Waziri wa Habari na Mawasiliano Jerry Slaa ateua wajumbe 6 wa Bodi ya TTCL

Waziri wa Habari na Mawasiliano Jerry Slaa ateua wajumbe 6 wa Bodi ya TTCL

Mindyou

JF-Expert Member
Joined
Sep 2, 2024
Posts
1,869
Reaction score
4,877
wzr.png

Waziri wa Habari, Mawasiliano, na Teknolojia ya Habari, Mheshimiwa Jerry William Silaa (Mb), ameteua Wajumbe wa Bodi ya Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL) kwa mujibu wa Sheria ya TTCL ya mwaka 2017, Kifungu cha 7(2)(3) kikisomwa pamoja na Kipengele cha 1(1) cha Jedwali la Sheria hiyo.

Uteuzi huu unahusisha wataalamu kutoka sekta mbalimbali, walioteuliwa kwa kipindi cha miaka mitatu kuanzia tarehe 26 Novemba 2024 hadi 25 Novemba 2027. Wajumbe walioteuliwa ni:

Soma Pia: Baada ya Wenyeviti kuondolewa, Waziri Jerry Silaa avunja Bodi za TTCL, Shirika la Posta (TPC) na UCSAF


  1. Bw. Onorius John Njole – Mwandishi Mkuu wa Sheria (CPD).
  2. Bw. Khalfan Salim – Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Zanzibar.
  3. Bw. Mohammed Ame Makame – Mkurugenzi Mtendaji wa Zanzibar Civil Status Registration Agency (ZCSRA).
  4. Bw. Meshack Joram Anyingisye – Kamishna wa Bajeti, Wizara ya Fedha.
  5. Prof. Saudin Jacob Mwakaje – Mhadhiri Mwandamizi, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.
  6. Bi. Kapwete Leah John – Meneja wa Huduma za Sheria, Bodi ya Utalii.
Uteuzi huu unalenga kuimarisha utendaji wa Shirika la Mawasiliano Tanzania kwa kuhakikisha Bodi ina wajumbe wenye weledi, uzoefu, na uwezo wa kuliongoza shirika hilo kufikia malengo yake.
 
Hilo shirika ni shamba la bibi.
 
Ttcl kwanink nguzo.zenu.zinaanguka zinapinda na.hamfanyi chochote. Hivi hamuoni nguzo.zenu.ziko katika hali.mbaya.sana
 

Waziri wa Habari, Mawasiliano, na Teknolojia ya Habari, Mheshimiwa Jerry William Silaa (Mb), ameteua Wajumbe wa Bodi ya Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL) kwa mujibu wa Sheria ya TTCL ya mwaka 2017, Kifungu cha 7(2)(3) kikisomwa pamoja na Kipengele cha 1(1) cha Jedwali la Sheria hiyo.

Uteuzi huu unahusisha wataalamu kutoka sekta mbalimbali, walioteuliwa kwa kipindi cha miaka mitatu kuanzia tarehe 26 Novemba 2024 hadi 25 Novemba 2027. Wajumbe walioteuliwa ni:

Soma Pia: Baada ya Wenyeviti kuondolewa, Waziri Jerry Silaa avunja Bodi za TTCL, Shirika la Posta (TPC) na UCSAF

  1. Bw. Onorius John Njole – Mwandishi Mkuu wa Sheria (CPD).
  2. Bw. Khalfan Salim – Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Zanzibar.
  3. Bw. Mohammed Ame Makame – Mkurugenzi Mtendaji wa Zanzibar Civil Status Registration Agency (ZCSRA).
  4. Bw. Meshack Joram Anyingisye – Kamishna wa Bajeti, Wizara ya Fedha.
  5. Prof. Saudin Jacob Mwakaje – Mhadhiri Mwandamizi, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.
  6. Bi. Kapwete Leah John – Meneja wa Huduma za Sheria, Bodi ya Utalii.
Uteuzi huu unalenga kuimarisha utendaji wa Shirika la Mawasiliano Tanzania kwa kuhakikisha Bodi ina wajumbe wenye weledi, uzoefu, na uwezo wa kuliongoza shirika hilo kufikia malengo yake.
Nawaonea huruma kwa sababu TTCL inakufa mikononi mwao baada tu ya Starlink kutia timu TZ!!
 
Nimeomba huduma ya fiber connection mwezi unaisha sasa, mashirika ya umma ni kansa ya taifa, hakuna wanachoweza kufanya kwa ufanisi.
 
Wanasheria TTCL jamani? Kufanya nini?
Hapo unahitaj watu wa Telecom, Finance, Marketing, Sales etc .

Wakurugenzi wa sheria wanaenda kunywa 'chai'tu hapo😂.

Dhana za kwamba maprof mnawajaza kwenye usimamizi wa mashirika ya umma haujawah kuwa na 'tija' kwa taifa...

Waacheni wafundishe..

Yas na Voda na Airtel kuna 'PhD ngapi?

Shirika lenyewe ' lilishajifia' toka zamani, kwa mwendo huu labda ni 'kulizika' kifamilia zaidi
 
Back
Top Bottom