Waziri wa Masuala ya Afrika Mashariki wa Rwanda awekewa vikwazo na Marekani. Mungu wabariki wazungu, Mungu mbariki Trump!

Waziri wa Masuala ya Afrika Mashariki wa Rwanda awekewa vikwazo na Marekani. Mungu wabariki wazungu, Mungu mbariki Trump!

Wakati nchi za Afrika Mashariki zikiendelea kumpet pet Kagame, masaa machache yaliyopita Wizara ya Fedha ya Marekani imetangaza rasmi kuwawekea vikwazo Waziri wa Mambo ya Afrika Mashariki wa Rwanda Generali James Kabarebe na Msemaji wa M23 Lawrence Kanyuka Kingston kutokana na vita vinavyoendelea Mashariki mwa Kongo.


Wakati Viongozi wa Afrika Mashariki wakiendelea kumlea Kagame ambaye sasa anawachezea kama vitoy Wazungu wameamua kufanya kweli.

Itakumbukwa James Kabarebe amekuwa akitajwa sana kama mtu anayetumiwa sana na Kagame katika kupanga na kufanikisha mipango ya ku destabilise Congo.

Wasiomfahamu General James Kabarebe amewahi kuwa bodyguard wa Kagame kipindi vuguvugu lililosababisha cha mauaji wa kimbari nchini Rwanda mwaka 1994. Pia amewahi kuwa Mkuu wa Majeshi ya Congo baada ya kumsadia Mtutsi .wenzao Raurent Kabila kupindua Serikali ya Mobutu Seseko. Aidha amewahi kuwa Mkuu wa Majeshi wa Rwanda na Waziri kwenye Wizara mbalimbali ambapo kwa sasa anashika cheo cha Waziri wa Afrika Mashariki wa nchi hiyo.


Asante sana Trump. Usiache kumulika hawa Viongozi wa CCM wanaotaka kufanya Uchaguzi bila Reforms.
View attachment 3243253
Ningemkubali angeenda Kumtoa kama Bush alivyofanya Iraq kwa Sadam
 
Viongozi wenu wa hapo Afrika si wanamlea. Nyie Tanzania ndo mlikuwa mnafahamika kwa kumshikisha adabu saivi mmeufyata. Anawakoromea na kuuwa wanajeshi wenu alafu mnamchekea chekea tu.

Acha wazungu wanaojua thamani ya uhai wa mwanadamu waingilie kati.
Mfadhili mkuu wa mauaji ya Waarabu huko Middle East ni nani?
 
Africa bado mnaamini solutions za matatizo yenu zipo kwa Wazungu? Whites toka walipoanza kuja Africa hadi leo hawajawahi kuweka maslahi ya Africa mbele.

Tshikedi juzi wenzake wapo Addis Ababa, yeye kaenda German kulia lia. Wazungu ni wanafiki mno, washaona Congo inagawanyika sasa, wanajifanya kujitutumua kuonyesha wanamuhurumia Tshikedi.
Hao Viongozi wa Afrika walipokutana Addis Ababa, Ethiopia kuna jambo lolote la maana limetokea?

Au walivyokutana Dar, Viongozi wa SADC na EAC kuna lolote la maana walifanya? Au walikunywa juice tu?

Acha Mzungu awe Mzungu maana anajua hakika namna ya kuchukua hatua. Hacheki na Nyani anafanya kweli. Nyie endeleeni kuchekeana na kufurahisha genge.
 
Mi nilidhani utasema ni uongo maana hao 23 na kagame si mnadai wanafadhiliwa na Us.Ajabu umeruka hadi parestina huko,kweli unafiki ni kidonda ndugu.
We hujawazoea Waafrika? Mabingwa wa Conspiracy theories na stori za kusadikika.
 
Viongozi wenu wa hapo Afrika si wanamlea. Nyie Tanzania ndo mlikuwa mnafahamika kwa kumshikisha adabu saivi mmeufyata. Anawakoromea na kuuwa wanajeshi wenu alafu mnamchekea chekea tu.

Acha wazungu wanaojua thamani ya uhai wa mwanadamu waingilie kati.
Mnachekesha sana. Kwamba leo wazungu wanathamini maisha ya mwafrika? Nonsense
 
Kwani nyie Waafrika mnathamini maisha yenu?
Hakuna mzungu mwenye uchungu na maisha ya nwafrika. Miaka zaidi ya 100 walikuwa wakiuza na kununua watumwa kutoka afrika huku wengine wakiuawa kikatili.

Nakushangaeni leo mnakuja kuwasifia hapa. Na huu ujinga ndio unawawafanya wazidi kutuona washenzi
 
..Kagame angekuwa amesababisha Wazungu milioni 6 wakapoteza maisha kama alivyofanya kwa Wacongomani sidhani kama Wazungu wangempa second chance.
Hakuna Wacongo milioni 6 waliopoteza maisha kwa sababu ya Kagame. Putin amesababisha vifo vya zaidi ya watu laki moja Ukraine lakini Trump amempa kila kitu.
 
Back
Top Bottom