulu amesema hayo wakati akichangia Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ujenzi kwa Mwaka wa Fedha 2024/2025 ambapo amesema chanzo hicho kitaanza kutumika kuanzia mwaka ujao wa fedha 2024/2025.
“Kuna uhitaji wa bajeti kwa ajili ya marekebisho ya barabara ambazo zimeharibika na tunalifanyia kazi hilo na hivi tunavyoongea tunatarajia tutakapokuja kwenye bajeti kuu tutatoa tamko kuhusu bajeti mahususi ya dharura kurejesha barabara zilizoharibika na tulivyokaa na wenzetu wa Wizara ya Ujenzi wametuamhia kwa upande wa ujenzi inahitajika takribani Tsh. bilioni 700 mpaka Tsh. trilioni 1”
“Kwa upande wa TARURA zinahitajika takribani Tsh. bilioni 300 na uwekezaji uliofanyika katika barabara hizi ni takribani Tsh. trilioni 40 na Serikali haiwezi ikaacha uwekezaji huu ukapotea hivihivi”
Akizungumzia uharibifu wa miundombinu ya barabara uliotokana na mvua za El-Nino zilizoharibu barabara pamoja na athari za kimbunga Hidaya amesema “Nilikuwa namuonea Huruma Waziri mwenzangu Bashungwa alikuwa akifika ‘site’ barabara imeharika Wananchi wamekwama anasema Waziri wa Fedha nimpelekee fedha lakini fedha hizo ambazo zinatakiwa zipatikane kimsingi sio za dharura tunalazimika tukate kutoka maeneo mengine na kwakuwa imekuwa ikijirudia itupe funzo kuwa tunahitaji tupate chanzo ambacho kitakuwa kikijilimbikiza wakati wa amani kiweze kutumika wakati wa dharura”
Pia soma: